Quantcast
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live

MAJAMBAZI SITA YAKAMATWA KWA MAUAJI YA AFISA WA POLISI DAR

JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam limewakamata majambazi sugu sita waliohusika kumuua Afisa wa Polisi ASP Elibariki Pallangyo, aliyekuwa akifanya kazi katika kikosi maalum cha kupambana na majambazi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Kamishna wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam,Suleiman Kova ambapo alisema kuwa majambazi hao wanaongozwa na Omary Salehe maarufu kama Bonge Mzito walifanya tukio hilo Agosti 4 mwaka huu nyumbani kwa Marehemu huko Yombo.

Kova amewataja majambazi hao kuwa ni Omary Salehe (39), Saidi Saidi Mzee (37),Rashid Waston(21),Ramadhan Salum (38),Bakari Salim Rashid (38), na Hamisi Hamisi (24) ambao wote walikubali kuhusika katika mauwaji hayo kwa makusudi.

Amesema kuwa majambazi hao walienda kwa ASP Pallangyo na kumvamia usiku wa manane akiwa amelala na familia yake na kumuua mbele ya familia nzima ikishuhudia.

Anaongeza kuwa mtuhumiwa namba moja Bw Salehe alikutwa na bastola aina ya Revolver iliyofutwa namba na baada ya kuhojiwa alidai kuwa silaha hiyo ndiyo iliyotumika katika tukio hilo.

Kamishna Kova amesema mtuhumiwa huyo alijaribu kuwa toroka Polisi kwa kuwadanganya kuwa ameficha silaha nyingine mahali na kutaka kukimbia lakini polisi walimuwahi na kumpiga risasi iliyopelekea akutwe na umauti.

"Mtuhumiwa mwingine huyu  Waston tumemkamata na silaha aina ya Shortgun iliyokatwa mtutu ambayo waliitengeneza kihenyeji ikiwa na risasi nne na betri nne zilizounganishwa kwaajili ya kulipua baruti,"amesema Kova

Katika tukio lingine Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine saba wa ujambazi wanaojihusisha na kuratibu matukio ya uvamizi wa vituo vya polisi pamoja na ugaidi ambao watano kati yao ni familia moja ya ukoo wa Ulatule.

Kamanda Kova amesema kuwa watuhumiwa hao wanahusika na matukio ya kupanga na kuratibu uvamizi wa vituo vya polisi ambapo pia wamekuwa wakiendesha kambi za mafunzo huko mkoani Morogoro kwa kutumia fedha walizokuwa wakijipatia kwa njia ya udanganyifu.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Siad Mohamed Ulatule (67),Ramadhan Ally Ngande(29),Hamis Mohamed Salum Simba Ulatule (51),Ally Mohamed Salum Simba Ulatule (65),Nassor Suleiman Ulatule (40),Seleman Abdallah Salum Ulatule (83) na Said Abdullah Chambeta (40).

"Jeshi la polisi limefanya operesheni hii kuhakikisha tunakomesha kabisa vitendo vya uvamizi wa vituo vya polisi pia tuna lengo la kuwaondolea wananchi hofu ya vitendo vya kigaidi nchini,"amesema Kova.


HATIMAYE VIJIJI VINNE WILAYANI HANANG’ VIMEPOKEA HATI ZA HAKIMILIKI ZA KIMILA ZA ARDHI‏‎.




Image may be NSFW.
Clik here to view.

   Mmoja kati ya wanakijiji waliopokea hati ya hakimiliki ya ardhi iliyotolewa Wilayani Hanang' na kudhaminiwa na shirika la Oxfam chini ya  shirika la Ujamaa Community Resource  Team(UCRT).



  Mgeni rasmi wa hafla hizo katibu tawala wa Wilaya ya Hanang’ John Gabriel akizungumza kabla ya kukabidhi rasmi vyeti.


 Baadhi ya wanakijiji wa Wilaya ya Hanang' waliohudhuria mkutano huo.


  Hawa ni mabinti wa kibarbaig waliokuwa kivutio kutokana na mavazi yao na moja kati ya waliotoa burudani na kufanya mkutano huo kuwa wa kipekee

 Wanakijiji wakifuatilia kwa makini mkutano huo wa kutoa hati za hakimiliki za ardhi.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
 Wananchi na viongozi wa Serikali ya kijiji  wakipitia kwa makini hati za hakimiliki za kimila za ardhi.


Sherehe zilipambwa na ngoma ya wa-Barbaig

 Hizi ndizo hati za haki miliki za ardhi zilizotolewa kwa vijiji vinne Wilayani Hanagh.




Image may be NSFW.
Clik here to view.
 Wananchi na viongozi wa Serikali ya kijiji  wakipitia kwa makini hati za hakimiliki za kimila za ardhi.

 Eveline Mirai, afisa ardhi wa wilaya ya Hanang' akizungumza na wananchi kuhusu kuheshimu mipaka inayowekwa kisheria kwa sababu mipaka hiyo inawekwa kwa gharama na wananchi wenyewe wanakuwa wameikubali.





WENYEKITI wa vijiji vinne vya wilaya ya Hanang’ wamepokea hati za hakimiliki za kimila za ardhi ya vijiji vyao baada ya kuwa vimepimwa na wao kupewa mafunzo ya matumizi bora ya ardhi.

Zoezi hilo lilisimamiwa na kufadhiliwa na shirika la
Oxfam chini ya  shirika la Ujamaa Community Resource Team(UCRT).

Katibu tawala wa Wilaya ya  Hanang’John Gabriel,amekabidhi hati hizo akimuwakilisha mkuu wa wilaya hiyo kwenye mkutano uliofanyika katika kijiji cha Mureru na kuhudhuriwa na wakazi zaidi ya 100 kutoka katika vijiji hivyo ambavyo ni Mureru, Ming'enyi, Dirma na Gehando.

Gabriel amesema hiyo itasaidia mtu kujua mipaka ya eneo lake hivyo hataweza kudhulumiwa ardhi kirahisi.

"Mara nyingi wakina mama ndio wanaothitika zaidi kwanihuwa wanakosa haki zao pale mume anapofariki, ananyanganywa mali zote ikiwa ni pamoja na ardhi wakati anaachiwa watoto awatunze,lakini wanapokuwa na hati za hakimiliki hakuna mtu anayeweza kuwapokonya kirahisi,"anasema.

