Quantcast
Channel: Matukio
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live

MGODI WA DHAHABU WA BULYANHULU WAKABIDHI MADAWATI KWA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA

$
0
0
  Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ,Bi Zainab Telack (aliye vaa ushungi) akiongozwa na Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu Elias Kasitila (kushoto kwake) wakati wakielekea uwanja wa Taifa wa mjini Kahama kwa ajili ya makabidhiano ya Madawati kutoka kampuni ya Acacia.Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack akihutubia wananchi katika uwanja wa Taifa Kahama wakati wa zoezi la Kukabidhiwa madawati kutoka kwa kampuni ya Mgodi wa Dhahabu wa Acacia, Bulyanhulu.
Wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,kutoka kushoto ni Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii katika Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Elias Kasitila, Afisa Miradi Mzee Hamisi, Afisa Mahusiano ya Jamii William Bundala Chungu pamoja na Afisa Mahusiano ya Jamii David Magege, wakiwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama kabla ya zoezi la Kukabidhi Madawati .
Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Shinyanga wakichukua taarifa kwa ajili ya kuuabarisha umma juu ya tukio la makabidhiano ya Madawati.

Madawati yaliyotolewa na kampuni ya Acacia kwa ajili ya shule katika mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi,Zainab Telack akikata utepe kuashiria kupokea madawati yaliyotolewa na kampuni ya Acacia.



Na Dixon Busagaga,Shinyanga.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack amekabidhiwa madawati 2,000 yenye thamani ya Shilingi 240,800,000/= na Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu uliopo katika Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama, Mkoa wa Shinyanga. Makabidhiano yamefanyika leo mjini Kahama.

Akimkabidhi madawati hayo Meneja wa Ufanisi wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Bwana Elias Kasitila amesema, “hii ni awamu ya nne kwa mgodi wa Acacia Bulyanhulu kukabidhi madawati ndani ya mwaka huu katika kipindi ambacho taifa linaendelea kutekeleza kampeni ya kitaifa ya dawati kwa kila mwanafunzi iliyoagizwa na Mheshiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa lengo la kuboresha mazingira ya elimu nchini Tanzania.”

Ameongeza kuwa, “licha ya Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu kuchangia madawati pia inachangia miradi mingine kwenye jamii lakini kwenye sekta ya elimu mgodi unashirikiana na jamii kuitekeleza miradi kama vile ujenzi na ukarabati wa nyumba, ofisi za walimu madarasa, maabara za sayansi na udhamini wa masomo kwa wanafunzi.”

Miradi ya Madawati 2016 kutoka Mgodi wa Acacia Bulyanhulu

Mei tulikabidhi madawati 380 kwa Halmashauri ya Msalala yenye thamani ya shilingi 28,500,000/=
Juni tulikabidhi madawati 1,000 kwa Halmshauri ya Msalala yenye thamani ya shilingi 88,500,000/=
Julai tulikabidhi madawati 500 kwa Wilaya ya Nyang’wale Mkoani Geita yenye thamani ya shilingi 37,500,000/=
Na hii leo Agosti tunakabidhi madawati 2,000 kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga yenye thamani ya shilingi 240,800,000 /=
Aidha mwaka 2013 mgodi wa Acacia Bulyanhulu pia ulikabidhi dawati 1,389 kwa Wilaya ya Kahama

Mchango wa Miradi ya Madawati Kwenye Ajira Katika kipindi cha miezi minne, utengenezaji wa madawati yenye thamani ya shilingi 393,800,000 umewezesha kutolewa kwa tenda za kutengeneza madawati kwa vikundi vya wajasiliamali wadogo na kuwawezesha vijana kujipatia ajira.

Wanafunzi ambao Wamenufaika Mradi wa Madawati wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu umewaondelea adha jumla ya wanafunzi 5,040 ya kuketi sakafuni wakati wa kupokea masomo yao, baada ya kupata madawati 3,880 bora ya kudumu ambayo yametengenezwa kwa awamu nne hadi sasa.

Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu na Sekta ya Elimu Nchini

Mgodi wa Bulyanhulu unaamini kwamba elimu ni msingi wa maendeleo ya jamii na unaendelea kushirikiana na serikali na wadau wengine wa maendeleo katika ngazi mbalimbali kuendeleza shughuli za uboreshaji wa elimu hapa nchini kupitia miradi mbalimbali inayofadhiliwa na mgodi kupitia Mfuko wa Maendeleo wa Kampuni ya ACACIA, (ACACIA Maendeleo Fund).

Mkuu wa Mkoa Shinyanga Bi Zainab Telack amesema, “ Tukio hili la kukabidhiwa madawati ni tukio kubwa, nimefurahi sana na ninajua furaha ya watoto watakaotumia madawati haya itakuwa mara mbili yake, kwa hivyo kwa niaba ya Mkoa wa Shinyanga nawashukuru sana Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu kwa kututengenezea madawati elfu mbili, mkoa wa Shinyanga ulikuwa na upungufu wa Dawati elfu 7000 lakini sasa kupitia mchango wa leo kutoka Bulyanhulu na wadau wengine sasa mkoa wetu unamaliza kabisa upungufu wa madawati.”

MKURUGENZI ILEJE ATOA ONYO KALI KWA WASIMAMIZI WA MITIHANI YA DARASA LA 7

$
0
0
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi akiandika baadhi ya hoja kutoka kwa baadhi ya wasimamizi wa mitihani ya darasa la saba inayotarajiwa kufanyika siku ya jumatano tarehe 07 /09 /2016 na alhamisi tarehe 08 /09 /2016.


baadhi ya wasimamizi wa mitihani ya darasa la saba wakimsikiliza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi.


Na fredy mgunda,ileje

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ileje Haji Mnasi, amewaasa wasimamizi wa mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kutofanya kazi kwa mazoea ili kutoruhusu mianya itakayowafanya wanafunzi wasiokuwa na uelewa kufaulu mitihani hiyo.

Alisema kumekuwa na baadhi ya wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika wanafaulu mithani hiyo kitendo kinachotia mashaka kwa wasimamizi hao kushindwa kunyakazi waliyopewa kwa makini.

Mnasi aliyasema hayo jana, wakati akitoa semina ya mafunzo kwa wasimamizi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje ambapo alisema usimamizi hafifu wa mitihani umesababisha kuwepo kwa watumishi wasiokuwa na uwezo kitaaluma.

Aidha kabla ya uteuzi wa Rais wa jamhuri ya muungazo wa tanzania Dr John Pombe Magufuli mkurugenzi huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu alikuwa afisa elimu shule ya msingi manispaa ya iringa alisema iwapo ikibainika kufaulu kwa wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika mtuhumiwa wa kwanza kwenye uzembe huo atakuwa msimamizi wa mitihani na hatua kali zitachukuliwa zidi yake.

“Nawatahadharisha kwamba mnaweza mkarubuniwa kuwawezesha wanafunzi wasiokuwa na sifa wafaulu mitihani hiyo,kufanya hivyo ni kukiuka kanuni za usimamizi na uendeshaji wa mtihani na kuwaambia hayupo tayari kutumbuliwa na rais kwasababu za wasimamizi”alisisitiza Mnasi.

Hata hivyo Mnasi aliwataka wasimamizi hao kuwa makini katika kufanyakazi hiyo na kama kuna jambo lolote ambalo hawajalielewa kuhusu kazi hiyo ni vyema wakauliza ili kupewa majibu.

“hakikisheni kuwa taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo na kuwataka wasimamizi wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu.“Nawaasa wasimamizi wa mitihani kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani serikali itachukua hatua kali kwa yeyote atakayebainika kukiuka taratibu za mitihani,” alisema Mnasi.

Mnasi alibainisha kuwa, serikali imezingatia uwezo wa kitaaluma, uadilifu na uaminifu hivyo wasimamizi hao kupewa jukumu la kusimamia mitihani hiyo muhimu ya kitaifa. Aliongeza kuwa mitihani hiyo ni muhimu ili kuliwezesha taifa kupima kiwango cha elimu kilichpo nchini na kuwapata wasomi wa kiwango cha juu.

