Quantcast
Channel: Matukio
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live

WIZARA YA AFYA KUFANYA UZINDUZI WA KONDOMU MPYA MKOANI MWANZA

$
0
0
Baada ya juzi Agost 30,2016 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kuzindua aina mpya ya Kondomu iitwayo Zana Kondomu mkoani Mbeya, Uzinduzi kama huo unatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Septemba 05,mwaka huu.

Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni (pichani), jana alisema mkoa wa Mwanza unatarajia kupokea ugeni kutoka wizara hiyo ambao utajumuisha wataalamu mbalimbali wa afya watakaokuwa wakitoa semina na elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kutumia vyombo vya habari, wakielezea juu ya uzinduzi wa kondomu hiyo.

Alisema miongoni mwa dhumuni la kuzindua aina hiyo mpya ya Kondomu, ni kusaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukwimwi ambapo Wizara itakuwa ikigawa bure kondomu hizo zenye ubora kwa wananchi, kote nchini.
Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni
Baadhi ya Wanahabari mkoani Mwanza, wakimsikiliza Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza.

MBUNGE MUFINDI KASKAZINI ATOA MSAADA WA AMBULACE JIMBONI KWAKE

$
0
0


MBUNGE wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa akikabidhi gari hilo kwa viongozi wa wilaya ya mufindi
MBUNGE wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa akikabidhi gari hilo kwa viongozi wa wilaya ya mufindi huku wananchi wakiwa kwa pembeni

na fredy mgunda,iringa

Gari la kubebea wagonjwa [Ambulance] lenye thamani ya mill.80 lakabidhiwa katika kwa mkurugenzi na mkuu wa wilaya wa Mufindi na MBUNGE wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa ametoa msaada wa gari la kubeba wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya matumizi ya hospitali ya wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa iliyopo katika jimbo lake hilo.

Mgimwa alikabidhi gari hilo ikiwa ni moja ya ahadi yake aliyoitoa wakati akiomba kura kwa wananchi wa jimbo la mufindi kaskazini katika kampeni ya uchaguzi mkuu 2015,ambapo alisema kutokana na changamoto ya uhaba wa gari ya kubebea wagonjwa katika zahanati na vituo vya afya katika jimbo hilo, endapo atapewa ya kuwa mbunge atahakikisaha gari ya wagonjwa linapatikanaili wagonjwa waweze kufika hospital kwa wakati.

Akizungumza na wananchi wakati wa kukabidhi gari hilo,mbunge Mgimwa alisema muda wa kupiga siasa umeshapita na kazi iliyopo hivi sasa ni kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuwatatulia changamoto zinazowakabili.

Alisema pamoja na kuongeza gari ya wagonjwa atahakikisha anaboresha vituo vya Afya vilivyopo katika jimbo lake ili kupunguza wimbi kubwa la msongamano wa wagonjwa wanaokuja kutibiwa katika Hospitalini ya wilaya.

‘’’Nipo kwenye mchakato wa kuboresha vituo vyote vya Afya ndani ya jimbo langu,na nitahakikisha huduma muhimu zinapatikanaikiwa pamoja na dawa za kutosha na vifaa mbalimbali vinavyohitajika ili wananchi wangu waweze kuhudumiwa bila usumbufu katika vituo hivyo,hii itasaidia kupunguza msongamano katika hospitali ya wilaya’’’’’alisema Mgimwa

Aidha katika mkutano huo mbunge alisisitiza swala la uaminifu kwa watumishi waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wahakikishe wanajikinga na vitendo vinavyoashiria rushwa ,vinavyoweza kuwaharibia sifa ya utendaji kazi zao na kushindwa kuwajibika ipasavyo katika majukumu yao.

‘’’Sisi wabunge,madiwani na mtumishi yeyote aliyepewa dhamana na wananchi anatakiwa ajiepushe na swala zima la rushwa ili aweze kutenda haki kwa kuwatatulia changamoto wananchi wake waliomchagua. Tunatakiwa tuwatumie wananchi kuwaletea maendeleo ipasavyo na si vinginevyo’’’alisema

Jamhuri William ni mkuu wa wilaya ya Mufindi,akipokea msaada wa gari hilo kutoka kwa mbunge Mgimwa alisema gari hilo litaweza kusaidia kuokoa vifo vya wanamufindi hasa mama na mtoto ambapo hapo awali kuliwa na gari moja tu.

Williamu alisema kutokana na uwingi wa wagonjwa wanaoenda kutibiwa katika hospitali ya wilaya kwa mwezi ni zaidi ya 500 aliosimia kubwa ni akina mama wajawazito na wengi wao wanafikishwa wakiwa katika hali mbaya kutokana na gari la wagonjwa kuwa moja na kushindwa kumudu.

“Tunamshukuru mbunge kwa kuliona hili na na kuokoa maisha ya watu hasa mama na mtoto ingawa bado hitaji lipo kutokana na uwingi wa wagonjwa endapo tutapata gari la tatu itasaidia sana”alisema

Williamu ameongeza kwa sasa gari hilo litahudumiwa na wilaya kuanzia kuwalipa wafanyakazi wa gari hilo,kulifanyia marekebisho ya gari hilo endapo litatokea kuharibika kwa aina yoyote ile.

Wananchi nao walitoa malalamiko yao kwa mbunge Mgimwa,ambapo Markusi Chusi alimuomba mbunge aweze kusiomamia swala la utapikananji wa vibali vya kuvuna miti,kwa kumtaka ahakikishe wazawa wa eneo husika wanapewa kipaumbele ili waweze kunufaika mali alisi hiyo ilipo kwako.

‘’’’Tumelia kwa muda mrefu,sisi tunanyanyasika kwa kuwapendelea wageni na kutuacha sisi wenyeji tuliopo hapa.Nimeomba mara tano hivi sasa na ukizingatia mimi ni mjane lakini naachwa na pesa yangu inaliwa wageni wanapewa hali inayotukatisha tama wananchi tuliouzunguka msitu huu.’’’’alisema


MBUNGE wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa akifurahia jambo na viongozi wa wilaya ya mufindi
MBUNGE wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa na viongozi wa wilaya ya mufindi wakiangalia muonekano wa wa gari hilo la kubebea wagonjwa
na hii ndio sehemu ya ndani ya gari la kubebea wagonjwa alilokabizi mbunge wa Mufindi kaskazini,Mahamood Mgimwa akikabidhi gari hilo kwa viongozi wa wilaya ya mufindi.



SHINDANO LA OZONA MISS LAKE ZONE 2016 LAZINDULIWA RASMI JIJINI MWANZA

$
0
0
Shindano la Ulimbwende la "Ozona Miss Lake Zone 2016" linaloshirikisha Walimbwende 18 kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa limezinduliwa rasmi hii leo Jijini Mwanza.