Akizungumza kwa niaba ya wenyekiti wa vijiji hivyo,Mbisha Gicharoda ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Ming’enyi ameyashukuru mashirika ya Oxfam na UCRT kwa kuwapatia elimu ya matumizi bora ya ardhi na kuwasaidi kupata hati za hakimiliki za ardhi katika vijiji vyao.

"Sisi kama wafugaji hatukua tukijua thamani ya ardhi yetu lakini sasa tumeamka na tumejua haki zetu,manufaa na umuhimu wa kuwa na cheti cha umiliki wa ardhi"anasema Gicharoda.

Alisema vijiji vyao kupata hati za hakimiliki za ardhi itawasaidia kuwa na eneo la pamoja la malisho na kuwa na nguvu zaidi ya kuilinda ardhi yao na kuisimamia vyema hali ambayo itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi.

Naye afisa ardhi wa wilaya ya Hanang' Bi. Eveline Mirai ameshukuru mashirika ya Oxfam na UCRT kwa kuwasaidia wakina mama wajane kupata hati za hakimiliki za maeneo yao sambamba na kusaidia vijiji hivyo vinne kupata hati za vijiji.

Bi.Eveline amewataka wananchi kuheshimu mipaka inayowekwa kisheria kwani mipaka hiyo imewekwa kwa gharama na wananchi wenyewe.

“Mtakapoheshimu mipaka hatutakua na migogoro ya ardhi tena na wananchi wenye maeneo yao wahakikisha wanapata hati za hakimiliki za maeneo yao ili wayamiliki kisheria,"anasisita.

Aidha meneja wa masuala ya ufugaji kutoka oxfam Laurent Wambura amesema serikali inatakiwa kushirikisha mashirika na wadau mbalimbali wa maendeleo wakati wa ugawaji wa maeneo ya ardhi za vijiji ili kuongeza ufanisi katika sekta ya ardhi.


"Wanapogawa vijiji wakati bado mchakato wa upimaji unaendelea ni hasara kwa mashirika hayo kwani aidha yanalazimika kuanza kazi upya au kushindwa kwa sababu tayari fedha zinakuwa zimetumika na tatizo kwa wananchi linakuwa halijatatuliwa,"amesema Gabriel.


Akizungumzia changamoto amesema ni migogoro ya mipaka katika vijiji pamoja na udhaifu katika uongozi wa serikali ya vijiji ambazo huchelewesha mipango lakini pia kuchelewa kupata ripoti ya matumizi ya ardhi kutoka wizarani.

WIZARA YA UJENZI YAELEZEA MAFANIKIO YAKE KWA KIPINDI CHA MIAKA 10.

 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi, Segolena Francis(kulia), akizungumza na wanahabari Dar es Salaam leo  wakati akimkaribisha Mkurugenzi wa Barabara wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Ven Ndyamkama (kushoto), kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya serikali katika sekta ya ujenzi kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015.

 
 Mkurugenzi wa Barabara wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Ven Ndyamkama (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo , kuhusu mafanikio ya serikali katika sekta ya ujenzi kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa wizara hiyo, Segolena Francis.
Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mkutano huo.


WIZARA ya Ujenzi imesema itashirikiana na Sekta Binafsi
(PPP) kuhakikisha kuwa baadhi ya miradi ya barabara inajengwa na sekta hiyo ili kukamilisha miundombinu ya usafiri nchini.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Barabara katika Wizara hiyo
Mhandisi Ven Ndyamukama wakati akizungumza na waandishi wa habari leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.

Amesema mfano wa mradi wa ushirikiano wa Serikali na PPP ni
barabara ya Dar es Salaam hadi Chalinze ambayo itakuwa na njia sita unatarajiwa kuanza hivi karibuni.


Amesema lengo la Serikali kushirikiana na sekta binafsi ni
kuhakikisha kuwa miradi mingi inakamilika kwa wakati ambapo kwa kipindi chamiaka 10 ya Serikali ya awamu ya nne wamekamilisha ujenzi wa kilometa 5,568 za lami zilizogharimu sh. bilioni 4,090 kati kilometa 17,762 ambazo zilitarajiwa kujengwa.


"Tumejipanga kushirikiana na sekta binafsi katika
utekelezaji wa miradi mingi hapa nchini lakini kwa kuanza ni huu wa Dar es Salaam hadi Chalinze unaotarajiwa kuanza hivi karibuni," anasema.

Pia amesema kilometa 3,873 zinaendelea kujengwa kwa kiwango
cha lami kwa gharama ya jumla ya sh.bilioni 4,533 na barabara zenye urefu wa kilometa 4,965 zimefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa gharama ya shilingi bilioni 29.257 ambapo Serikali inatafuta fedha za ujenzi wa lami.

TANESCO:KUKATIKA KWA UMEME MWISHO OCTOBA 20.


Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi Felchesmi Mramba akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ambapo alieleza  juhudi zinazofanywa na shirika hilo katika kutatua kero ya umeme nchini.






SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendeleza juhudi ya kuboresha  upatikanaji wa umeme nchini kwa kuzalisha megawati 35 katika gridi ya Taifa jana mchana.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi Felchesmi Mramba ameeleza kuwa juhudi za kuhakikisha upatikanji wa umeme unakuwa wa uhakika zinaendelea ambapo megawati 90 zinatarajiwa kuzalishwa wiki hii.

 “Katika kuhakikisha hali ya umeme inarejea kama zamani tunatarajia kuzalisha megawati 70 kupitia mitambo ya Kinyerezi na megawati 20 kupitia mitambo ya Symbion na hivyo kufanya jumla ya megawati 90 hii itapunguza ugumu wa upatikanji wa umeme nchini” alisema Mramba.

Aidha aliongeza kuwa kufikia tarehe 20 Oktoba mwaka huu uzalishaji wa umeme nchini  utakuwa wa kutosha  kutokana na jitihada  mbalimbali zinazofanywa na Tanesco .

Vilevile alieleza kuwa upungufu wa umeme unatokana  na kupungua kiwango cha maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme kwa asilimia 81.3 na hivyo kupelekea tatizo la kukati kwa umeme mara kwa mara.

 Mramba  ametoa wito kwa wananchi na wateja wa Tanesco  kuendelea kuwa na subira katika kipindi hiki cha upungufu wa umeme kwa kuwa juhudi madhubuti zinaendelewa kufanywa kuhakikisha hali hii inatatuliwa.