Nao wasimamizi wa mitihani hiyo wamemuahidi mkurugenzi huyo kuwa watasimamia mitihani hiyo kwa kufuata sheria na kanuni za usimamizi wa mitihani walizopewa. Lakini mitihani hiyo ya kuhitimu darasa la saba inatarajiwa kufanyika siku ya jumatano tarehe 07 /09 /2016 na alhamisi tarehe 08 /09 /2016.

UZINDUZI WA KONDOM MPYA YA ZANA WAFANYIKA MKOANI MWANZA

$
0
0
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (kushoto) akizindua Kondom mpya ya Zana inayotolewa na Serikali bure kwa wananchi kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi.

Kondom ya Zana ni mbadala wa kondom iliyokuwa ikitolewa pia bure na serikali na kusambazwa na Bohari ya Dawa nchini MSD ambapo kondom hiyo haikuwa na jina, rangi na kifungashio chenye kuvutia hali ambayo ilisababisha wananchi kudhania kwamba haina ubora jambo ambalo hata hivyo halikuwa sahihi kwani ilikuwa na ubora kama aina nyingine za kondom.

Na BMG
Uzinduzi wa Zana Kondom mkoani Mwanza
Zana kondom kwenye ubora wake
Wadau wakiwa kenye picha ya pamoja na mgeni rsami, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (mwenye suti).
Wanahabari wakiwa kenye picha ya pamoja na mgeni rsami, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (mwenye suti).
Waelimisha rika wakiwa kenye picha ya pamoja na mgeni rsami, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (mwenye suti).
Viongozi mbalimbali Wadau wakiwa kenye picha ya pamoja na mgeni rsami, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (mwenye suti).
Viongozi mbalimbali wakiwa kenye picha ya pamoja na mgeni rsami, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi (mwenye suti).
Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, amesema kumekuwa na dhana potofu kwa wananchi kuhusu kondom zinazotolewa bure na serikali kwamba hazina ubora jambo ambalo siyo sahihi ambapo amewahahikikishia kwamba kondom ya Zana ina ubora wa hali ya juu hivyo ni vyema wakazingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom hiyo ili kuondokana na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi, amebainisha kwamba serikali imekuwa ikitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwahudumia wanaoishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hivyo ni vyema wakazingatia matumizi ya kondom ili kujikinga na maambukizi hayo.
Dr.Pius Masele ambaye ni Mratibu wa Ukimwi mkoa wa Mwanza, akizungumza na wanahabari ambapo amesema hali ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi ni asilimia 4.2 na kwamba serikali inaendelea kuhakikisha kwamba inatomeza mambukizi hayo pamoja na magonjwa mengine ya ngono kwa kuhamasisha wananchi kuzingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom
Kutoka kushoto ni Dr.Pius Masele, Mratibu wa Ukimwi mkoani Mwanza, Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dr.Leonard Subi, Mratibu wa TACAIDS mkoani Mwanza, na Mratibu PSI mkoani Mwanza, Clement Mbogo.
Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Dr.Pius Masele, Mratibu wa Ukimwi mkoani Mwanza, akizungumza kwenye uzinduzi huo
Mratibu PSI mkoani Mwanza, Clement Mbogo, akizungumza kwenye uzinduzi huo wa Zana Kondom mkoani Mwanza
Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dr.Leonard Subi, akizungumza kwenye uzinduzi wa Zana kondom mkoani Mwanza
Taswira Ukumbini
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa kondom ya Zana mkoani Mwanza
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa kondom ya Zana mkoani Mwanza


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dr.Leonard Subi, amebainisha kwamba serikali imekuwa ikitumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kuwahudumia wanaoishi na maambukizi ya virusi vya Ukimwi hivyo ni vyema wakazingatia matumizi ya kondom ili kujikinga na maambukizi hayo.

Amesema ili kuondokana na matumizi hayo ya fedha, Serikali inawahimiza wananchi kuzingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom, ili kuondokana na maambukizi ya virusi hivyo pamoja na maambukizi mengine ya magonjwa zinaa ikiwemo kaswende.

Dr.Subi ameyasema hayo hii leo kwenye uzinduzi wa kondom mpya ya Zana uliofanyika mkoani Mwanza, ambayo itakuwa ikisambazwa bure kwa wananchi na serikali ili kusaidia wananchi kuondokana na magonjwa ya zinaa pamoja na kimba zisizotarajiwa.

Amesema ni vyema wananchi wakaendelea kuhimizwa kuwa na matumizi sahihi na endelevu ya kondom ya Zana, hatua itakayosaidia kupunga ongezeko la waathirika wa magonjwa ya zinaa ikiwemo virusi vya Ukimwi na hivyo kuipunguzia serikali matumizi makubwa ya fedha kwa ajili ya kuwahudumia wenye maambukizi hayo.

Naye Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, amesema kumekuwa na dhana potofu kwa wananchi kuhusu kondom zinazotolewa bure na serikali kwamba hazina ubora jambo ambalo siyo sahihi ambapo amewahahikikishia kwamba kondom ya Zana ina ubora wa hali ya juu hivyo ni vyema wakazingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondom hiyo ili kuondokana na magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa.

Uzinduzi wa kondom mpya ya Zana inayotolewa bure na serikali kwa wananchi, ulifanyika Kitaifa Agosti 30,2016 mkoani Mbeya ambapo kwa mkoa wa Mwanza umefanyika hii leo Jijini Mwanza ambapo wahamasishaji rika watakuwa wakipita mitaani kuwahamasisha wananchi juu ya matumizi sahihi ya kondom hiyo na baadae uzinduzi kama huo utaendelea katika mikoa mingine nchini lengo likiwa ni kuwahamasisha wananchi kutumia kondom hiyo ili kusaidia mapambano dhidi ya magonjwa ya zinaa ikiwemo virusi vya Ukimwi na mimba zisizotarajiwa.

Bonyeza HAPA Kutazama picha za Kikao Elekezi

MUWSA YAKABIDHI MADAWATI KWA SHULE YA MSINGI MANDELA MJINI MOSHI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.Said Mecky Saidiq akiwasili katika shule ya msingi Mandela iliyopo kata ya Bomabuzi wilaya ya Moshi kwa ajili ya kupokea msaada wa Madawati yaliyotolewa na Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA).
Wanafunzi katika shule ya Msingi Mandela wakiimba nyimbo wakati wakipokea wageni waliofika katika tukio la kukabidhi madawati.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA) Joyce Msiru akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq alipowasili katika shule ya msingi Mandela kwa ajili ya kukabidhiwa Madawati.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akiwa na Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba (kushoto) pamoja na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi,Raymond Mboya (kulia) wakati wa makabidhiano ya Madawati kwa ajili ya shule ya msingi Mandela.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) ,Joyce Msiru akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi madawati kwa ajili ya shule ya msing Mandela.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiq Madawati kwa ajili ya shule ya Msingi Mandela iliyopo Manispaa ya Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiq (katikati) akiwa ameketi kwenye Dawati na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru pamoja na mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi Mandela.
Wanafunzi katika shule ya Msingi Mandea wakiwa wameketi katika madawti yaliyotolewa na Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Moshi(MUWSA).

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akikabidhi madawati kwa mkuu wa shule ya msingi Mandela ,Pegi Michael.




Na Dixo Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

RAIS MUSEVENI AWASILI DAR ES SALAAM JIONI HII TAYARI KWA MKUTANO WA VIONGOZI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0

Mwenyekiti wa Jumuya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akitambulisha wasaidizi wake kwa Rais wa Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni mgeni wake huyo alipowasili Ikulu Dar es salaam leo jioni ya Septemba 7, 2016 tayari kwa mkutano wa Viongozi wa jumuiya hiyo utaofanyika ukumbi wa mikutano wa Ikulu


Mwenyekiti wa Jumuya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni wakiingia ndani na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika mashariki, Kikanda na Kimataifa Dkt Augustine Mahiga (kushoto) mara mgeni huyo alipowasili Ikulu Dar es salaam leo Septemba 7, 2016 tayari kwa mkutano wa Viongozi wa jumuiya hiyo hapo kesho katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu


Mwenyekiti wa Jumuya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono Rais wa Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni mgeni wake huyo alipowasili Ikulu Dar es salaam jioni ya leo Septemba 7, 2016 tayari kwa mkutano wa Viongozi wa jumuiya hiyo hapo kesho katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu


Mwenyekiti wa Jumuya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni wakiwa na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika mashariki, Kikanda na Kimataifa Dkt Augustine Mahiga (kuia) na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Plilip Mpango (kushoto) mara mgeni huyo alipowasili Ikulu Dar es salaam leo Septemba 7, 2016 tayari kwa mkutano wa Viongozi wa jumuiya hiyo hapo kesho katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu


Mwenyekiti wa Jumuya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli katika mazungumzo na Rais wa Uganda Mhe Yoweri Kaguta Museveni mgeni wake huyo alipowasili Ikulu Dar es salaam leo Septemba 7, 2016 tayari kwa mkutano wa Viongozi wa jumuiya hiyo hapo kesho katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu.