Shindano hilo litakalofanyika jumamosi Septemba 10,2016 katika Ukumbi wa Rock City Mall, limeandaliwa na Flora Promotions na kupewa nguvu na wadhamini mbalimbali akiwemo mdhamini mkuu, Kampuni ya vipodozi ya Ozona ambayo imetoa zawadi ya gari lenye thamani ya shilingi Milioni 12 kwa mshindi wa kwanza.

Katika picha, kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Ozona, Dr.Thobias Mkina, akizungumza katika uzinduzi wa shindano hilo ambapo kushoto ni Mkurugenzi wa Flora Promotions, Flora Lauwo.

Na BMG
Wadau mbalimbali Ozona Miss Lake Zone wakiwa kwenye uzinduzi wa shindano hilo hii leo
Wadau mbalimbali Ozona Miss Lake Zone wakiwa kwenye uzinduzi wa shindano hilo hii leo
Mkurugenzi wa Flora Promotions, Flora Lauwo, akiteta jambo kwenye uzinduzi wa shindano la Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Baadhi ya Washiriki wa Ozona Miss Lake Zone 2016
Mzee wa Masauti, Christian Bella pamoja na Mchekeshaji Erick Omond wanatarajiwa kuungana na watumbuizaji wengine pamoja na wadau wengine kwenye kufanikisha Usiku wa Ozona Miss Lake Zone 2016.

MGODI WA BULYANHULU UMETOA MILIONI 100 KWA AJILI YA MADAWATI MKOA WA GEITA

$
0
0
Naibu Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jafo akihutubia wadau wa kampeni ya kuchangia Madawati Mkoa wa Geita kwenye Harambee iliyofanyika Mjini Geita

Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii katika Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Elias Kasitila akitoa maelezo kuhusu namna Acacia ilivyoshiriki mwaka huu kuchangia kwenye zoezi la madawati.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Bwana Graham Crew akiwa amenyoosha mikono kusalimia umma wa Watanzania waliongana kwenye harambee ya madawati Geita


Timu ya Wafanyakazi wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri baada ya Meneja wa Ustawi na Mahusiano ya Jamii katika Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Elias Kasitila kutanga kuwa Mgodi utatoa shilingi milioni Mia Moja kwa ajili ya madawati Mkoa wa Geita.



Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog.

Mgodi wa Dhahabu Bulyanhulu Umetoa Tsh 100m/- kwa Ajili ya Madawati ya Shule Mkoani Geita.

Akitangaza kiwango hicho katika hafla ya changizo iliyofanyika Desire Park Mjini Geita , Meneja Ufanisi na Mahusiano na Jamii wa Mgodi wa Dhahabu Bulyanhulu bwana Elias Kasitila amesema, “Bulyanhulu imebarikiwa kuwa karibu na Wilaya mbili,Halmashauri ya Msalala iliyopo Mkoa wa Shinyanga na Nyang’wale iliyopo Mkoa wa Geita.

“ Hivyo basi tulipopokea mwaliko kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Nyang’wale kuhusu kampeni ya leo ya madawati tumeamua kwamba japokuwa miradi mingine ya madawati tumeifanya mkoa wa Shinyanga tumeona kuna umuhimu wa kufanya hivyo mkoa wa Geita pia.”alisema Kasitila.

"Hivyo basi siku ya leo tunajitolea kuchangia Tsh100m/- kwa ajili ya kampeni za mikoa inayolenga kuondoa upungufu wa madawati 70,000.”aliongeza Kasitila.

Elias aliongeza kuwa, “misaada ya madawati kutoka kwenye migodi iliyoko chini ya Acacia ambayo ni, North Mara, Buzwagi and Bulyanhulu,kwa mwaka huu Acacia imetumia takriban fedha za kitanzania zaidi ya Billion Moja ambayo inakadiliwa kutengeneza zaidi ya madawati 10,000.

Mgeni rasmi katika hafla ya kuchangia madawati mkoa wa Geita alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ambaye aliwakilishwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi ,Utumishi na Utawala Bora, Mh.Suleiman Jafo.

Akiwahutubia washika dau waliokuwa Desire park Naibu Waziri Jafo alisema “Nitapeleka salamu kwa waziri mkuu kuhusiana na mwitikio ambao nimeushuhudia leo ninaagiza kamati ya Kampeni ya madawati Geita kuorodhesha washika dau wote waliochangia leo na kuwasilisha orodha hiyo kwenye ofisi ya Waziri Mkuu ili binafsi awatambue wote walioonesha kuguswa kuiondolea Geita uhaba wa madawati.”

Katika hafla hiyo Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Aacacia Bulyanhulu Graham Crew binafsi alijitolea kuchangia fedha za kitanzania shilingi 750,000/- kwa ajili ya kampeni hiyo.





WATANZANIA WACHANGAMKIA KUPATWA KWA JUA NA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII.

$
0
0
Wafanyabiashara wa tikiti maji wakitumia tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali kuuza matunda hayo kwa wananchi waliofika katika eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa Jua.
Wafanyabiashara wa Mchele wao pia hawakubaki nyuma wakatumia fursa hiyo kuuza Mchele kwa wananchi waliofika kushuhdia tukio hilo.

Mama lishe pia hawaubaki nyuma kuhakikisha wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo .
Benki ya NMB pia walitoa huduma ya kufungua Akaunti kwa wananchi waliofika katika eneo hilo kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Umati mkubwa wa wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yaiendelea katika eneo hilo.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ,Amosi Makala akizungumza juu ya fursa za kiuchumi zilizojitokeza kutokana na tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali.
Mkuu wa Mkoa wa Songe Luteni Mstaafu ,Chiku Galawa akizungumza na wananchi waliofika katika eneo hilo kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA ,Pascal Sheluetete akizungumza na wanahabari ambapo shirika hilo limetangaza kufungua lango la Ikoga kwa ajili ya kuingia Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa upande wa Bonde la Ihefu.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Songwe,Luteni Mstaafu ,Chiku Galawa walipokutana kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Amosi Makala,(katikati) ,Mkuu wa Mkoa wa Songwe ,Chiku Galawa na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA) Pascal Shelutete wakitizama tukio la kupatwa kwa jua ka kutumia miwani maalumu za kutizamia.
Hatua ya mwanzo ya tukio la kupatwa kwa jua ,baada ya mwezi kuanza kupita mbele ya Jua na kuanza kuzuia mwanga usifike katika uso wa Dunia.
Mwezi ukiwa umebakiza kipande kidogo wakati ukipita mbele ya jua.
Mwezi ukiwa katikati ya jua na kutengeneza kipete.
Mwezi ukiwa umeanza safari ya kuliachia jua.
Baadhi ya wananchi wakitizama tukio hilo .
Wengine walilazimika kutumia miwani maalumu kwa ajili ya kuchomea vyuma kutizama tukio hilo.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Mbarali ,Mbeya.

KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MWANAHABARI DAUDI MWANGOSI, UTPC YALILIA MAZINGIRA HURU KWA WANAHABARI KUFANYA KAZI

$
0
0
Septemba 2,2012 Mwandishi wa Habari, Marehemu Daudi Mwangosi (hayuko pichani), aliyekuwa pia Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Iringa, aliuawa na polisi akiwa kazini katika Kijiji cha Nyololo mkoani Iringa ambapo aliyemuua alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani julai mwaka huu.

Na BMG

Kufuatia mauaji hayo, Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini, UTPC ulitenga tarehe hiyo kuwa kumbukumbu ya Kifo cha Daudi Mwangosi ikiambatana pia na tuzo inayotolewa kwa mwanahabari aliyefanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo kupigwa ama kuuawa kutokana na kazi yake.

Leo UTPC imekutana na wanahabari Jijini Mwanza imekutana na wanahabari ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya kifo cha Mwangosi ambapo imelaani mazingira magumu ambayo wakati mwingine wanahabari na vyombo vya habari wanayapitia katika utendaji wao wa kazi ikiwemo vyombo vya habari kufungiwa.
Makamu wa Rais wa UTPC, Jane Mihanji (kushoto) amesema wanahabari wanataka mazingira huru ya kufanya kazi huku akilaani serikali kuvifungia baadhi ya vyombo vya bila kusikilizwa juu ya yale yanayodhaniwa kufanywa na vyombo hivyo kinyume cha sheria.

Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan, amebainisha kwamba tunzo ya Daudi Mwangosi mwaka huu pia haikupata mshindi kwa namna ambavyo jopo la tuzo hiyo lilivyoweka vigezo vyake ikiwemo Mwandishi anayepaswa kuichukua awe amepigwa, kuumizwa ama kuuawa akiwa kazini. Mwaka 2013 tuzo hiyo ilichukuliwa na Mwanahabari Absolum Kibanda.
Makamu wa Rais wa UTPC, Jane Mihanji
Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan, amebainisha kwamba tunzo ya Daudi Mwangosi mwaka huu pia haikupata mshindi kwa namna ambavyo jopo la tuzo hiyo lilivyoweka vigezo vyake ikiwemo Mwandishi anayepaswa kuichukua awe amepigwa, kuumizwa ama kuuawa akiwa kazini. Mwaka 2013 tuzo hiyo ilichukuliwa na Mwanahabari Absolum Kibanda.
Vingozi wa UTPC wakimkumbuka marehemu Daudi Mwangosi
Wanahabari mkoani Mwana wakimkumbuka marehemu Daudi Mwangosi
Bonyeza HAPA Kujua Zaidi

SERIKALI YAAHIDI MAZINGIRA SALAMA KWA WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU

$
0
0
Afisa Tawala Wilaya ya Nyamagana, Kombe Danty (wa pili kushoto), akizungumza kwenye ungaji wa Mafunzo/Semina ya Utetezi wa Haki za Binadamu katika Sekta ya Madini nchini hii leo jijni Mwanza.

Na George Binagi-GB Pazzo

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Mary Tesha, amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Watetezi wa Haki za Binadamu nchini ikiwemo kuweka mazingira salama katika utendaji wao wa kazi.

Tesha ameyasema hayo hii leo Jijini Mwanza, katika hotuba yake iliyosomwa na Afisa Tawala Wilaya ya Nyamagana, Kombe Danty, kwenye ungaji wa Mafunzo/Semina ya Utetezi wa Haki za Binadamu katika Sekta ya Madini nchini.

Naye Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Onesmo Olengurumwa, amesema mtandao huo umekuwa ukitoa semna kwa watetezi mbalimbali wa haki za binadamu ili kuwajengea uwezo wa kufanya kazi bila migogoro yoyote na serikali.
Kutoka ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Heri Nkoromo, Afisa Tawala Wilaya ya Nyamagana, Kombe Danty, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Onesmo Olengurumwa na Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu mikoa ya Mara, Mwanza na Simiyu, Antony Mayunga.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Heri Nkoromo, akizungumza kwa niaba ya mbunge huyo, ambapo amewasihi washiriki wa mafunzo hayo kufikisha elimu waliyoipata kwa watetezi wengine ambao hawakubahatika kuhudhuria semina hiyo.
Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini, Onesmo Olengurumwa (kulia), anasema wakati mwingine Watetezi wa Haki za Binadamu wamekuwa wakichukuliwa kama wachochezi kwenye jamii jambo ambalo si sahihi.
Washiriki wa Semina hiyo ya siku tatu, iliyoanza Agosti 31,2016 wamepatiwa vyeti vya ushiriki ambapo pichani ni Jimmy Luhende kutoka taasisi ya Utawala Bora nchini, akipokea cheti cha ushiriki.
Angel Benedict kutoka Shirika la Kutetea Wafanyakazi wa Majumbani, Wote Sawa, la Jijini Mwanza, akipokea cheti cha Ushiriki.
Mwanahabari na Mwendeshaji wa Mtandao wa Mabadiliko Forums, akipokea Cheti cha Ushiriki.
Mshiriki akipokea cheti cha Ushiriki
Mshiriki akipokea cheti cha Ushiriki
Mshiriki akipokea cheti cha Ushiriki
Mshiriki akipokea cheti cha Ushiriki
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini (THRD) unajumuisha Watetezi/Watu wanaotetea haki mbalimbali katika jamii ikiwemo kwa makundi ya Wakulima, Wafugaji, Waandishi wa Habari, Wanasheria, Katiba, Utawala Bora, Watoto, Wanawake miongoni mwa makundi mengi katika jamii.
Bonyeza HAPA Kujua Zaidi

KIWANDA CHA SARUJI CHAIPIGA TAFU SHULE YA SEKONDARI YA ILBORU YA ARUSHA

$
0
0

Tangakumekuchablog

Tanga, KIWANDA Cha Saruji Cha Simba (Simba Cement) cha Tanga, kimeipa shule ya Sekondari ya Ilboru Secondary School ya Arusha mifuko 400 ya saruji yenye thamani zaidi ya milioni 4.8 kwa ujenzi wa vymba vya madarasa.

Akizungumza wakati wa halfa fupi ya makabidhiano leo, Mkuu wa Idara ya Rasilimaliwatu kiwanda cha Saruji cha Simba Cement, Diana Malambugi, alisema msaada huo umetolewa ili kupunguza changamoto za vyumba vya madarasa kwa shule hiyo.