RAIS KIKWETE APOKEA HATI YA UTAMBULISHO WA MABALOZI.




Balozi mteule wa Ubelgiji nchini Tanzania Mhe. Paul Cartier akikabidhi hati ya utambulisho  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete mapema hii leo Ikulu jijini Dar es Salaam.



Balozi mteule wa Hispania nchini Tanzania Mhe. Felix Costales akikabidhi hati ya utambulisho  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete mapema hii leo Ikulu jijini Dar es Salaam.

Balozi mteule wa Msumbiji nchini Tanzania Mhe. Monica Patricio Clemente akikabidhi hati ya utambulisho  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Kikwete mapema hii leo Ikulu jijini Dar esSalaam.

OFISI YA TAKWIMU ZINAONYESHA MFUMUKO WA BEI UMESHUKA KUFIKIA ASILIMIA 6.1


 Mkurugezi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu wa NBS, Ephraim Kwesigabo akizungumza na Waandishi wa habari leo katika ofisi za Takwimu jijini Dar es Salaam kuhusu fihirisi za bei za Taifa kwa mwezi Septemba 2015.


Wahandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo .



OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mfumuko wa bei umeshuka hadi asilimia 6.1 kwa Septemba kutoka asilimia 6.4 kwa kipindi cha Agost 2015.

Akizungumza Dar es Salaam leo Mkurugezi wa Takwimu za Jamii na

Sensa ya Watu wa NBS, Ephraim Kwesigabo ameeleza kuwa kushuka kwa mfumuko wa bei kunachangiwa na kushuka kwa bidhaa za vyakula zinazotumiwa majumbani na kwenye migahawa pamoja na vinywaji baridi.

Amesema mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa Septemba 2015 umepungua hadi kufikia asilimia 9.6 kutoka asilimia 10.2 kwa Agosti 2015.

"Bidhaa za huduma kwa mwaka huu Septemba umepungua ikilinganishwa na kiasi cha bei kilichokuwepo Agost mwaka uliopita ambapo farihisi za bidhaa zimeongezeka hadi 159.4 na kutoka 149.93 Septemba 2014,"anaeleza.

Kwesigabo amesema mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwaka unapima unapima kiwango cha badiliko la kiasi cha bei za bidhaa pamoja na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi.

"Mfumuko wa bei ambao haujumlishi bei za vyakula  na nishati umebakia kuwa asilimia 22 kwa Septemba 2015 kama ilivyokuwa Agost 2015,''anaeleza.

Pia amesema thamani ya shilingi inatafsiriwa katika matumizi ya mlaji wa bidhaa mbalimbali ambapo shilingi ya Tanzania imeonekana kununua bidhaa na huduma zilezile katika vipimo tofauti tofauti.

''Uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma imefikia shilingi 62 na senti 88 kwa Septemba 2015 kutoka Septemba 2010,''anaongeza.

Vilevile Mkurugezi huyo amesema farisihi za nishati na mafuta zimekuwa na mwenendo wa hali ya juu kwa kipindi chote zikilinganishwa na farihisi nyingine.

Amesema mfuko wa bei kwa kipindi cha mwezi mmoja umeongezeka kwa aslimia 0.1 ukiwa umechangiwa na baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula kama vile mkaa,pamoja na huduma za saluni.

MAKAMU MWENYEKITI NCCR-MAGEUZI ASEMA YEYE BADO KIONGOZI

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi(Bara) Leticia Mosore amesema mpaka sasa bado anaendelea kushikilia wadhifa huo kwani kikao kilichoitishwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa James Mbatia hakikuwa na uhalali wa kikatiba.




Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambapo alisema haridhishwi na utaratibu uliotumiwa na Mbatia wa kuitisha kikao ambacho kilihudhuriwa na viongozi wengine  wakuu huku na kumvua madaraka wakati ni kinyume na Katiba ya Chama hicho.

Amesema sheria na utaratibu vilikiukwa kwani Katiba ya NNCR-Mageuzi ya mwaka 1992 toleo la 2014/ibara ya 27 (3)(C) inasema Makamu Mwenyekiti wa Taifa ataweza kuondolewa kwenye madaraka baada ya mapendekezo ya Halimasahauri kuu ya Taifa kwa azimio la mkutano mkuu wa Taifa,kwa zaidi ya nusu ya kura za wajumbe halali watakaodhuria na kupiga kura.

"Lakini pia kanuni za NCCR-Mageuzi toleo la mwaka 2012,umewekwa utaratibu wa kufuatwa kataika kumwajibisha kiongozi au mwanachama, kanuni hizi zinaitwa kanuni za nizamu na usuruhishi za Chama chetu,1996 kwa ujumla wake mashitaka ama malalamiko zidi ya mwanachama au kiongozi lazima yawakilishwe katika kikao cha utendaji cha ngazi husika kupitia kwa Katibu wa ngazi hiyo",ameeleza Mosore na kuongeza

"Mara baada ya kupokea malalamiko kikao husika kitamtaarifu muhusika juu ya malalamiko na kumtaka ajayajibu kwa maandishi katika muda wa majuma mawili".

Amesema lakini Mbatia amekiuka utaratibu huo wa Katiba na kanuni za Chama,mfano kikao anachodai kilikaa Septemba 22 mwaka huu hakikuwa kikao halali kwa mujibu wa Katiba na kanuni za Chama hicho  bali kilikuwa ni kikao cha tathimini ya uchaguzi wa nchi ambao NCCR-Mageuzi inashiriki kinyonge kwa mwavuli wa UAKAWA.

"Hata kama kikao hicho kingekuwa halali bado kingekiuka haki ya msingi ya binadamu ya kupewa muda wa kujitetea,tena kanuni za Chama zinafafanua vizuri kabisa kwamba lazima mwanachama apewe majuma mwaili ya kujitetea kimaandishi ambayo mimi kama Makamu Mwenyekiti sikupewa kimsingi(Right to defend)",anasema Mosore na kuongeza

"Napenda kuufamisha umma na wana NCCR-Mageuzi wasiofahamu kwamba sina imani na kamati ya nidhamu na maadili ya Chama chetu kwa sababu nyingi ambazo ni,Kamati imeundwa na mWenyekiti mwenywe Mbatia,Mwenyekiti wake ni kaka yake aitwaye Thomas Nguma,Katibu ni shemeji yake aitwaye Tibajindela,huku wajumbe wakiwa ni shemeji yake aitwaye Dkt.Kahagwa na dada yake aitwaye Ndera.Je Kamati hii itaweza kutenda haki kwa mtu mwingine zaidi ya Mbatia?".Anahoji Mosore.