RAJAB NA KITHARA TAARAB ZANZIBAR WALIVYOTUMBUIZA JIJINI WASHINGTON

$
0
0
Kundi zima la Rajab and Kithara Taarab lenye kupiga mziki wa mahadhi ya mwambao kutoka Zanzibar, walipotumbuiza siku ya Jumanne Sept 6. ndani ya ukumbi wa The John F. Kennedy Center for the Performing Arts Jijini Washington.  Rajab and Kithara watakua hapa Marekani mwezi mzima wakitumbuiza States mbali mbali hapa Marekani. kwa ratiba zao bofya hapa  centerstageus.org
Mmoja wa waimbaji wa kundi zima la Rajab and Kithara,  Saada Nassor, akitumbuiza wimbo wa Chungu,  ndani ya ukumbi wa The John F. Kennedy Center for the Performing Arts  iliopo Jijini Washington. (Picha zote na swahilivilla.blogspot.com)
 Picha  zaidi Bofya hapa
Saada Nassor, akionyesha pozi wakati anawatumbuzia Wamarekani.

Makame Faki  akitumbuiza wimbo wa "Salaam Aleikum" 
Makame Faki  akiimbaa wimbo wa "Salaam Aleikum"
Wataalamu wa upigaji wa vyombo vya mahadhi ya mwambao,  mpiga ngoma Foum Faki, (kushoto) akiwa na  mpiga bass kitaa,  Daudi Shahil, wakitumbuiza  wageni waalikwa 
Kundi zima la Rajab and Kithara Taarab,  Zanzibar walivyotumbuiza Jijini Washington 
 Mtaatam wa wa quanun Zanzibar ambae pia ni kiongozi wa kundi zima la  Rajab and Kithara, Rajab Suleiman akitambulisha kundi zima la Rajab and Kithara.  Picha  zaidi Bofya hapa

MWAKILISHI WA JIMBO LA TUNGUU AZINDUA BARAZA LA VIJANA WA SHEHIA TATU ZA UNGUJA UKUU

$
0
0
Shekh Mohammed Suleiman akisoma Quran kabla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana kwa Shehia Tatu za Unguja Ukuu Kaebona, Unguja Ukuu Kaepwani na Unguja Ukuu Tindini uliofanyika katika viwanja vya mpira Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akisalimiana na Sheikh Mohammed Suleiman baada ya kusoma quran wakati wa uzinduzi wa Baraza la Vijana Unguja Ukuu Zanzibar.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Kaepwani, Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini wakifuatilia Uzinduzi huo wa Mabaraza yao.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu wakisoma Utenzi wa Uzinduzi wa Mabaraza yao ya Vijana katika Jimbo la Tunguu Zanzibar.
Mhe Simai Mohammed Said, Mkuu wa Wilaya ya Kati Unguja Mhe Mashavu Sukwa wakisikiliza utenzi wakati wa uzinduzi huo.
Msanii wa Ngogoti Mussa akionesha umahiri wao wakati wa uzinduzi huo.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed SDaid akionesha dhana ya ushupavu na moyo wa ujasiri wa kucheza na chatu wakati wa Uzinduzi wa Mabaraza la Vijana wa Jimbo la Tunguu Shehia za Unguja Ukuu Kaepwani, Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini uliofanyika katika viwanja vya Idumu Unguka Ukuu leo jioni.
Vijana wa Jimbo la Tunguu wakimpiga picha Mwakilishi wao wakati akicheza na Chatu katika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana leo jioni katika viwanja vya Idumu Unguja Ukuu Zanzibar Wilaya ya Kati.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akimsalimia Msanii Mussa Nyoka baada ya kutowa burudani wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana la Jimbo hilo.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akiwa na simu wakati Mhe Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Anayeshughulikia Muungano Mhe. Januari Makamba akiongea na Wananchi akiwa Mjini Dodoma alikuwa ahudhuria uzinduzi huo wa Mabaraza la Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Zanzibar na kutoa ahadi ya kuchangia shilingi milioni tatu kwa Shehia hizo Tatu za Unguja Ukuu Kaepwani. Unguja Ukuu Kaebona na Unguja Ukuu Tindini.
Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu wakimsikiliza Mhe Januari Makamba akizungumza na Wananchi wa Shehia hizo kupitia simu ya mkononi akiwa Mjini Dodoma akihudhuria Kikao cha Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kiongozi wa Mabaraza ya Vijana wa Unguja Ukuu akisoma risala ya Vijana wa Mabaraza ya Unguja Ukuu wakati wa uzinduzi huo. uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akihutubia Vijana wa Shehia za Unguja Ukuu Zanzibar wakati wa Uzinduzi wa Mabaraza hayo uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja leo jioni.
Wazee wa Unguja Ukuu wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akizindua Mabaraza ya Vijana wa Jimbo lake uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya mpira vya Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu akihutubia wakati wa Uzinduzi huo wa Baraza la Vijana Unguja Ukuu Zanzibar.
Vijana wa Shehia za Ungujav Ukuu Wilaya ya Kati Unguja wakimsikiliza Mwakilishi wao Mhe. Simai Mohammed Said akiwahutubia.
Mkuu wa Wilaya ya Kati Unguja Mhe Mashavu Sukwa akizungumza wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Shehia za Unguja Ukuu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kati Unguja na Diwani wa Wadi ya Bungi Mhe Saidi Mtaji Askari, akizungumza wakati wa uzinduzi huo wa Baraza la Vijana wa Unguja Kuu Wilaya ya Kati Unguja.
Mwenyekiti wa Vijana wa UVCCM Wilaya ya Kati Unguja Ndg Khamis Hamza Chilo, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi huo wa Baraza la Vijana Shehia ya Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
Vijana wa Shehia ya Unguja Kuu wakimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Mhe Simai Mohammed Said akihutubia wakati uzinduzi huo.
Msanii wa Ngogoti akionesha umahiri wake wakati wa uzinduzi huo. akicheza na nyoka aina ya chatu
Wasanii wa Kikundi cha Sarakasi cha Bungi wakinesha umahiri wao.





Kikundi cha Wasanii wa Dance wa Bungi wakionesha umahiri wa kudance wakati wa hafla ya uzinduzi huo.

Sheikh Mohammed Suleiman akisoma dua baada ya kumalizika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo la Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar akizungumza nma Viongozi wa Mabaraza ya Vijana ya Shehia za Unguja Ukuu wakati wa kumalizika kwa hafla hiyo ya Uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya mpira vya Idumu Unguja Ukuu Wilaya ya Kati Unguja.
 Imetayarishwa na OthmanMapara.Blogspot.com
Zanzinews.com.

MAMLAKA YA MAJI TANGA YAPATA TUZO

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto akipokea tuzo ya mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) ya ubora wa kimataifa,kupitia hati ya ISO 9001:2015 ulitokana na ushindi wa kuwa mamlaka bora ya hduuma za Maji Safi na Usafi wa Mazingira nchini kwa Mwaka 2014/2015 wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo,Salum Shamte


Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo,Salum Shamte kulia akipokea tuzo hiyo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella walioipata mamlaka hiyo ushindi wa kuwa mamlaka bora ya huduma za maji na usafi wa mazingira nchini mwaka 2014/2015

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo,Salum Shamte kulia akimkabidhi tuzo hiyo Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katikati akiwa na kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi ambapo kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi Mpya wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Salum Shamte,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira,Mhandisi Joshua Mgeyekwa wa kwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Abdulla Lutavi na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi


Mkuu wa Tanga,Martine Shigella akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa bodi mpya ya mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) uliyoteuliwa na Waziri wa Maji


Mkuu wa Tanga,Martine Shigella akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa bodi mpya ya mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) uliyoteuliwa na Waziri wa Maji ikiwemo wafanyakazi wa Mamlaka hiyo


Mkuu wa Mkoa wa Tanga akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga ( Tanga Uwasa) na wafanyakazi wa mamlaka hiyo







MKUU wa Kitengo cha Uzalishaji Maji katika kituo cha Kusafishia Maji Mabayani Jijini Tanga,Faraji Nyoni akimueleza mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella namna uzalishaji wa maji uzalishaji unavyofanyika na usafishaji wake kabla ya kuwafikia wananchi.