Alisema msaada huo utapunguza uhaba wa vyumba vya madarasa na kutoa wito kutumika kama ilivyokusudiwa na kuiagiza kamati ya shule kuhakikisha mifuko hiyo inatumika ipasavyo.

‘Mifuko hii ya saruji itapunguza changamoto inayoikabili shule yako ikiwemo vyumba vya madarasa na ujenzi wa nyumba za walimu, sera yetu moja wapo ni hii ya elimu” alisema Malambugi

Alimtaka mwalimu huyo na kamati yake ya shule kuitunza mifuko hiyo ya saruji na kumhakikishia kuisaidia pale ambapo kutakuwa na uhitaji na kuwataka wadau wengine wa elimu kusaidia sekta ya elimu zikiwemo kuondosha changamoto za uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa.

Kwa upande wake, mwalimu mkuu wa shule ya Ilboru sekondari school , Julias Shulla, alikishukuru kiwanda hicho na kusema kuwa msaada huo utatumika kama ilivyoombwa.

Alisema shule yake inakabiliana na changamoto nyingi zikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja uhaba wa vifaa vya maabara hivyo kuwataka wadau wa elimu kuisaidia.

‘Tunakishukuru kiwanda cha saruji cha simba kwa moyo wao waliounyesha kwetu, kwa fadhila hii tunawaahidi kuwa tutaitumia saruji kama tulivyoiomba” alisema Shulla

Alisema mifuko hiyo itapunguza kwa kiasi kikubwa changamoto ambazo shule yake inakabiliana nazo na kusema kuwa msaada huo ni faraja kwao na wanafunzi wa shule yake.



Mkuu wa Idara ya Rasilimawatu kiwanda cha Sauji cha Simba Cement cha Tanga, Diana Malambugi, akimkabidhi mifuko ya saruji 400 yenye thamani zaidi ya milioni 4.8 kwa mwalimu mkuu shule ya Sekondari ya Ilboru ya Arusha, Julias Shulla ikiwa ni ujenzi wa vyumba vya madarasa.nyuma kulia ni Mkuu wa fedha Pieter Jaggar na kushoto ni Emmanuel Jonas mhasibu.







  Mhasibu wa kiwanda cha Saruji cha Simba Cement, Emmanuel Jonas, akimkabidhi mwalimu mkuu wa shule ya Sekondari ya Iboru ya Arusha, Julias Shulla mifuko ya saruji 400 yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 4.8 kwa ajili ya ujenzi wa vymba vya madarasa, nyuma ni mkuu wa fedha, Pieter Jaggar.









 Afisa Uhusiano kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga, Mtanga Nnour, akimkabidhi mifuko ya saruji 400 yenye thamani zaidi ya shlingi milioni 4.8 kwa mwalimu  mkuu wa shule ya sekondari ya Ilboru ya Arusha, Julias Shulla, ikiwa ni kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa. Nyuma ni mkuu wa fedha, Pietre Jaggar.





 Mkuu wa fedha kiwanda cha saruji cha Simba Cement, Pieter Jaggar, akimabidhi mifuko ya saruji 400 yenye thamani zaidi ya shilingi milioni 4.8 mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya Ilboru ya Arusha, Julias Shulla ikiwa ni kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa, kulia ni meneja usambazaji na ugawaji, Samwel Shoo, nyuma kulia ni Afisa Uhusiano , Nour Mtanga  na mkuu wa Idara ya Rasilimawatu, Diana Malambugi.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Kumekucha. 0655902929

BENKI YA DIAMOND TRUST YASAIDIA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

$
0
0
Meneja wa kitengo cha Masoko wa Benki ya Diamond Trust (DTB), Sylvester Bahati (kulia), akikabidhi magodoro 50 kwa Mkuu wa kituo cha watoto wenye mahitaji aalumu kilichopo Chamazi, Bi. Winfrida Rubanza.  Pichani chini ni Bi. Winfrida Rubanza akihojiwa na mwandishi wa habari. Tukio hili liliratibiwa na Benki ya Diamond Trust ikishirikiana na Bi Lorna Dadi ambaye ni mwandishi wa kitabu cha Vipande Vya Maisha.





RAIS DKT MAGUFULIA ALAKIWA KWA SHANGWE MJINI ZANZIBAR AKITOKEA KISIWANI PEMBA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba ambako aliweka shada la maua kwenye kaburi la Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hayati Dkt Omar Ali Juma, na kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Gombani ya Kale.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitelemka kutoka kwenye ndege ya ATCL katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akivishwa shada la maua ya asumini baada ya kutelemka kutoka kwenye ndege ya ATCL katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na makamanda wa vikosi vya ulinzi na usalama katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zuberi Ali Maulid katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri  wa Ujenzi, Mawasilaino na usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Abeid Karume katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Yussuf Masauni   katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Mwakilishi wa jimbo la Uzini Mhe. Mohamed Raza Hassanali  katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na  Waziri wa Afya Mhe.  Mahmoud Thabit Kombokatika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mohamed Seif Khatib katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Mratabu wa Diaspora,Ofisi ya Rais Ikulu na Ushirikiano wa Kimataifa Zanzibar Ndugu Hassan Hafidh katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na mmoja wa makada waandamizi wa CCM katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na viongozi mbalimbali  katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa  katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono na mmoja wa viongozi  katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiakisalimiana na mmoja wa viongozi katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na mmoja wa wazee mashiuhuri katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said  katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifurahia ngoma ya utamaduni ya Kilua katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiangalia ngoma ya Msewe baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume mjini Zanzibar leo jioni akitokea kisiwani Pemba. Picha na IKULU

JESHI LA POLISI MWANZA LASHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA YA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Taasisi mbalimbali zikiwemo za Serikali na binafsi kutoka ndani na nje ya nchi zimeshiriki Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki, yanayofanyika viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza. Maonesho hayo huandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo nchini, TCCIA.

Taasisi mbalimbali za Wajasiriamali, Wafanyabiashara na Viwanda hutumia Maonesho hayo kukutana na wateja wapya, kutangaza na hata kuuza bidhaa zake. Mbali na hilo taasisi mbalimbali hutumia fursa hiyo kukutana na wananchi na kufikisha elimu husika.

Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa kujumuisha vitengo vyake ikiwemo Kikosi cha Usalama barabarani na dawati la jinsia, limetumia maonesho hayo kufikisha elimu mbalimbali kwa wananchi na hata kupokea maoni kutoka kwa wananchi.