"Kwa tafsiri hiyo ya Katiba na kanuni za Chama chetu mimi ni Leticia Mosore mpaka sasa ni Makamu Mwenyekiti halali  wa NCCR-Mageuzi (Bara)kwani ninatambulika na Katiba ya Chama,nilichaguliwa na mkUtano mkuu wa Taifa na wazifa wangu utakoma kuwa kiongozi kwa hiari ama kwa kufuata utaratibu kwa mujibu wa sheria na kanuni za Chama",Anaeleza.

Amesema anasikitishwa na ubakwaji wa demokrasia uliofanywa na Mbatia ambaye ndiye kiongozi wa juu wa Chama kwa maslahi binafsi bila kujali uhai na masalahi mapana ya NCCR-Mageuzi baada ya uchaguzi mkuu wa nchi wa mwaka huu Oktoba 25.

"Masikitikito yangu makubwa ni pale ninapoona kiongozi mkubwa kama Mbatia hadi sasa hajatembelea majimbo yetu ya ngome ya Chama huko Kigoma wala kampeni hazikufunguliwa katika majimbo yetu ya ngome badala yake ameenda kufungulia kampeni huko Vunjo.Je haoni anastahili kuyapa sapoti majimbo haya ya ngome?".Anahoji Mosore.

Amesema amekuwa akituhumiwa na Mbatia kuwa amewalaghai makimishina wa Chama hicho kwa kuwaita katika vikao vya kukihujumu Chama,na kudai kuwa kwa mujibu wa Katiba yeye akiwa kiongozi wa ngazi za juu ana mamlaka ya kukutana na wanachama,viongozi wa Chama,Makamishina na hata Katibu Mkuu mahali popote na kufanya mazungumzo.

Amesema kuhusiana na tuhuma za  kuwa yeye amepanga njama za kumdhuru Mwenyekiti wake James Mbatia anaviachia vyombo vya usalama wa nchi vifanyie kazi  na kuaidi kuwa atatoa ushirikiano wa dhati pale atakapohitajika kufanya hivyo.

"Lakini pia mimi kama Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi(Bara) nashutumiwa na James Mbatia kuwa natumiwa na baadhi ya viongozi wa CCM Katika kukihujumu Chama chetu.Ndugu zangu, wanachama wa NCCR-Mageuzi na watanzania kiujumla,mwenye akili timamu apime na aelewe, Mbatia aliteuliwa ubunge viti maalumu na Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM,je kazi gani aliowafanyia CCM hadi akazawadiwa nafasi hiyo nyeti?Ninamuomba athibitishe na kuwataja viongozi wa CCM ninaoshirikiana nao",Alisema Mosore na kuongeza

"Mimi kama Mkamu Mwenyekiti wa NNCR-Mageuzi(Bara) narudia tena kutoridhishwa na mwenendo wa ushirikiano wa vyama vinavyounda UKAWA.Kwanini NCCR-Mageuzi ipewe mgawanyo wa majimbo machache ambayo ni 12, kati ya hayo majimbo 6 yameingiliwa na CHADEMA hivyo uhakika wa kushinda  katika majimbo hayo ni mdogo sana kwani kura zitagawanyika na hali hii haikubaliki kwani inadhoofisha Chama chetu cha NNCR-Mageuzi"anaeleza.

KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI OMBENI SEFUE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TAKWIMU DAR ES SALAAM LEO.


Image may be NSFW.
Clik here to view.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (kushoto), akihutubia wakati akifungua mkutano wa wadau wa takwimu Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Profesa Adolph Mkenda na Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa. Mkutano huo uliandaliwa na NBS.
.

 Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa akihutubia kwenye mkutano huo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Profesa Adolph Mkenda akizungumza katika mkutano huo.
 Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Dk.Rogers Dhliwayo akizungumza kwenye mkutano huo.
Washiriki wakiwa katika mkutano huo leo.


KATIBU Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amewataka watendaji wa Serikali kutoa takwimu mbalimbali za maendeleo na kuziweka katika mitandao ili wananchi waweze kuziona na kuhoji mipango ya maendeleo iliyofanyika hama kukwama.

Amebainisha hayo leo wakati akifungua mkutano wa wadau wa takwimu ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dar es Salaam leo kwa lengo kukubaliana jinsi ya kushirikiana katika kuhakikisha takwimu za viashiria vya Mpango wa Maendeleo Endelevu zinapatikana kwa wakati.

Amesema takwimu mbalimbali ni lazima zioneshe mipango ya maendeleo iliyofanyika au kumalizika badala ya kuwa siri na kuwafanya wananchi kushindwa kuhoji.

"Takwimu mbalimbali za maendeleo zikiwa wazi itasaidia wananchi kufahamu miradi ya maendeleo iliyopo na iliyokwama jambo ambalo litasaidia kusukuma maendeleo ya nchi" anaeleza Sefue.

Amesema lengo la lengo la kuelimishana juu ya kukamilika kwa utekelezaji wa Malengo ya Milenia (MDGs) na kuanza kwa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu - Sustainable Development Goals (SDGs).

Anaongeza kuwa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia - MDGs ulikuwa ni wa miaka 15 kuanzia mwaka 2000 hadi 2015.

Mpango huu wa MDGs unakamilika mwaka huu na kuanza kwa mpango mpya wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambao pia ni miaka 15 ijayo.

Amesema Tanzania ni nchi ya kwanza kuanza kufanya vikao vya kutekeleza mpango huo wa maendeleo jambo ambalo linaonesha kuwa na kasi ya kuyafikia maendeleo hayo ya dunia.

Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) umehudhuriwa na wadau wa takwimu takribani 100 kutoka Wizara, Idara, Wakala na Taasisi za Serikali, Wadau wa Maendeleo, Wadau wa Sekta Binafsi pamoja na Wadau wa Taasisi za Elimu ya Juu.

Septemba mwaka huu, viongozi wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Rais Jakaya Kikwete walikutana nchini Marekani kwa ajili ya kutathmini utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia – MDGs ambapo ilionekana kwamba kuna baadhi ya malengo yalikuwa yamefanikiwa na mengine hayakufanikiwa.