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) imeweza kuwa mamlaka ya kwanza nchini kufikia vigezo vya kupewa leseni ya EWURA ya Daraja la kwanza (Class 1Lesence).

Leseni hiyo ilitolewa Juni 17 mwaka huu na Waziri wa Maji na Umwagiliaji katika mkutano wa kuzindua ripoti ya mwaka 2014/2015 ya mamlaka za maji uliofanyika Mjini Dodoma.

Akizungumza mwishoni mwa wiki,Mkurugenzi Mkuu wa EWURA ,Felix Ngamlagosi alisema kuwa leseni hiyo ilitolewa kwa Tanga Uwasa na kwa sasa ndio mamlaka ya maji pekee nchini iliyo na leseni ya EWURA ya daraja la kwanza nchini.

Alisema kuwa leseni hiyo ya daraja la kwanza imetolewa baada ya EWURA kupitia utendaji kazi wa Tanga Uwasa na kutadhimini viwango vilivyowekwa ili mamlaka ya maji kuweza kupata daraja la kwanza na kujiridhisha kuwa vimefikiwa.

Aidha alisema vigezo ambavyo vimeangaliwa kuwa mamkala bora ni kugharamia uendeshaji wa mamlaka,kugharamia uchakavu wa miundombinu na kuweza kulipia riba za mikopo ya uwekezaji.

"Lakini pia uwezo wa Mamlaka hiyo kujitegemea kiufundi na kiuendeshaji"

Mkurugenzi huyo alisema kuwa mamlaka hiyo imeweza kuwa ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo miongoni mwa mamlaka kubwa 25 za maji zinazotoa huduma katika makao makuu ya mikoa Tanzania bara.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa alisema wao kama mamlaka wataendelea kuhakikisha wanatoa huduma bora zinazoendena na viwango vikubwa ili kuendelea kuwa mamlaka bora nchini.

Alisema pamoja na changamoto walizokuwa nazo lakini wameweka mikakati kabambe ya kuhakikisha wanakabiliana nazo kwa kuwawezesha wananchi waweze kunufaika ana huduma ya Maji kwa kiwango kikubwa .

"Lakini pia sisi kama mamlaka tumejiwekea mipango kabambe ya kuhakikisha huduma za maji zinaimarika sambamba na kujiandaa na fursa ya ujio wa bomba la mafuta utakaoanzia nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga ili changamoto ya maji isiwepo wakati wa ujio wa fursa hiyo.

habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

MBUNGE COSATO CHUMI AANZA KUTATUA TATIZO LA MAJI KWENYE SHULE ZA JIMBO LA MAFINGA MJINI

$
0
0
Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akikagua pump kwenye moja ya kisima kwenye shule ya Msingi Makalala, anayetizama ni Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi
Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akimsikiliza kwa makini Mhandisi wa Maji wa Mji wa Mafinga Eng Eradius.
Pichani baadhi ya wanafunzi na waalimu wa shule ya Msingi Makalala wakiwa katika picha ya pamoja na Mrs Lee na Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi



na Fredy Mgunda,iringa

MBUNGE wa jimbo Mafinga mjini Cosato Chumi ameendeleza juhudi zake za kuwatafutia maendeleo wananchi wa jimbo lake kwa kufanya kazi kwa ukaribu na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali za nje ya nchi ya Tanzania pamoja na taasisi za ndani.

Hivi karibu balozi wa korea nchini Tanzania Bw Song Geum Young akiwa na NGO ya Kutoka Korea ya World share alitembelea jimbo la mafinga mjini kwa lengo la kujionea changamoto za jimbo hilo na kutafuta njia za kutoa msaada wa kutatua baadhi ya changamoto hizo na walitoa msaada wa taa ndogo za solar kwa kaya masiki mia saba.

Baada ya balozi huyo kurudi jijini Dar es Salaam alimuagiza Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee kutembelea jimbo la mafinga mjini na kuzifanyia tafiti kwa kina baadhi ya changamoto za jimbo hilo ambazo alikuwa amezianisha hapo awali ili kuweza kusaidia kuzitatua.

Aidha mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee alifanikiwa kutembelea baadhi ya shule za jimbo la mafinga mjini na kuzifanyia tafiti changamoto zilizopo kama uhaba wa maji na kuahidi kuzitatua kwa kuwa ameshazifanyia utafiti.

“Leo nimetembelea Shule za Msingi Makalala, Mkombwe, Ndolezi na Mwongozo na Shule ya Sekondari Luganga na nimejionea shida ya upatikanaji wa maji hivyo kwa kuwa NGO yetu inajihusisha na uchimbaji wa visima hivyo tumewasilisha taarifa hizi makao makuu ya ofisi zetu na tunasubili majibu”alisema Bw Donsun Lee.

Bw Donsun Lee alimpongeza mbunge wa jimbo mafinga mjini Cosato Chumi kwa juhudi alizozifanya za kuwashawishi kutembelea jimbo hilo na kujionea baadhi ya changamoto ambazo wanaweza kuzitatua kwa kushiriana na mbunge huyo.

Katika ziara hiyo Bw Lee na timu yake walitembelea Shule za Msingi Makalala, Mkombwe, Ndolezi na Mwongozo na Shule ya Sekondari Luganga. Aidha baada ya tafiti hizo, Bw Lee atawasilisha taarifa zake Makao Makuu ya NGO ya Serving Friends International huko Seoul, Korea.

Nia ya kufanya tafiti hizo ni kuiweka Katika Mipango Halmashauri ya Mji wa Mafinga kwa sababu ndo utaratibu wa NGO hiyo ambayo kwa Sasa wanachimba visima mkoani Singida

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la mafinga Cosato Chumi amemshukuru Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International Bw Donsun Lee kwa kufanikisha kufanya tafiti ambazo amejine mwenye na kuleta matumaini kwa wananchi wa jimbo hilo la kutatuliwa tatizo la maji kwa kuchimbiwa visima na taasisi hiyo.

Chumi ameongeza kuwa haya ni matokeo ya ziara ya Balozi wa Korea ambaye alitembelea jimbo la Mafinga Mwezi mmoja uliopita na kujionea changamoto hizo. Lakini mbunge Chumi amewataka wananchi wa jimbo la mafinga kufanya kazi kwa kujituma na kuunganisha na nguvu za mbunge wao ili kupata maendeleo kwa kasi inayotakiwa.

“Unakuta mbunge nahangaika kuwaletea maendeleo wananchi wangu kama hivi mnavyoona lakini ukienda vijiweni unakuta wananchi wanacheza bao,pooltable na wengi wanapiga soga zisizo na malengo,wakati wangeutumia muda huo kufanya kazi jimbo la mafinga mjini litakuwa na maendeleo ya kasi sio muda”.alisema Chumi

MRADI WA KUONGEZA UJUZI NA IDADI YA WAKUNGA MAENEO YA VIJIJINI NCHINI WATAMBULISHWA MKOANI MWANZA

$
0
0
Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Projestus Rubanzibwa, akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza, kwenye kikao cha Utambulisho wa Mradi wa kuongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi, kilichofanyika hii leo Jijini Mwanza.

Amesisitiza kwamba Wakuu wa Vyuo vya vya Ukunga nchini wanao wajibu wa kuhakikisha kwamba wanatoa mafunzo bora kwa wahitimu wa vyuo hivyo ili watakapohitimu masomo yao waweze kusaidia kutoa huduma bora afya.