Na BMG
Banda la Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, Kitengo cha dawati la jinsia
Banda la Jeshi la polisi mkoani Mwanza, kitengo cha Usalama barabarani
Maonesho hayo yalianza Agosti 26,2016 na ufungi rasmi kufanyika Agosti 30,2016 ambapo Mkuu wa Wilaya ya Ilemela alifungua Maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kama picha inavyoonekana mgeni rasmi akiwa kwenye banda la jeshi la polisi mkoani Mwanza.
Endelea kutazama picha, Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, akikagua mabanda ya washiriki mbalimbali
Soma zaidi HAPA

SIMIYU YAJIPANGA KUANZA KUTENGENEZA CHAKI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akionesha aina tofauti za maboksi yatakayotumika kufungashia chaki nyeupe na za rangi ambazo zinatarajiwa kuanza kuzalishwa na Vijana wa Wilaya ya Maswa, Mkoani humo wakati alipohitimisha Mafunzo ya Teknolojia ya Utengenezaji wa Chaki kwa vijana hao, (katikati) Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Seif Shekalaghe (kulia) Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Maswa, Mhe. Peter Bunyongoli.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Seif Shekalaghe akizungumza na vijana na wadau wengine wakati wa kuhitimisha mafunzo Teknolojia ya utengenezaji chaki yaliyotolewa na Shirika la Viwanda Vidogo vidogo SIDO kwa Vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Maswa, katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Meneja wa Shirika la Viwanda Vidogo vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga, Athanas Moshi (aliyesimama) akizungumza na vijana na wadau wengine wakati wa kuhitimisha mafunzo ya Teknolojia ya utengenezaji chaki yaliyotolewa na Shirika hilo kwa Vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Maswa.

Baadhi ya Vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Maswa wakiangalia sampuli za maboksi yaliyopendekezwa kutumika kufungashia chaki pindi uzalishaji utakapoanza wakati Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) akihitimisha mafunzo ya Teknolojia ya utengenezaji chaki yaliyotolewa na SIDO kwa vijana hao, wilayani humo





Vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Maswa wakiweka chaki walizotengeneza wakati wa mafunzo ya Teknolojia ya utengenezaji chaki yaliyotolewa na SIDO katika maboksi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (hayupo pichani) kabla ya Mkuu huyo wa mkoa kuhitimisha mafunzo hayo.



Na Stella Kalinga, Simiyu


Serikali Mkoani Simiyu imetangaza azma yake ya kuanza kutengeneza Chaki ambazo zitauzwa katika Wilaya za Mkoa huo na nchi nzima kabla ya Oktoba 14 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony John Mtaka wakati alipohitimisha mafunzo ya Teknolojia ya utengenezaji wa Chaki kwa vikundi vya vijana Wajasiriamali wilayani Maswa, yaliyotolewa na Shirika la Viwanda Vidogo vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga.

Mtaka amesema shule zote za Msingi na Sekondari za Serikali Mkoani humo zinatumia jumla ya katoni 1200 za chaki ambazo zinagharimu shilingi 25,000,000 kwa kila mwezi, hivyo kama Vijana wa Wilaya ya Maswa wakizalisha Chaki na kusambaza katika mkoa mzima watajipatia kipato na kuondokana na umaskini.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema katika kutekeleza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwa na Tanzania ya Viwanda, Mkoa huo umejipanga kuimarisha uwekezaji katika viwanda vidogo vidogo ambavyo vitazalisha mahitaji ya kila siku ya wananchi, hivyo wamedhamiria kuwa na uzalishaji wa bidhaa moja kwa kila wilaya ( one district one product), ambapo Wilaya ya Maswa itakuwa ikizalisha chaki.

“ Wilaya ya Maswa imepokea shilingi 38,000,000 Meatu 31,000,000 kwa ajili ya vijana kutoka Wizara yenye dhamana na Vijana, sasa hivi tumepeleka maombi ya wilaya zilizobaki. Tumedhamiria kuutambulisha Mkoa kwa kuzalisha bidhaa zetu wenyewe, tumeanza na Chaki wilaya ya Maswa, Wilaya ya Meatu wao watazalisha maziwa, tutaendelea kutengeza utambulisho(brand) wa wilaya nyingine kwa kuzalisha bidhaa zinazoendana na malighafi zilizopo” alisema Mtaka.

Akizungumza katika hitimisho la Mafunzo hayo kwa Vijana, Meneja wa Shirika la Viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga, Athanas Moshi ametoa wito kwa vikundi vya vijana kuwa na mipango itakayowasaidia kutangaza bidhaa zao na kupata soko la bidhaa hizo ndani na nje ya Mkoa ili kujiongezea kipato.

“Mtakapoanza kuzalisha chaki, kulingana na tathmini iliyofanyika kama mtauza kwa Mkoa wa Simiyu tu mtakuwa na uwezo wa kutengeneza faida ya shilingi 8,000,000 kila mwezi, hiyo si fedha ndogo mkiwa na mipango thabiti mkazalisha chaki bora mtaweza kuuza chaki zenu nchi nzima na hata nje ya nchi” alisema Moshi.

Naye mmoja wa vijana waliopata mafunzo ya utengenezaji wa chaki, Kelvin Steven ametoa wito kwa Wananchi wa Simiyu na Watanzania kwa ujumla, kuunga mkono juhudi za Vijana Wajasiriamali na kuthamini bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ili kuinua uchumi wa Vijana hao na Taifa kwa jumla.

KIKOSI KAZI CHA TANESCO CHAANZA KUBADILISHA MIUNDOMBINU YA UMEME JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Meneja Mwandamizi wa Usambazaji Umeme wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), ambaye pia ndiye Meneja wa Mradi wa kuimarisha miundombinu ya Umeme, Injinia Theodory Bayona.(katikati), akisimamia kazi hiyo leo Septemba 3, 2016


Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Leila Muhaji, akizungumza na waandishi wa habari kwenye eneo la mradi


NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID

WAHANDISI, na mafundi wa Shirika la Umeme Nchini Tanzania, (TANESCO), kwa kushirikia na wale wa kampuni za Kijapani za Yachiyo Engineering Co Limited, Takaoka na National Construction Co. Limited, wameanza kazi ya uboreshaji miundombinu ya umeme kwenye kituo kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam, imeanza leo Septemba 3, 2016.

Kazi kubwa inayofanyika hivi sasa ni kubadilisha laini kutoka umeme mdogo kwenda umeme mkubwa, lakini pia kubadilisha vifaa vingine muhimu ili kuwezesha usafirishaji umeme uweze kuwafikia watumiaji katika ubora ulio juu.