MAADHIMISHO YA SIKU YA MACHO DUNIANI


IMEELEZWA kuwa takribani watu 945,000 wanasumbuliwa na matatizo  ya kuona kwa viwango mbalimbali hapa nchini idadi yao ikiwa ni mara tatu ya watu wasioona kabisa ambao ni takribani watu 315,000.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii idadi ya watoto wenye matatizo ya kuona duniani ni milioni 19 huku wazee wakiongoza kwa asilimia 82 pia nchi zinazoendelea zinaongoza kwa idadi kubwa ya watu wenye matatizo hayo kwa asilimia 90.

Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Dkt.Donan Mmbando,Katibu Mkuu wa wizara hiyo,ikiwa nisehemu ya kuadhimisha siku ya afya ya macho duniani yenye kauli mbiu ya "Afya bora ya macho kwa wote"yenye lengo la kuhamasisha wadau kushirikana katika kuimarisha  upatikanaji wa huduma za macho katika ngazi zote za utoaji huduna za afya.

Imebainika  kuwa kuwa asilimia 80 ya matatizo yote ya kutokuona yanayoikabili dunia yanachangiwa na sababu zinazoweza kuzuilika.

"Inakadiriwa kuwa takribani watu milioni 285 duniani wana matatizo ya kuona,kati ya hao wenye upofu ni milioni 39 na 246 wana uoni hafifu,"inaeleza taarifa hiyo.

Aidha kutokana na taarifa hiyo sababu zinazosababisha upofu unaoweza kuzuilika hapa nchini na dunia kwa ujumla ni pamoja na mtoto wa jicho,makovu kwenye kioo cha jicho,trakoma,upofu wa utotoni unaotokana unaookana na upungufu wa vitamini A.

Pia maambukizi ya surua,maambukizi ya kisonono kutoka kwa mam kwenda kwa mtoto,upungufu wa upeo wa macho kuona,matatizo ya retina pamoja na ugonjwa wa kisukari na umri mkubwa.

Hata hivyo Wizara ya Afya na ustawi wa jamii inatoa wito kwa Watanzania kupima afya ya macho angalau mara moja kwa mwaka pamoja na wadu na mashirika ya kiserikali na watu binafsi kuwekeza katika rasilimali katika huduma ya macho kwa maendeleo ya nchi.

DKT.BILALI AHUDHURIA KIKAO CHA DHARURA CCM.


Mjumbe wa Kamati Kuu CCM, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungabo wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki na baadhi ya wajumbe wa CCM kusimama na kuomboleza kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Ulanga Mashariki, marehemu Celina Kombani, wakati wajumbe hao walipokutana kwa dharura jijini Dar es Salaam,kujadili kuhusu mrithi wa jimbo hilo

 .

Mjumbe waKamati Kuu CCM, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungabo wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia) akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM, Abrahman Kinana (kushoto) na Mjumbe wa Kamati Kuu, Salim Ahmed Salim (katikati) wakati wakitoka ukumbini baada ya kumalizika kwa kikao cha dharula cha CCM kwenye Ukumbi wa CCM Makao Makuu Lumumba jijini Dar es Salaam,

Mjumbe wa Kamati Kuu CCM, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungabo wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Katibu Mkuu wa CCM, Abrahman Kinana (kushoto) na Mjumbe wa Kamati Kuu, Salim Ahmed Salim (katikati) wakifurahia jambo nje ya ukumbi wa CCM Makao Makuu Lumumba, baada ya kumalizika Kikao cha dharura.

Mjumbe wa Kamati Kuu CCM, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungabo wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (kulia) akiagana na Katibu Mkuu wa CCM, Abrahman Kinana, nje ya Ukumbi wa CCM Makao Makuu Lumumba jijini Dar es Salaam, baada ya kumalizika kwa Kikao cha dharula jana Okt. 10, 2015. Katikati ni  Mjumbe wa Kamati Kuu, Salim Ahmed Salim.

FAINI ZILIVYOSAIDIA KUPUNGUZA MAKOSA YA UKATILI WA JINSIA MASOKONI

Image may be NSFW.
Clik here to view.
FAINI zinazotolewa kwa watu wanaobainika na makosa ya unyanyasaji wa kijinsia katika soko la Gezaulole lililopo Kiwalani Bomubomu Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam zimesaidia kupunguza vitendo hivyo kwenye soko hilo

Hayo yamebainishwa Dar es Salaam leo asubuhi na Mwezeshaji wa Sheria katika soko hilo, Khadija Mohamed wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari waliotembea soko hilo kujua ni kwa kiwango gani vitendo hivyo vimepungua katika soko hilo baada ya Shirika la Equality for Growth (EfG) kutoa elimu ya kupinga unyanyasaji katika masoko ya Manispaa ya Ilala
"Faini tunazo watoza wafanyabiashara wanaobainika na makosa ya kutumia lugha chafu, kupigana na kuwadhalilisha wenzao kwa kuwakamata  maunguni na unyanyasaji mwingine zimesaidia kupunguza makosa hayo katika soko letu" alisema Mohamed.

Alisema mara zote matusi katika masoko yamekuwa yakichangia kuwakimbiza wateja na ndio maana wana lishukuru shirika la EFG kwa kuwapa elimu iliyowasaidia na kuwafanya waendelee na biashara zao kama kawaida
Mwezeshaji wa Sheria Amina Mussa alisema hapo awali wanaume walikuwa wamekubuhu kwa kutukana tusi la mama jambo ambalo lilikuwa linawakera lakini hivi sasa wanashukuru mungu baada ya wanaume hao kujitambua na kuacha matusi hayo

Mwenyekiti wa soko hilo, Muhidin Waziri alilipongeza shirika hilo kwa kuwasaidia wafanyabiashara katika masoko mbalimbali ya Manispaa ya Ilala na kujitambua hivyo kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia masokoni.

Katibu wa soko hilo, Salum Yusuf(PICHANI JUU) alisema changamoto kubwa waliyokuwa nayo hapo awali kabla ya kufikiwa na EfG ilikuwa ni kutojua maana ya unyanyasaji ambapo mtu aliyekuwa akishikwa mwilini au kutukanwa alikuwa hachukui hatua yoyote

Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Shirika hilo, Samora Julius alitoa ushauri kwa Serikali hasa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali katika masuala mbalimbali yakiwemo ya ukatili wa jinsia

Julius aliomba serikali kuyaunga mkono mashirika yanayofanya vizuri kwa kuyapa ruzuku itakayosaidia kuwafikia wananchi kwa wingi na jamii kwa ujumla.