Mradi wa kuongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini, unatekelezwa na Shirika la Jhpiego kwa kushirikiana na Taasisi ya Wakunga nchini Canada, Shirika la Amref, Serikari ya Canada, Taasisi ya Wakunga Tanzania na Wizara ya Afya nchini, lengo likiwa ni kuboresha huduma za afya kwa akina mama na mtoto ili kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi maeneo ya Vijijini nchini.

Na BMG
Kaimu Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, Dr.Silas Wambura, akizungumza kwa niaba ya Mganga Mkuu mkoa wa Mwanza, ambapo amesema mkoa wa Mwanza unakabiriwa na upungufu mkubwa wa idadi wa wakunga pamoja na vifaa tiba hali ambayo inasababisha kuwepo kwa vifo vya akina mama na watoto.
Dr.Dustan Bishanga ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Mama na Mtoto Shirika la Jhpiego, amesema lengo la mradi huo ni kuhakikisha unaongeza Ujuzi na Idadi ya Wakunga maeneo ya Vijijini hapa nchini ambapo wahitimu wa masomo ya Sayansi katika maeneo hayo watakuwa wakipewa ufadhiri wa masomo kwa makubaliano ya kurudi kwenye maeneo yao ili kutoa huduma za afya. Mradi huo unatarajiwa kufikia tamati mwaka 2021.
Kikao cha Utambulisho wa Mradi wa kuongeza ujuzi na idadi ya Wakunga katika maeneo ya Vijijini mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kilichofanyika hii leo Jijini Mwanza.
Dr.Dustan Bishanga ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Mama na Mtoto Shirika la Jhpiego, akizungumza na wanahabari kwenye kikao hicho.
Martha Rimoy ambaye ni Mratibu wa Taifa wa Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA), amesema bado maeneo mengi nchini yanakabiloiwa na upungufu wa Wakunga kutokana na idadi ya Wakunga wanaohitimu vyuoni kutoendana na idadi ya ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya huku wengine pia wakishindwa kwenda kufanya kazi maeneo ya Vijijini kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mazingira duni.
Gustav Moyo ambaye ni Mkurugenzi wa huduma za Uuguzi na Ukunga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, amesema hali ya upungufu wa Wakunga nchini hususani maeneo ya Vijijini si nzuri hivyo Serikali inatumia jitihada mbalimbali ikiwemo kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi ili kutatua changamoto hiyo.

Amesema asilimia kubwa ya mikoa ya Kanda ya Ziwa inakabiliwa na upungufu huo na kwamba Serikali itakuwa ikitolea kipaumbele kwenye mikoa hiyo pindi inapotoa ajira kwa Wakunga.
Kikao hicho kimewajumuisha wadau mbalimbali wa afya wakiwemo Wakunga, Waganga Wakuu wa Wilaya na Maafisa Elimu ambao watakuwa na wajibu wa kuwahamasisha wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi ili kuongeza idadi ya Wakunga.

Wadau wa afya kutoka Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Tabora, Kigoma na Mara wameshiriki kwenye kikao hicho.

MKUU WA MKOA WA TANGA SHIGELLA ATEMBELEA BANDARI MKOANI HUMO

$
0
0

Kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella wa kwanza kulia aliyekaa kwenye boti wakati alipofanya ziara ya kuitembelea bandari hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa kwanza kulia akitazama maeneo ya bahari akiwa kwenye boti wakati alipoitembelea kuona namna ya utendaji wao katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi na kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari wa Tanga Henry Arika
Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika wa pili kutoka kulia akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kulia wakati alipofanya ziara ya kuitembelea Bandari hiyo kuona namna inayofanya kazi kwa ufanisi,


Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akishuka kwenye boti la Bandarini akisaidiwa kushuka wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella aliyoitembelea bandari hiyo kuona namna inavyofanya kazi zake


Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga Bandari ya Tanga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella ambaye aliitembelea Bandari hiyo anayefuatia ni Mkuu huyo wa mkoa


Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanda ngazi kuelekea kwenye meli iliyotinga nanga baharini wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella juzi kuona namna inavyofanya kazi zake


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga bandari ya Tanga wakati wa ziara yake ya kuitembelea Bandari hiyo


Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akipanda ngazi kuelekea kwenye meli hiyo akifuatiwa na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga,Faidha Salim wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella


Kaimu Meneja wa Bandari wa Tanga Henry Arika akipanda ngazi kuelekea kwenye meli ya mizigo iliyotia nanga kwenye bandari ya Tanga wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kuitembelea Bandari hiyo kuona shughuli zake anayefuatia ni PRO wa Bandari ya Tanga,Moni Jarufu


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella katikati akiteta jambo na PRO wa Mamlaka ya Bandari ya Tanga,Moni Jarufu wakati wa ziara yake





Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa kwanza kushoto akionyeshwa kitu na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,(Ras) Mhandisi Zena Saidi wakati wa ziara yake ya kuitembelea Bandari hiyo jana


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kushoto katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi wakiteta jambo wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa kuitembelea Bandari hiyo kuona namna inayofanya kazi zake kulia ni PRO wa Bandari ya Tanga,Moni Jarufu




Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akiwa ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika kushoto wa kwaza kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa wakifurahia jambo wakati wakiwa kwenye ziara ya kuitembelea Bandari ya Tanga



Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha Blog

RAIS MAGUFULI AONGOZA MKUTANO WA 17 WA DHARURA WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli na viongozi wenzie wakisimama wakati wimbo wa Jumuiya ukipigwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 17 wa Dharula wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 8, 2016


Sehemu ya waliohudhuria wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Jumuiya ukipigwa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 17 wa Dharula wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es salaam leo Septemba 8, 2016


Ujumbe wa Burundi


Sehemu ya mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa mkutanoni hapo


Wageni kutoka nchi wanachama


Mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa mkutanoni hapo


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiongoza mkutano. Anafuatiwa na Rais Paul Kagame wa Rwanda, Mwakilishi maalum wa Rais wa Sudan ya Kusini Mhe Aggrey Tisa Sabuni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Liberat Mfumukeko


Waziri Mkuu Mstafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kati) na Katibu Mkuu Mstaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Juma Mwapachu (kushoto) wakiwa na viongozi wastaafu wa Jumuiya


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiongoza mkutano. Kushoto kwake ni Rais Paul Kagame wa Rwanda, Mwakilishi wa Rais wa Sudan ya Kusini Mhe Aggrey Tisa Sabuni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein. Kulia kwake ni Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto na mwakilishi wa Rais wa Burundi na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Balozi Alain Aime Nyamitwe


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiongoza mkutano akiwa na Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Liberat Mfumukeko


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano huo


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiendelea na hotuba yake


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akipigiwa makofi na wahudhuriaji


Sehemu ya mabalozi wakisikiliza hotuba ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli


Wanahabari wakirekodi hotuba ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akihutubia


Dkt Mussa Lulandala wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam alikuwa nyota wa mkutano kwa kuweza kufasiri kwa ustadi wa hali ya juu hotuba zote kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili na Kiswahili kwenda Kiingereza
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Balozi Liberat Mfumukeko


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiongea jambo na Rais Paul Kagame


Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo akila kiapo katika mkutano huo.


Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo akitoa heshima meza kuu baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Rais Paul Kagame wa Rwanda akimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto akimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Viongozi na wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakimshangilia Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Viongozi na wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakimpongeza Naibu Katibu Mkuu wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Manaibu Makatibu wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakimpongeza Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumjuiya ya Afrika Mashariki (atayesimamia Utawala na Fedha) Mhe Christophe Bazivamo baada ya kula kiapo katika mkutano huo.