“Ikumbukwe kwamba, hapa tulikuwa na laini mbili (waya mbili) zilizokuwa na uwezo wa kusafirisha umeme kiasi cha Megawati 120 kila moja, kutoka hapa Ubungo kwenda kituo cha Ilala, lakini kazi inayofanyika sasa, ni kubadili njia hizo (waya za umeme), ambazo zitakuwa na uwezo wa kupitisha kiasi cha umeme wenye Megawati 220 kila moja,” Alifafanua Meneja Muandamizi wa Usambazaji Umeme wa Shirika hilo, ambaye pia ndiye Meneja wa wa Mradi wa kuimarisha miundombinu ya Umeme, Injinia Theodory Bayona.

Kwa mantiki hiyo, kazi inayofanyika leo hii itawezesha umeme utakaokuwa ukisafirishwa kutoka hapa Ubungo kwenda Ilala, kuwa na jumla ya Megawati 440 kwa laini zote mbili, tofauti na hapo awali ambapo uwezo wa kusafirisha umeme ulikuwa Megawati 240 tu,” Alisema.

Kazi ikikamilika wakazi wa jiji la Dar es Salaam, watakuwa wakipata umeme wa uhakika, na ulio bora, alifafanua Injinia Bayona

Naye Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Nchini Tanzania, (TANESCO), Leila Muhaji, amewaomba wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambapo Shirika linafanya juhudi kubwa za kuwapatia umeme wa uhakika wananchi kwa kuimarisha miundombinu yake,.

“Ili kuwawezesha mafundi wetu kufanya kazi katika mazingira salama, tutakuwa tukikata umeme kuanzia leo hii Septemba 3 na umeme utakuwa ukikatika kuanzia saa 2 asubuhi na kurejea saa 11 jioni kwa utaratibu na tarehe kama ifuatavyo; Septemba 3-4, Septemba 10-11, Septemba 17-18, na Septemba 24-25, 2016.” Alifafanua Leila, na kuwaomba wananc hi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki.

Mradi huu ulioanza Februari 2015 na unaotarajiwa kukamilika Juni 2017 unatekelezwa na Serikali kupitia TANESCO kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) .
Tsutomu Sato, wa kampuni ya Takaoka ya Japan, akiwa kazini
Mafundi wa TANESCO, wakitayarisha nyaya hizo mpya
Fundi wa TANESCO, akifunga kikombe wakati wa kazi ya kubadilisha miundombinu ya kusafirisha umeme kwenye kituo kikuu cha kupooza na kusambaza umeme cha Ubungo, jijini Dar es Salaam
Raphael Mjata, Msimamizi Mkuu wa Njia Kuu za Umeme, akionyesha uwezo wa kituo cha Ubungo cha kupooza umeme wenye kilovolti 132
Mafunzi wa TANESCO na kampuni ya National Construction Company Limited, wakivuta nyaya hizo mpya
Hizi ndio nyaya zitakazofungwa kwenye laini mbili za kusafirisha umeme kutoka kituo cha kupooza na kusafirisha umeme cha Ubungo

Mhandishi Bayona, akielezea waandishi wa habari mwenendo wa kazi hiyo
Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO makao makuu, Leila Muhaji, na Afia Uhusiano wa Shirika hilo, Henry Kilasila, wakiwa kazini

Mhandisi Bayona (kulia), akijadiliana jambo na Wahandisi wenzake, Yasutaka Osawa, (kushoto), ambaye ni mwakilishi katika mradi wa kuboresha umeme jiji la Dar es Salaam, kutoka kampuni ya Takaoka Engineering Co Ltd, na Mhandisi Ahmed Mmingwa, ambaye ni Msimamizi wa Mradi kutoka TANESCO
 Fundi wa TANESCO, akiwa kazini leo Septemba 3, 2016

Tamai Masayuki, Mwakilishi wa kampuni ya Kijapani ya Yachiyo Engineering Co. Limited, akizungumza na waandishi wa habari kuhsuu maendeleo ya uboreshaji huo
 Wahandisi wakijadiliana jambo
 Fundi wa TANESCO akiwa kazini
Kazi inaendelea





Meneja Mwandamizi wa Usambazaji Umeme wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), ambaye pia ndiye Meneja wa Mradi wa kuimarisha miundombinu ya Umeme, Injinia Theodory Bayona.(katikati), Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Leila Muhaji, (kulia) na Afisa Habari wa Shirika hilo makao makuu, Henry Kilasila, (wakwanza kushoto) na waandishi wa habari, wakitembelea eneo la mradi mapema leo asubuhi Septemba 3, 2016 ambapo kazi ilianza kwa kasi





Wafanyakazi wa TANESCO chumba cha ufuatiliaji mwenendo wa umeme (control room) wakiwa akzini


Chumba cha kufutialia mwenendo wa umeme jijini Dar es Salaam, (Control room), cha TANESCO-Ubungo sub station)

RAIS DKT MAGUFULI ALIPOHUTUBIA WANANCHI UWANJA WA DEMOKRASIA ZANZIBAR JUMAMOSI

$
0
0
Viongozi mbalimbali wakiwa wamejipanga kumsubiri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Mstahiki Meya wa Mji wa Zanzibar Mhe Khatib Abdurahaman Khatib alipowasili kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji Wananchi Uchumi na Ushiriuka.Mhe Haroun Ali Suleiman kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais wa Chama cha Siasa ADA-TADEA Mhe. Juma Ali Khatib kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa kabla kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Balozi Ali Karume
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akioungia umati kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Mafundi mitambo wa AZAM TV wakiongozwa na Mehboub Al Hadad wakiwa tayari kurusha live mkutano wa hadhara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Shekhe akitoa mawaidha kabla Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na viongozi wengine wakiwa katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimshukuru Shekhe wakati wa mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Shekhe akipongezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano) Mhe. January Makamba na waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi
Jukwaa kuu
Wasomautenzi walisisimua umati
Wasoma utenzi wakipongezwa jukwaa kuu
Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano
Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano
Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano
Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano
Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia mkutano
Jukwaa kuu
Risala 
Pongezi kwa msoma risala
Bendi ya vijana
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud akisoma muhtasari wa shughuli na kutambulisha wageni
Sehemu ya umati mkubwa uliojitokeza
Umati
Nyomi
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akitambulishwa
Mke wa Rais wa Zanzibara Mama Mwanamema Shein akitambulishwa
 Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Zuberi Ali Maulid akitambulishwa
Mawaziri wakitambulishwa
Viongozi wa vyama mbalimbali wakitambulishwa
Bw. Hafidh Ameir, mume wa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akitambulishwa
Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Abdulhamid Yahya Mzee akitambulishwa
Viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa wakitambulishwa
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahmoud akisoma muhtasari wa shughuli na kutambulisha wageni
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha akisalimia viongozi
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha akitambulishwa jukwaani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein wakiongea
Mama Fatma Karume akitambulishwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein wakiongea, Kushoto ni  Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mhe Vuai Ali Vuai 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akisalimia
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi akisalimia wananchi
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ, Mhe. Haji Omar Kheri akisalimia
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Mhe Vuai Ali Vuai akisalimia
Umati ukshangilia
Furaha
Makamu wa Rais wa Chama cha Siasa ADA-TADEA  Mhe. Juma Ali Khatib  akisalimia
Makamu wa Rais wa Chama cha Siasa ADA-TADEA  Mhe. Juma Ali Khatib  akipongezwa 