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Ofisa Ufuatiliaji na Tathmini wa Shirika hilo, Samora Julius akitoa ushauri kwa Serikali hasa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kushirikiana na Mashirika yasiyo ya kiserikali katika masuala mbalimbali yakiwemo ya ukatili wa jinsia. Kushoto ni mtaalamu wa kujitolea wa masuala ya kijinsia kutoka nje ya nchi,

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Mwezeshaji wa Sheria, Khadija Mohamed (kulia), akielezea mafanikio waliyoyafikia ya kukabiliana na vitendo hivyo katika soko hilo baada ya kuwezeshwa na EfG.

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Mfanyabiashara wa samaki katika soko hilo, Asha Mohamed akihojiwa na wanahabari kuhusu namna wanavyo pambana na ukatili katika soko lao hilo la Gezaulole.



NAIBU KATIBU MKUU MPYA WIZARA YA MAMBO YA NDANI AANZA KAZI RASMI


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aliyeteuliwa hivi karibuni, John Mngodo, akijitambulisha kwa Watumishi mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Lilian Mapfa na kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE.


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba akijitambulisha mbele ya Naibu Katibu Mkuu mpya, John Mngodo (hayupo pichani) wakati wa Mkutano kati ya Watumishi na Naibu Katibu Mkuu huyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara.

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, akizungumza na Watumishi mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu mpya wa Wizara (hayupo pichani) alipofanya mkutano na watumishi hao mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.

HAFLA YA KUSHEREHEKEA KUAPISHWA KWA RAIS WA 5 WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


Image may be NSFW.
Clik here to view.

Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipongezwa na mmiliki wa blog ya Imma Matukio ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Gazeti Huru la Kila Siku la Majira, katika hafla iliyofanyika katika viwanja via Ikulu jijini Dar es Salaam jana.

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwasili kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Alhamisi usiku kwa ajili ya mchapalo maalum ulioandaliwa na Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli kusherehekea kupishwa kwake

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Sheim

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan kifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Hadija Mwinyi akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Sitti Mwinyi akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Salma Kikwete akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Asha Suleiman Iddi akifuatiwa na mkewe Mama Janet Magufuli

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli na viongozi wengine wakiwa hema kuu

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Mama Janet Magufuli akisalimiana na Mhe Makongoro Nyerere

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mhe Makongoro Nyerere

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Makongoro Nyerere

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akienda kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Mtera Mteule Mhe Livingstone Lusinde

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.







Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Mama Janet Magufuli akiwa na wageni wao

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.







Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na kutaniana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana kutniana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mhe Augostino Lyatonga Mrema wakati akiendelea kusalimiana na wageni wake




Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake. Hapa akiongea na Mbunge wa Morogoro vijijini mteule Mhe Propser Mbena

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake.

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake. Hapa akiteta jambo na kijana George Mathias Mgina

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais Dkt Magufuli akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Mizengo Pinda na Mzee Joseph Butiku

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Mama Janet Magufuli akiamkia na na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Mizengo pinda wakiwa Rais Dkt Magufuli na Mzee Joseph Butiku

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janet Magufuli wakiwa na kijana George Mathias Mgina

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Tunu Pinda akiwa na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Mizengo pinda na wanafamilia

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa na wake wa viongozi na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe Mizengo Pinda

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Mama Janet Magufuli akisalimiana na Mama Hasina Kawawa

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mhe Ole Sendeka

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Balozi wa Tanzania nchiniNigeria Mhe Njoolay akiwa na Mhe Chiligati na Mhe Profesa Jumanne Maghembe

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Wadau wakifurahia mchapalo

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Wadau wakiwa katika mchapalo huo

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe Saidi Mwambungu na Mbunge Mteule wa Nyasa

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Blogger maarufu Haki Ngowi (kushoto) na nduguye ambaye ni mbunifu wa mavazi wa mkimataifa Sheria Ngowi ndani ya nyumnba

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake. Hapa ni rafiki yake na Waziri Mkuu wa Zamani wa Kenya Mhe Raia Odinga na ujumbe wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiendelea kusalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Mama Salma Kikwete na familia ya Rais Mstaafu

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimianana na Mufti Mkuu wa Tanzania

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipozi na viongozi wa BAKWATA

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimaiana na viongozi wa dini

Image may be NSFW.
Clik here to view.







Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na msanii Mrisho Mpoto

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.







Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.







Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na wageni wake

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Yamoto Band ikitumbuiza. Picha zote na IKULU

HAKIKISHA HUPITWI NA KIPINDI KIPYA CHA DANGA CHEE

WASHIRIKI 20 BONGO STYLE WAENDELEA KUJIFUA





Image may be NSFW.
Clik here to view.

 Ikiwa ni siku ya tano tangu Washiriki 20 wa Shindano la Bongo Style linalo andaliwa na asasi isiyo ya Kiserikali ya Faru Arts and Sport Development Organization (FASDO), ikiwahusisha Wapiga picha na wabunifu wa mavazi wenye umri kati 19-25 walioingia rasmi kambini Novemba 5 mwaka huu,ambapo washiriki hao wameendelea kujifua zaidi huku wakipewa kazi mbalimbali za ubunifu na masomo mengine ikiwa ni sehemu ya shindano hilo.


Wakiwa kambini washiriki hao wamepata nafasi ya kujifunza mambo mapya ambayo walikuwa hawayafahamu. Fainali hizi zinatarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu ndani ya ukumbi waAlliance Francaise Jijini Dar es Salaam.

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti washiriki wa upande wa picha wamekili kuwa walikuwa wanaona kama wanafahamu vema kupiga picha lakini baada ya kupata somo wamegundua kuwa kuna mambo mengi ambayo walikuwa hawayafahamu na menginewalikuwa wanayafanya lakini bila kujua kuwa walikuwa sahihi.

Pia waliongeza kuwa wanashukuru kuwapata wataalam ambao wameweza kuwaonesha ni jinsi gani wanatakiwa kuwa wapiga picha wazuri.