Sehemu ya waliohudhuria


Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda akihutubia


Rais Paul Kagame wa Rwanda akiongea machache


Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto akizungumza machache


Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto akisisitiza jambo


Mwakilishi wa Rais wa Burundi na Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Balozi Alain Aime Nyamitwe akiongea machache


Mwakilishi wa Rais wa Sudan ya Kusini Mhe Aggrey Tisa Sabuni akishukuru kwa nchi yake kukubaliwa kuwa mwanachama kamili wa Jumuiya


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akiongea machache ikiwa ni pamoja na kukumbushia umuhimu wa Sudan ya Kusini kuwa mwanachama wa Jumuiya kwani awali nchi hiyo ilikuwa kiungo muhimu kwa nchi wanachama


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akiendelea kuhutubia


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akisisitiza jambo


Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Liberat Mfumukeko akisoma maazimio ya mkutano


Meza kuu wakisaini na kuridhia maazimio ya mkutano


Wimbo wa Jumuiya ukipigwa kuashiria mwisho wa mkutano


Wageni mashuhuri wakisimama kwa wimbo wa Jumuiya


Viongozi wakisalimiana na waalikwa


Viongozi katika picha ya pamoja na mawaziri kutoka nchi wanachama


Viongozi katika picha ya pamoja na mawaziri kutoka nchi wanachama


Viongozi katika picha ya pamoja na wabunge wa Jumuiya hiyo


Picha ya pamoja na Sekretarieti ya Jumuiya


Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Gerson Msigwa akisimamia shughuli ya picha za pamoja


Viongozi na wageni mashuhuri


Viongozi na wageni mashuhuri


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akimsindikiza Rais Paul Kagame wa Rwanda


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiteta jambo na Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiteta jambo na Naibu Rais wa Kenya Mhe William Rutto


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mmoja wa wageni baada ya kumalizika kwa mkutano huo. PICHA NA IKULU

KAMPUNI YA MIKAELA PROFESSIONAL TAILORS KULITAMBULISHA JIJI LA MWANZA KWENYE UBUNIFU WA MAVAZI

$
0
0
Ofisi za Mikaela Professional Tailors zinapatikana Ghana Green View, barabara ya Airpot Jijini Mwanza. Wapigie kwa nambari 0767 68 28 88 ili wakuhudumie kwa wakati na kwa ubora.


Tofauti na ilivyo katika majiji mengine nchini kama vile Jijini Dar es salaam, Jiji la Mwanza halina mwamko mkubwa katika ubunifu wa mavazi.

Ni kutokana na hali hiyo, Wataalamu na Mabingwa wa Ushonaji wa mavazi ya aina mbalimbali (Kike na Kiume) Jijini Mwanza, Mikalela Professional Tailors, wameahidi kulitambulisha Jiji hilo katika ubunifu wa mavazi ili kuendana na kasi iliyopo katika majiji mengine.

"Awali nilikuwa nateseka sana. Nguo zangu nilikuwa nikishea Jijini Dar au Arusha na nikizivaa watu wengi wakawa wanauliza niliposhonea na kutamani niwapeleke. Nikaona kumbe Mwanza kuna uhitaji mkubwa wa ubunifu na ushonaji wa mavazi hivyo nikaamua kuanzisha kampuni ya ubunifu na ushonaji wa mavazi ya Mikaela Professional Tailor ili kukata kiu hiyo.

DC STAKI: APIGA MARUFUKU KUFANYA BIASHARA KWA KUJAZA RUMBESA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule akikagua magunia yaliyokutwa yakiwa yamejazwa Rumbesa
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule akizungumzia unyonyaji wanaokumbana nao wananchi kutoka kwa wafanyabiashara wanaotaka magunia yaliyojazwa Rumbesa
Gari aina ya Fuso likiwa limekamatwa mara baada ya kubainika kuwa limebeba magunia ya vitunguu ambayo yamejazwa Rumbesa

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Anna-Claire Shija akisisitiza jambo wakati wa mkutano na wananchi Wilayani humo

 Dc Staki akikagua mashamba ya wakulima mara baada ya kuzuru katika maeneo hayo


 Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na wananchi
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo wakisikiliza malalamiko ya wananchi

Na Mathias Canal, Kilimanjaro

Wakulima wa mazao mbalimbali likiwemo zao la vitunguu wametakiwa kutofanya biashara kwa kujaza rumbesa ili kuwanufaisha wafanya biashara ambao wanajitokeza vijijini kunua mazao kwani jambo hilo linawanyonya zaidi wakulima na kuwanufaisha wafanya biashara.

Marufuku hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki Senyamule mara baada ya kuitisha mkutano wa wananchi katika ziara yake ya kuwahimiza kwa pamoja kujitokeza kushiriki katika zoezi la upimaji ardhi linaloendeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Same.

Hata hivyo lengo mahususi la kuamua kuwapo kwa zoezi la upimaji ardhi ni kutaka kuondoa migogoro ya ardhi iliyokithiri katika maeneo mbalimbali Wilayani humo sambamba na kupinga kipimo cha Rumbesa kinachowanyonya wakulima wengi nchini.

Katika mkutano huo uliofanyika Katika Kitongoji cha Jitengeni na Mvungwe uliwahusisha pia wataalamu wa kilimo na ardhi kutoka katika Halmashauri ya Wilaya hiyo sambamba na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama katika Wilaya hiyo.

Katika mkutano huo Mkuu wa Wilaya hiyo aliwataka wakazi wa Kijiji cha Ruvu Jiungeni kushiriki kikamilifu katika zoezi la upimaji ardhi hivyo kuwaarifu pia wananchi wote kujitokeza katika mashamba yao wakati wa zoezi la upimaji ili kuondoa adha inayochochea migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Dc Staki alisema kuwa wananchi wanapaswa kupinga kuzidisha kipimo halisi kinachokubalika kwani kutofanya hivyo ni kukubali kupunjwa na kuinyima Halmashauri mapato.

Alisema kuwa wakulima wanapaswa kujiamini kwani mazao wanayolima yana soko popote nchini hivyo kidanganywa kwa kuweka Lumbesa ni kujinyima haki yao ya msingi katika kukabiliana na wimbi la umasikini.

Aidha kabla ya mkutano na wananchi Dc Staki alitembelea mashamba ya vitunguu na kujionea jinsi ambavyo Rumbesa inavyofungwa.

Sambamba na hayo pia Mkuu huyo wa Wilaya alimtaka mkuu wa Polisi Wilaya ya Same Asteriko Maiga kusimamia na kulikemea suala la Rumbesa kwenye mageti yote na endapo watawabaini wafanya biashara wanaofanya hivyo wanapaswa kukamatwa na kuchukuliwa hatua.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Anna-Claire Shija alisema kuwa wananchi wanapaswa kuwa makini katika kuimarisha kilimo na kujitokeza kwa wingi katika shughuli za maendeleo.

WAZIRI MBARAWA AZINDUA GATI JIPYA PANGANI, TANGA LAGHARIMU ZAIDI YA BILIONI 3

$
0
0

WAZIRI wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Proffesa Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Karim Mattaka wakati alipofanya ziara ya kuzindua gati mpya wilaya ya Pangani Mkoani Tanga katikati ni Meneja wa Tanroad Mkoani Tanga,Mhandisi Alfred Ndumbaro


Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Proffesa Makame Mbarawa akizundua gati jipya la Bandari ya Pangani ambalo liligharimu zaidi ya bilioni 3 kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano wa mwisho kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA)Karim Mattaka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella


Kulia ni Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Proffessa Makame Mbarawa akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)Karim Mattaka wapili kutoka kulia wakati wa uzinduzi wa gati jipya wilayani Pangani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika akifuatilia mazungumzo hayo





Viongozi waliokaa meza mkuu wakifuatilia matukio yaliyokuwa yakiendelea wakati wa uzinduzi wa Gati Jipya wilayani Pangani 




Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM),Jumaa Aweso wakifuatilia hafla ya uzinduzi wa Gati jipya wilayani Pangani


Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani na mkoaani Tanga wakifuatilia uzinduzi wa Gati jipya


Baadhi ya watumishi wa Mamlaka ya Bandari Mkoani Tanga wakifuatiliaa uzinduzi huo kutoka kulia ni PRO wa Mamlaka hiyo,Moni Jarufu kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Daudi Mayeji


Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani wakifuatilia uzinduzi wa Gati hiyo




Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Proffessa Makame Mbarawa akisalimiana na wananchi wilayani Pangani mara baada ya kuzindua gati jipya


Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Proffessa Makame Mbarawa akiwa na viongozi mbalimbali akisoma maelekezo yaliyoandikiwa kwenye jiwe la msingi mara baada ya kufanya kuzindua gati jipya la Bandari wilayani Pangani kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Karim Mattaka kulia ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika,Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella na PRO wa Mamlaka ya Bandari ya Tanga,Moni Jarufu.