Mwananchi akifurahia hotuba
Umati ukifuatilia hotuba
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikaribishwa na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein kuhutubianmkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016
Jukwaa kuu wakifurahia jambo wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe akihutubia Magufuli mkutano wa hadhara katika uwanja wa Demokrasia mjini Unguja Jumamosi Agosti 3, 2016 
Jukwaa kuu likifurahia hotuba
Viongozi wakifurahia

RC SHIGELLA MGENI RASMI UZINDUZI WA BODI YA TANGA UWASA KESHO

$
0
0

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa) Mhandisi, Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa bodi mpya.kesho


Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira leo itazindua bodi mpya yake iliyoteuliwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge Julai Mosi mwaka huu baada ya ile ya awali kumaliza muda wake ambayo ilidumu kwa kipindi cha miaka mitatu.

Katika uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ambayo inatarajiwa kuanza asubuhi.

Akizungumza jana,Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi Joshua Mgeyekwa aliwaambia waandishi wa habari kuwa halfa hiyo pia itatumika kutambua na kupongeza juhudi zinazofanywa na bodi,menejimeni na wafanyakazi wa mamlaka hiyo.


Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)Mhandisi,Joshua Mgeyekwa kushoto aliyesimama na PRO wa Mamlaka hiyo

Alisema licha ya wafanyakazi hao lakini pia wateja wao kwa kuiwezesha mamlaka hiyo kuwa bora kwa utoaji wa huduma za maji safi miongoni mwa mamlaka 23 za maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo tokea mwaka 2012/2013.

Aidha alisema pia mamlaka hiyo imepata leseni ya daraja la kwanza baada ya kukithi vigezo vya mdhibiti wa huduma za nishati na maji hivyo kuwa mamlaka ya kwanza ya maji safi na usafi wa mazingira hapa nchini kufikia hatua hiyo ya juu katika ufanisi wa utendaji wa mamlaka.

“Waandishi wa habari kama mnavyojua mamlaka yetu ina cheti cha ithibati ya Ubora (ISO 9001) ambacho imekipata tangu mwaka 2007 tokea kipindi hicho mamlaka imekuwa ikifanya kazi zake kwa viwango vya kimataifa katika usimamizi wa mfumo wa kumhudumia mteja kwa kufuata vigezo vya ubora “Alisema.


Waandishi wa habari mkoani Tanga wakifuatilia hotuba ya mkurugenzi huyo


“Lakini pia cheti hiki huuishwa kila baada ya miaka mitatu kwa kukidhi vigezo vya utoaji wa huduma vinazohitajika ,uhuishaji ulifanyika miaka 2010 na 2013 kwa kupata ISO 9001:2008 na mwaka huu Tanga Uwasa imekuwa taasisi ya kwanza nchini chini ya kampuni ya Ithibati ya SGS Tanzania kupata cheti cha Ithibati cha 9001:20015.

Aidha aliongeza kuwa mafanikio makubwa sana ambayo hayo yametokana na juhudi za pamoja kati ya bodi ya wakurugenzi, menejimenti,wafanyakazi,wateja na wadau wa Tanga Uwasa.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KUSHIRIKI UANGALIZI WA UCHAGUZI WA SHELISHELI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustine Mahiga akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Shelisheli, Alix Michel.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania ilikabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa kuongoza Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC Organ), katika Mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika huko Mbabane, Swaziland tarehe 29 – 31 Agosti, 2016. 

Mara baada ya kukamilika kwa Mkutano huo, Mheshimiwa Dkt. Augustine P. Mahiga (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alielekea Jamhuri ya Shelisheli kwa lengo la kumwakilisha Mheshimiwa Dkt. John P. Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuongoza ujumbe wa Waangalizi wa SADC katika Uchaguzi wa Shelisheli utaofanyika tarehe 8 - 10 Septemba, 2016.


Wajibu huu wa Tanzania katika kuongoza misheni hiyo ya waangalizi wa uchaguzi imetokana na misingi na muongozo wa chaguzi za kidemokrasia katika Kanda ya SADC. Akiwa nchini Shelisheli, Mheshiwa Mahiga (Mb), alizindua rasmi misheni hiyo tarehe 2 Septemba, 2016 kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Magufuli. Misheni hiyo ya waangalizi itakua na waangalizi kutoka nchi za SADC .

Wakati akiwa nchIni Shelisheli, Mheshimiwa Waziri Mahiga alipata fursa ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mhe. James Alix Michel Rais wa Sheliseli .

Pia Mheshimia Waziri Mahiga aliweza kufanya mazungumzo na Mhe. Joel Morgan, Waziri wa Mambo ya Nje wa Seychels na kukutana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Seychels.

Imetolewa na :



BALOZI INNOCENT E. SHIYO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustine Mahiga akimtambulisha Balozi Innocent Shiyo kwa Rais wa Shelisheli, Alix Michel
Rais wa Shelisheli, Alix Michel akiwa kwenye kikao na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Baloz Dk. Augustine Mahiga nchini Shelisheli.

Waangalizi wa uchaguzi wa wabunge wa Shelisheli katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustine Mahiga na Balozi Innocent Shiyo. (Picha kwa hisani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki).



USIKU WA BWANA NA BIBI BALIYANGA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA

$
0
0

Jana Septemba 04, 2016 ilikuwa siku njema kwa waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, Bwana Robson Mkesha Baliyanga na Miss Penina Mkama, baada ya kufunga ndoa takatifu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji Kiongozi Dkt.Daniel Moses Kulola.

Baada ya ndoa, Hafla ilifanyika kwenye Ukumbi wa Maendeleo House Jijini Mwanza, kama picha inavyoonesha maharusi wakiingia Ukumbini.