Nao washiriki wa ubunifu wa mavazi wameshukuru kupata wataalam ambao wamekuwa wakiwapa maelekezo mengi ambayo  yalikuwa ni chachu kwao kwasababu kila mmoja kwa upande wake wamejifunza mambo mapya mengi na kuona kuwa kumbe sio lazima kuwa na ubunifu wa aina moja ya mavazi lakini wanaweza wakawa na aina nyengine nyingi kulingana na mazingira waliyopo na kuishukuru Fasdo kwa kuwakutanisha.

 Mwalimu na mtaalam wa kupiga picha  Sameer Kermalli amekili kuwa tangu darasa lianze washiriki hao wamekuwa na uelewa wa haraka na yeye kupata nafasi ya kuwaelekeza mbinu mbalimbali za kupiga picha na kanuni mbambali za upigaji picha, washiriki hao wamekuwa wasikivu na wameongeza ubunifu zaidi jambo ambalo limemtia moyo mtaalam huyo.

Kwa upande wa Mbunifu wa mavazi Martin kadinda(pichani juu) alisema kuwa washiriki wapo vizuri na kila mbunifu anakitu chake cha kipekee ambacho yeye anafanya mfano wapo wale ambao wanabuni nguo zao kwa kutumia kitenge tu, wengine wanatumia vitu vya asili, nguo za kisasa, nguo ambazo zipo tayari kwa ajili ya kuvaliwa na zenginezo, aliwashauri kuwa wasiegemee katika kitu kimoja tuu au aina moja ya mavazi lakini wawe na ubunifu na kubadilika kila wakati kwa sababu mitindo inakwenda ikibadirika.

Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande alipata nafasi ya kutembelea kambini na kujionea jinsi washiriki wanavyojituma katika kazi zao na maandalizi ya shindano hilo yanavyo kwenda.

" Ninachukua nafasi hii kwa niaba ya Fasdo kuwapongeza washiriki wote mliofanikiwa kuingia katika shindano hili la Bongo style lengo likiwa ni kuwajengea uwezo zaidi wa kile ambacho mlikuwa nafanya ipate kuwa zaidi aliongeza kuwa kuna ushindani mkubwa na shindano linafuata vigezo vyote vya ushindani na washindi watakuwa wamekidhi vigezo hivyo”anasema.
 Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande akiwa na washiriki wa shindano la Bongo Style ambao hawapo pichani , akiwa na Mratibu wa FASDO Tanzania Joyce Msigwa alipofika kuwatembelea na kuongea nao machache.


 Baadhi ya  Washiriki kwa upande wa Ubunifu wa mavazi wakiwa wanachakalika kuandaa kazi zao mbalimbali
 washiriki  wa ubunifu wa mavazi wakiendelea na kazi
  Tunukiwa Daudi (Aliyesimama) akitoa somo juu ya matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii na Faida zake.
 Baadhi ya washiriki upande wa kupiga picha wakifurahia jambo.
 Muwezeshaji kutoka Wiki Loves Africa akitoa somo juu ya upigaji picha kwa washiriki ambao hawapo pichani.
Hawa ni washiriki kwa upande wa kupiga picha wakikamilisha moja ya mazoezi waliyopewa(Picha kwa hisani ya Washiriki upande wa wapiga picha).

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AKABIDHIWA RASMI OFISI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amekabidhiwa rasmi ofisi na Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohammed Gharib Bilal Ikulu, Jijini Dar es salaam.
 Baada ya makabidhiano hayo Mhe. Samia, alikaribishwa na watumishi wa ofisi yake ambapo alitumia fursa hiyo kuwataka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii kulingana na kauli mbiu ya 'Hapa ni Kazi tu'.
"Kila mmoja afanye kazi kwa bidii mahala pake pa kazi. Wale ambao kauli mbiu ya Hapa ni Kazi tu, itawapita wakae pembeni... watatusamehe", alisema Makamu wa Rais.
Aidha Mhe. Samia alisisitiza suala la kuendelea kupendana na kushirikiana miongoni mwa watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais ili kufanikisha azma ya kuleta matarajio ya maendeleo ya Watanzania wanayotaka kuyaona katika uongozi wa awamu ya tano.
Baada ya kutoa nasaha hizo alifanya kikao na Menenjimenti ya ofisi ambapo alitoa uelekeo wa utendaji kazi katika ofisi hiyo hususan kuzingatia kusimamia masuala ya muungano na mazingira ili kufanikisha malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Aliitaka Menejimenti hiyo kujipanga upya na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa ajili ya kuleta mabadiliko kwa upande wa masuala ya muungano na mazingira.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akisaini Kitabu cha wageni wakati alipoingia Ofisini kwake kwa mara ya kwanza baada ya kukabidhiwa Ofisi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo Nov 9, 2015
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia kwake), Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Sazi Salula na Naibu Katibu Mkuu wake, ....baada ya makabidhiano ya Ofisi yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam,leo

 Mmoja wa wafanyakazi akimtunuku shada la maua baada ya kukabidhiwa ofisi hiyo na Makamu mstaafu Dkt.Gharib Bilali.
 Hapa akipeana mikono na baadhi ya wafanyakazi wa ofisi hiyo mara baada ya kukabidhiwa rasmi.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakati alipowasili kwenye Ofisi hiyo leo Nov 9, 2015 baada ya makabidhiano. Akizungumza na wafanyakazi hao Mama Samia, aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa mashirikiano na kwa bidii ili kutimiza Kaulimbiu ya Mhe.Rais ya 'HAPA KAZI TU'.
 Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakiwa wamejipanga mstari wakisubiri kumpokea Bosi wao Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akiwasili leo kwa mara ya kwanza baada ya makabidhiano rasmi ya Ofisi na Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Bilal.


 








MERU LOGISTICS WASAFIRISHAJI MIZIGO KUTOKA ULAYA KUJA TANZANIA


Karibu Meru Logistics kwa huduma nzuri, safi, zenye uhakika na haraka kutuma mizigo kutoka UK kwenda Tanzania.

Wasiliana nasi pia kama unahitaji chochote kutoka UK kama vile magari, matractor, fridge, TV, Vyombo nk. tuta kusaidia kununua na kukutumia mpaka Tanzania bila tatizo lolote na vitafika salama kabisa.