MLIMBWENDE WA OZONA MISS LAKE ZONE 2016 APATIKANA

$
0
0
Jumamosi Septemba 10, 2016 kuamkia leo jumapili, kinyang'anyiro kikali cha kumsaka mlimbwende wa Kanda ya Ziwa, (OZONA MISS LAKE ZONE 2016), kimefanyika ambapo Mlimbwende, Eluminatha Dominick (pichani) kutoka mkoani Geita ameibuka mshindi miongoni mwa walimbwende 17 (baada ya mmoja kujitoa) waliokuwa wakiwania taji hilo.

Ushindi wa mlimbwende huyo ulionekana kuwafurahisha mamia ya watu waliohudhuria kwenye shindano hilo lililofanyika kwenye Viunga vya Rock City Mall Jijini Mwanza, likiwa nimeandaliwa na kampuni ya Flora Talent Promotions chini ya Mkurugenzi wake, Flora Lauwo na kudhaminiwa na makampuni mbalimbali ikiwemo mdhamini mkuu, kampuni ya vipodozi ya OZONA pamoja na 102.5 Lake Fm Mwanza.

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Mhe.Jeseph Linzwa Kasheku Msukuma, alisema ni furaha kubwa mkoa wa Geita kunyakua taji la Ozona Miss Lake Zone 2016 na kwamba matarajio ni kujiandaa vyema kwa ajili ya kunyakua taji la Miss Tanzania 2016 ikiwa ni sawa sawa na matarajio aliyoyaeleza mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016.

Na BMG
Mlimbwende, Eluminatha Dominick (pichani) kutoka mkoani Geita ameibuka mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, miongoni mwa walimbwende 17 waliokuwa wakiwania taji hilo.
Mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (katikati) kutoka mkoani Geita. Mshindi wa pili ni Mery Peter (Miss Mwanza 2016, kushoto) na Mshindi wa tatu ni Lucy Michael (Geita, kulia).
Mlimbwende wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (katikati) kutoka mkoani Geita. Mshindi wa pili ni Mery Peter (Miss Mwanza 2016, kushoto) na Mshindi wa tatu ni Lucy Michael (Geita, kulia).
Aliyekuwa akishikilia taji la Miss Lake Zone
Aliyekuwa Miss Lake Zone (kulia), akikabidhi taji la Miss Lake Zone mpya (kushoto)
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaa ya Nyamagana, Mhe.Mary Tesha (kushoto) akimkabidhi mshindi wa Ozona Miss Lake Zone mfano wa ufunguo wa gari alilokabidhiwa kama zawadi. Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone amewazadiwa gari lenye thamani ya shilingi Milioni 12 na kampuni ya Ozona.
Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mary Tesha, Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick, Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ozona, Dr.Thobias Mkina, wakiwa katika picha ya pamoja.
Mshindi wa Ozona Miss Lake Zone 2016, Eluminatha Dominick (kushoto) akiwa katika picha na Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini, Joseph Msukuma (kulia).
Washiriki walioingia nafasi tano bora ni, Eluminatha Dominick (wa pili kushoto kutoka Geita), Mery Peter (wa tatu kushoto kutoka Mwanza, Lucy Michael (wa kwanza kushoto kutoka Geita), Rose Masanja (wa pili kushoto kutoka Shinyanga) na Farida Hassan (wa kwanza kulia kutoka Mara).
Washiriki 17 wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Ozona Miss Lake Zone akizungumza na Wanahabari baada ya kukabidhiwa gari
Mchekeshaji Eric Omond kutoka nchini Kenya akizungumza na Vesterjtz wa BMG baada ya show
Kushoto ni Christian Bella, akizungumza na Vesterjtz wa BMG baada ya kudondoka burudani kali
Katikati ni mbunge Joseph Msukuma akizungumza na BMG
Kulia ni mmoja wa wanakamati akihojiwa na BMG
George Binagi-GB Pazzo (ushoto) katika picha ya pamoja na Christian Bella (kulia) baada ya show
Mwanahabari Sadam Sadick (kulia) akishow love na Bella
Ozona Miss Lake Zone 2016 (kushoto) akiwa na Vesterjtz
Kijukuu kutoka RFA akiwa na Ozona Miss Lake Zone 2016
Mambo ya karanga fotooo na Ozona Miss Lake Zone 2016
Bonyeza HAPA Kwa Picha za Awali

DC IKUNGI AITAKA SHANTA GOLD MINE KUWALIPA FIDIA WANANCHI ILI KUPISHA UCHIMBAJI WA DHAHABU

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi
Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi wakijadili jambo nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya kabla ya kuingia kwenye kikao
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu akielezea namna ambavyo watawalipa wananchi 67 ndani ya wiki hii


Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho kushoto kwake ni Kaimu katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi Dijovson Ntageki na wengine ni wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo
Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi wakisikiliza kwa makini maelezo ya mkuu wa Wilaya

Kamishina wa Madini Kanda ya Kati Sospita Masorwa akielezea namna ambavyo uthamini unakuwa umekamilika kuwa ni mara baada ya Mthamini Mkuu wa serikali kupitisha
Kutoka kushoto ni Afisa Tarafa ya Ikungi Josephine, Kamishina wa Madini Kanda ya Kati Sospita Masorwa, Ally Kassim Mjiolojia kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Meneja Mkuu Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu, David Rwechungura Meneja Rasilimali watu kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, na Daniel Mwita

Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akifunga kikao mara baada ya maridhiano
 
Na Mathias Canal, Singida

KAMPUNI ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining  Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida imetakiwa kuwalipa wananchi 69 waliosalia kulipwa fidia zao kwa ajili ya kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kufuatia malalamiko ya wananchi wa maeneo mbalimbali waliopo kwenye eneo la mradi huo waliotaka kufahamu hatima ya malipo yao kutokana na awamu ya kwanza kuonyesha kuwa watu 67 ndio watakaolipwa mwishoni mwa wiki hii na wengine waliobaki kulipwa katika awamu zijazo.

Dc Mtaturu ametoa agizio hilo wakati wa kikao cha pamoja kilichohudhuriwa na Wawakilishi wa kampuni ya Shanta Gold Mine Ltd, Wananchi wawakilishi kutoka Kijiji Cha Mlumbi na Uongozi wa kikosi kazi ambacho kilipewa jukumu la kuhakikisha wananchi wote ambao watapitiwa na mradi huo wanalipwa fidia sambamba na kusimamia uhamishaji wa makazi.

Kapuni ya Shanta Gold Mine ltd imetakiwa kutumia siku 68 yaani hadi kufikia mwezi Novemba mwaka huu kumaliza malipo ya watu 69 kati ya 136 ambao wanatakiwa kulipwa katika awamu ya pili ili wananchi hao waweze kupisha mradi huo ambao kwa kiasi kikubwa umeshindwa kuanza uchimbaji wa madini aina ya dhahabu kutokana na malalamiko ya malipo ya fidia kwa baadhi ya wananchi ambao tayari wamefanyiwa uthamini wa maeneo yao.

Sambamba na hayo pia Mkuu huyo wa wilaya ameagiza kikosi kazi kuendeleana kazi yake mpaka pale malipo ya wananchi hao yatakapokamilika pamoja na kuwapo kwa maneno kuwa kilivunjwa mwanzoni mwa mwezi wa tatu, jambo ambalo limepingwa vikali na uongozi huo wa Wilaya.

Kwa upande wake Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mine Ltd Philbert Rweyemamu amesema kuwa kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi hao juu ya kutaka wananchi wote walipwe kwa wakati mmoja jambo ambalo sio rahisi kutokana na pesa iliyopatikana kutoka kwa wawekezaji wa hisa tangu mwaka 2012 mpaka sasa bado inatumika haijaanza kuingiza faida hivyo malipo ya awamu yatakuwa muarobaini wa malipo hayo mara baada ya kuanza kwa uchimbaji hivyo kadri mradi unavyoendelea kuchelewa kuanza ndivyo ambavyo fedha inapoteza thamani.

Hata hivyo amejibu hoja ya wananchi kuwa Kampuni hiyo ndiyo ilileta Mthamini wa maeneo ya wananchi jambo ambalo halina ukweli halisi kwani wananchi wenyewe ndio walioamua juu ya Mthamini wanayemtaka kutokana na makubaliano yao.