Bei za kutuma mizigo ni kama ifuatavyo:

20' CONTAINER TO DAR /MOMBASA FROM £1,300 

40' CONTAINER TO DAR /MOMBASA FROM £1,800

4X4 TO DAR/MOMBASA FROM £850

SALOON CARS TO DAR/ MOMBASA FROM £750

AIR CARGO TO DAR £5 A KILO

AIR CARGO TO ZNZ £4 A KILO 

INCLUSIVE CLEARANCE

TO COLLECT CARGO LONDON FROM £25 

TO COLLECT CARGO OUTSIDE LONDON FROM £50

ONCE YOU PAY HERE IN UK YOU DONT PAY ANYTHING IN TANZANIA

(UKIISHA LIPA UK UNAKWENDA TU KUCHUKUA MZIGO WAKO)

Address in UK: Unit 12 Manor Way Business Centre

Marsh Way, Rainham, Essex

RM13 8UG

COLLECTION POINT IN DAR IS:

DAR FREE MARKET, ALI HASSAN MWINYI ROAD

OYSTER BAY NEAR KENYAN EMBASSY & DSTV

Telephone: +44 (0) 1708554632

Email: info@merulogistics.com


Instagram: @merulogistics 

Facebook: Meru Logistics

CUSTOMER SATISFACTION GURANTEED!!!

JESHI LA POILISI LAJIPANGA KUKABILIANA NA AJALI ZA MWISHO WA MWAKA


Image may be NSFW.
Clik here to view.


Mkuu wa Kitengo cha Elimu kwa Umma, Makao Makuu ya Trafiki, Dar es Salaam, ASP Abel Swai akitoa elimu ya usalama barabarani kwa abiria, muda mfupi kabla ya kuanza safari za mikoani katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo, jijini Dar es Salaam, elimu ambayo inalenga kudhibiti ajali za barabarani kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, PC Asha Adam, akiwasisitiza abiria kufunga mikanda iliyopo kwenye viti walivyoketi muda wote wa safari muda mfupi kabla ya magari kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi ya abiria Ubungo, jijini Dar es Salaam, kama hatua ya kudhibiti majeraha na vifo vitokanavyo na ajali za barabarani, kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka,

Image may be NSFW.
Clik here to view.


skari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Inspekta Ibrahim Omary Samwi(kushoto), na PC Elisante Bura(kulia), wakikagua moja ya magari yanayofanya safari zake mikoani, kutekeleza mkakati wa Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.Zoezi hili limefanyika muda mfupi kabla ya magari kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam kuelekea mikoa mbalimbali ya Tanzania .

Image may be NSFW.
Clik here to view.



Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Sajenti Jackson Mafuru (kulia), na PC Elisante Bura(kushoto), wakikagua moja ya magari yanayofanya safari zake mikoani. zoezi hili ambalo limefanyika muda mfupi kabla ya magari kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam, ni moja ya hatua ya Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.

Image may be NSFW.
Clik here to view.


Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Koplo Abdallah Bwasi akikagua moja ya magari yanayofanya safari zake nje ya mkoa wa Dar es Salaam, muda mfupi kabla ya magari kuondoka katika kituo Kikuu cha mabasi Ubungo,jijini Dar es Salaam.Hatua hii ya Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani imekuja kwa lengo la kudhibiti ajali kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka.(Picha zote na Abubakari Akida, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

WALIMU WAIDAI SERIKALI SH.BILIONI 1.1

Walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam wanaidai Serikali jumla ya sh. Bilioni 1.1 za madai yao mbalimbali kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Dar es Salaam, Mwalimu Amina Kisenge (pichani kushoto), katika kikao cha baraza la dharura la chama hicho lililoketi hivi karibuni.

"Awali CWT ilikua ikidai jumla ya Sh.Bilioni 3.9 kabla ya kupunguza kiasi cha Sh.Bilioni 1.9 mapema mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti, madeni hayo ni pamoja na malimbikizo ya nauli za likizo kuanzia mwezi Juni na Desemba, 2013 lakini pia Juni na Desemba mwaka jana.

Malimbikizo mengine ni pamoja na pesa ya kuwasafirisha wastaafu kwenda majumbani kwao," alisema Kisenge na kuongeza

"Uhamisho wa walimu kutoa kituo kimoja kwenda kingine ikiwa ni posho ya usumbufu na ya kujikimu pamoja na pesa za gharama za masomo baada ya walimu kujigharamia kujisomesha, imekuwa pia ni tatizo kwa serikali kutoa," alisema .


Aliongeza kwamba changamoto nyingine inayowakabili walimu ni mfuko wa PSPF kutowalipa walimu wastaafu kwa wakati ambapo walimu waliostaafu Januari hadi Septemba mwaka huu hawajalipwa mafao yao.
Alibainisha kuwa kero nyingine ni walimu kutopandishwa madaraja kwa wakati na kwa wale wanaobahatika kupanda madaraja, mishahara yao hairekebishwi.
Wakati huohuo, CWT iliitaka serikali ya awamu ya tano kuharakisha matumizi ya chombo cha ajira kwa walimu kilichopitishwa na serikali ya awamu ya nne kwamba chombo hicho ndicho mkombozi wao.









UZINDUZI WA USHIRIKA WA MAMA NA BABA LISHE KUFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Image may be NSFW.
Clik here to view.
Mratibu na Msimamizi Mkuu wa Jumuiya Ya Mama na Baba Lishe Mkoa wa Dar es Salaam, Said Said (wa pili toka kulia), akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idata Maleleo kuelezea kuhusu Uzinduzi wa Ushirika wa Mama na Baba Lishe unaotarajia kufanyika Novemba 15, 2015 ukumbi wa SabaSaba jijini Dar es Salaam. Lengo la jumuiya hiyo kuunganisha kwa pamoja wadau mbalimbali, kutoa fursa kulinda haki za ajira na kuzitafutia ufumbuzi na kuondoa tatizo la ajira kupitia tasnia hii ikiwa ni kumtambua mama na baba lishe kama sehemu ya maisha ya kila mmoja wetu, kwani kila mtanzania anaufahamu umuhimu wa mama na baba lishe na takwimu zinaonyesha asilimia 50% ya wanzania waishio mijini hupata huduma ya chakula. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.

Image may be NSFW.
Clik here to view.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mama na Baba Lishe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Mhonzu akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idata Maleleo kuelezea kuhusu Uzinduzi wa Ushirika wa Mama na Baba Lishe unaotarajia kufanyika Novemba 15, 2015 ukumbi wa SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Mama Lishe wakiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa idata Maleleo kuelezea kuhusu Uzinduzi wa Ushirika wa Mama na Baba Lishe unaotarajia kufanyika Novemba 15, 2015 ukumbi wa SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live