Rweyemamualisema kuwa endapo kama mradi huo ungeanza mapema kama vile ilivyokuwa imepangwa ni dhahiri sasa ungekuwa umezalisha ajira zaidi ya mara tano kwa wakazi wa maeneo husika na Taifa kwa ujumla jambo ambalo lingerahisisha kuongeza pato la wananchi wa Wilaya husika na Taifa kwa ujumla.

Naye Mwenyekiti wa wananchi walio katika eneo la mradi huo Ramadhani Said Nyeriamesifu juhudi za utendaji kazi wa serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kumteua Mkuu huyo wa Wilaya ambaye anaonyesha maslahi mapana na wananchi kutokana na juhudi mbalimbali za utendaji kazi.

Pamoja na pongezi hizo Nyeri amesema kuwa endapo viongozi mbalimbali wa serikali watafanya kazi kwa mazoea kwa kutumia vibaya nafasi zao ni dhahiri kuwa lawama na malalamiko ya wananchi yatakuwa laana kwao.

Nyerialisema kuwa kikosi kazi hicho kilianza kazi hiyo mwaka 2014 ambacho kilianzishwa na Kampuni ya Shanta gold Mine ltd kwa makubaliano na wananchi wa maeneo husika ambapo katika kipindi chote hicho vimefanyika vikao vitano ambavyo viliendeshwa vyema pasina malalamiko kwa upande wowote ule.

Akifunga kikao hicho Dc Mtaturu alisema kuwa katika makubaliano ya namna ya kuendesha utendaji kazi wa kikosi kazi hicho mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Tundu lissu alipaswa kuwepo lakini hajawahi kushiriki hata kikao kimoja jambo ambalo kwa kiasi kikubwa linaashiria mbunge huyo kukimbia majukumu yake kama muwakilishi wa wananchi.

Aidha amekipongeza kikosi kazi hicho kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya kwa kipindi chote hicho huku akiitaja miaka 10 waliyofanya kazi kumekuwa na daraja kutokana na baadhi ya viongozi kukimbia majukumu yao na kuwaacha wananchi kujishughulikia na kumaliza matatizo yao wao wenyewe.

MUWSA WASAFISHA MIFEREJI YA MAJI TAKA KITUO KIKUU CHA MABASI MJINI MOSHI

$
0
0
Tope zilizokuwa zimetuama katika mifereji ya kusafirisha maji taka katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi zikiondolewa.

Licha ya kuwepo na kampuni iliyopewa kandarasi ya usafi katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Moshi bado changamoto ya kuziba kwa mifereji ya kusafirisha maji taka imekuwepo .



Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) walishiriki kuzibua na kuondosha taka zote zilizokuwepo katika mifereji hiyo.





Kitengo cha maji taka cha Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi kilihusika zaidi kuhakikisha hakuna mfereji utakao kuwa umebaki na taka.





Taka ngumu zote ziliondolewa katika mifereji hiyo.



Baadhi ya wafanyabiashara katika kituo hicho kikuu cha mabasi walijitokeza pia katika kusaidia kufanya usafi .

Wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukailisha zoezi la usafi katika kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi.




Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

MKURUGENZI MTEULE WILAYA YA MBULU,AANZA KAZI KWA KUMTANGULIZA MUNGU

$
0
0

Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga, ambaye ameteuliwa mwishoni mwa wiki jana amesema anaamini ni Mungu aliyemuweka kwenye nafasi hiyo ili  awatumikie wananchi wa Mbulu kwa wakati huu. 

Akiongea kwenye ibada ya Jumapili hii  ndani ya  Kanisa la Living Water Center Kawe, wakati alipopewa nafasi na mtumishi wa  Mungu  Apostle Onesmo Ndegi  ili asalimia Kanisa Mheshimiwa Kamonga  alisema, anakwenda kwenye wilaya yenye changamoto nyingi za kimaendeleo ila anaamini Mungu atamwezesha kuzitatua kwa nafasi yake akishirikina na wananchi pamoja na  viongozi wengine kati halimashauri ya Mbulu.

Kamonga alisisitiza kuwa kwa kupata  nafasi hii ya  Ukurugenzi bado  ataendelea na utumishi wake kwa Mungu maana anaamini huo ndio uliomfanya kufikia hatua hiyo,hivyo kuamua kuwa anamtanguliza Mungu kaika kila atakachokuwa anafanya,alisema Kamoga

Pia alitoa shukurani za dhati kwa Mtumishi wa Mungu Apostle Ndegi pamoja na  watumishi wengine kanisani hapo na kusema kuwa kati ya vitu ambavyo hawezi kuvisahau na malezi mazuri ya kiroho pamoja na mafindisho ambayo amekuwa akiyapata kutoka  kwa Apostle Ndegi na watumishi wengine kanisani hapo, akisema mafundisho hayo yamesababisha kuwa vile alivyo sasa! Mwisho Mtumishi wa Mungu Mtume Onesmo Ndegi  na waumini walifanya maombi kwa ajili yake ili Mungu aambatane naye katika utumishi wake kwenye nafasi hiyo ya Ukurugenzi!.


Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga


Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga akiwa na Baba yake wa Kiroho Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimsiliza kwa makini akielezea uteuzi wake.

Mkurugenzi mteule wa Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga akiwa na Baba yake wa Kiroho Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimsiliza kwa makini akielezea uteuzi wake.
Apostle Onesmo Ndegi Kiongozi wa Kanisa la Living Water Center Kawe akimwombea Hudson Kamogaakiwa amepiga magoti
Waumini wa Kanisani Living Water Center Kawe wakiwa wamenyoosha mikono kwa Hudson Kamoga kuomba kwa ajili yake

MAKAMU WA RAIS MHE SAMIA ASHIRIKI UAPISHO RAIS WA 6 WA ZAMBIA MJINI LUSAKA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akipungia mkono maelfu ya wananchi waliokuwa wakimshingilia wakati akiingia kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016

Rais Robert Mugabe akisalimiana na Rais wa Kwanza wa Zambia Dkt Kenneth Kaunda


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Botswana Luteni Jenerali Seretse Khama baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Rais wa Kenya Mhe william Rutto, Makamu wa Rais wa Namibia Mhe. Nickey Iyambo na Rais wa kwanza wa Zambia Dkt. Kenneth Kaunda baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiwa na Naibu Rais wa Kenya Mhe william Ruttona wageni wengine wakielekea jukwaani kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka ambako amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akipitia ratiba kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka ambako kamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wakiwa kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka ambako kamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Rais mteule wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu akiwasili kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kwenye sherehe za kuapishwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Rais mteule wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu akipokea heshima ya mizinga 21 kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kwenye sherehe za kuapishwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Rais mteule wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu akiwa na mkewa Mama Esther Lungu kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kwenye sherehe za kuapishwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Rais mteule wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu akila kiapo kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka kwenye sherehe za kuapishwa kwake kuwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia leo Septemba 13, 2016


Taswira ya Makamu wa Rais wa Zambia Mama Inonge Mutukwa Wina akila kiapo ikionekana kqwenye luninga kubwa kwenyeUwanja wa Taifa wa Mashujaa jijini Lusaka leo Septemba 13, 2016


Rais Robert Mugabe wa Zambia akizungumza kwa niaba ya viongozi waalikwa wote


Ndege vita zikipita angani


Rais Edgar C. Lungu akielekea kukagua gwaride la heshima baada ya kula kiapo


Rais Edgar C. Lungu akikagua gwaride la heshima baada ya kula kiapo


Rais Edgar C. Lungu akielekea jukwa kuu baada ya kukagua gwaride la heshima


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi walikwa wengine kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Ndege vita zikipamba sherehe angani


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akimpongeza Makamu wa Rais wa Zambia Mama Inonge Mutukwa Wina kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wakisimama na kushiriki dua kwenye uwanja wa Taifa wa Mashujaa (National Heroes Stadium) jijini Lusaka baada ya shughuli za kuapishwa Rais Lungu.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akinong'onezwa jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Michezo na Maendeleo ya watoto Mhe. Agnes Musunga baada ya sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan akiongea na mwandhi wa habari wa ZNBC baada ya sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Awamu ya 6 wa Zambia Mhe Edgar C. Lungu leo Septemba 13, 2016. 

PICHA NA IKULU
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live