Na BMG
Maharusi, Bwana Robson Mkesha Baliyanga (kushoto) na Miss Penina Mkama (kulia) wakiingia ukumbini
Mc Joel Maduka, akitoa mwongozo kabla maharusi kuingia ukumbini
Mwenyekiti wa kamati ya harusi (kushoto) akiwakaribisha maharusi
Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Kulola, akifungua sherehe kwa maombi
Maharusi wakikata utepete kuingia ukumbini
Maharusi wakilishana keki, ishara ya upendo
Mwanamke heshima
Wasimamizi/Wapambe wa maharusi nao wakilishana keki
Maharusi na wapambe wao
Maharusi wakinyweshana shampeni
Ndugu, jamaa na marafiki wakiwapongeza maharusi
Ndugu, jamaa na marafiki wakiwapongeza maharusi
Mwenyekiti wa kamati ya harusi akitoa neno kwa maharusi
Kamati ya harusi
Kamati ya harusi
Wageni waalikwa
Waalikwa
Taswira ukumbini
Bonyeza HAPA Kwa Picha za Kanisani

USIKU WA BWANA NA BIBI BALIYANGA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA

$
0
0

Jana Septemba 04, 2016 ilikuwa siku njema kwa waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, Bwana Robson Mkesha Baliyanga na Miss Penina Mkama, baada ya kufunga ndoa takatifu katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza, chini ya Mchungaji Kiongozi Dkt.Daniel Moses Kulola.

Baada ya ndoa, Hafla ilifanyika kwenye Ukumbi wa Maendeleo House Jijini Mwanza, kama picha inavyoonesha maharusi wakiingia Ukumbini.

Na BMG
Maharusi, Bwana Robson Mkesha Baliyanga (kushoto) na Miss Penina Mkama (kulia) wakiingia ukumbini
Mc Joel Maduka, akitoa mwongozo kabla maharusi kuingia ukumbini
Mwenyekiti wa kamati ya harusi (kushoto) akiwakaribisha maharusi
Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Kulola, akifungua sherehe kwa maombi
Maharusi wakikata utepete kuingia ukumbini
Maharusi wakilishana keki, ishara ya upendo
Mwanamke heshima
Wasimamizi/Wapambe wa maharusi nao wakilishana keki
Maharusi na wapambe wao
Maharusi wakinyweshana shampeni
Ndugu, jamaa na marafiki wakiwapongeza maharusi
Ndugu, jamaa na marafiki wakiwapongeza maharusi
Mwenyekiti wa kamati ya harusi akitoa neno kwa maharusi
Kamati ya harusi
Kamati ya harusi
Wageni waalikwa
Waalikwa
Taswira ukumbini
Bonyeza HAPA Kwa Picha za Kanisani

WASHIRIKI 29 MAISHA PLUS EAST AFRIKA 2016 WAINGIA KIJIJINI KUANZA SAFARI YA KUISAKA MIL.30

$
0
0
Ally Masoud maarufu kwa jina la Kipanya akiwa katika kijiji na Babu mwenyeji wa kijiji cha Maisha Plus wakijadili jambo wakati wakiwangoja washiriki wa shindano hilo hapo jana ambapo pia ilikuwa ikirushwa live na kituo cha Luninga cha AZAM TWO chaneli 102
Babu mwenyeji wa kijiji cha Maisha Plus akiwa anaandaa mazingira ya kijijini hapo
Haya ni Baadhi ya maeneo katika kijiji cha Maisha Plus ambapo washiriki hao kutoka Nchi Tano za Afrika Mashariki watakaa kwa wiki 8
Washiriki wa shindano la Maisha Plus Msimu wa tano wakiwa wanaingia kijijini huku kila mmoja akiwa amefungwa kitambaa usoni wasijue wapo wapi.
Mwenyeji wa Kijiji Babu wa Maisha Plus akiwa anawakaribisha washiriki kwa namna yake
Hapa Washiriki wakiendelea kuingia katika kijiji cha Maisha Plus huku wasifahamu wapo wapi.
Masoud Kipanya akiwapa maelekezo washiriki wa Shindano la Maisha Plus kabla hawajafugua rasmi vitambaa na kujua wapo wapi
Hivi ni Baadhi ya Vifaa na vitu ambavyo vijana wa Maisha Plus watakuwa wakivitumia kipindi wapo kijijini kwa Muda wa Wiki8
Masoud Kipanya akitoa msisitizo wa Jambo kwa washiriki wa shindano la Maisha Plus Msimu wa tano
Washiriki wa wa Shindano la Maisha Plus Msimu wa tano wakiwa wanafungua vitambaa kuona rasmi kijiji ambacho wataishi kwa wiki 8
Hapa ilikuwa ni kasheshe baada ya kufungua vitambaa na kukuta wapo porini sehemu wasiyo ijua huku kukiwa hakuna jengo lolote.
Hapa washiriki wa shindano la Maisha Plus wakiwa wanajipanga kuanza kufanya mchakato wa kuanza kujenga nyumba zao
Bado shughuli ilikuwa ni Pevu sana hawaelewi kabisa wanaanzia wapi wanaishia kujishauri kwanza huku kila mmoja akiwaza Milioni 30 atazipata vipi?
Hapa bado shughuli ndio kwanza ilikuwa inaanza washiriki hawa pia walikuwa wakibadilishana mawazo wafanyaje.
Babu wa Kijiji cha Maisha Plus akiwa anatoa maelezo ya kina kwa washiriki wa shindano hilo ambao wanatoka katika Nchi 5 Afrika Mashariki jinsi gani wataishi, watakavyojenga nyumba zao na watakavyo ishi katika kijiji cha Maisha Plus
Wakiwa wanaleta mizigo yao ndani ya Kijiji cha Maisha Plus
Mmoja wa washiriki wa Shindano la Maisha Plus akinoa panga kwa ajili ya kujiandaa kwenda kukata miti kwa ajili ya kujenga nyumba zao za kuishi ambapo kila nyumba moja watakuwa wanaishi washiriki watatu.
Baadhi ya Mizigo ya washiriki baada ya kuwasili katika kijiji cha Maisha Plus
Washiriki wa Shindano la Maisha Plus wakiwa wameanza kuandaa makazi yao
Kazi Ikiendelea ya Kuandaa sehemu ya Kuishi
Hapa kazi tuu yani kila mtu yupo na yake alimradi tuu wapate kujenga nyumba za kuishi katika kijiji hicho cha Maisha Plus.
Kulikuwa hakuna namna lazima kila mmoja afanye kazi ili wapate sehemu ya kulala
Wakati wenzake wamekwenda tafuta Miti ya Kujengea nyumba yeye alikuwa anatengeneza mpini
Babu wa Kijiji cha Maisha Plus akiwa anatoa maelekezo na kutoa vipimo vya jinsi watakavyokujenga nyumba zao
Kila mshiriki akiwa ameshika nyenzo yake kwa ajili ya kujenga nyumba zao zakuishi
Kazi zinaendelea hapa na sasa ilikuwa ni mwendo wa kukata miti ili kuwahi kumaliza kujenga nyumba na kuanza kuishi.
Babu wa Maisha Plus akiwa anafatilia jambo kijijini hapo.
Bila kuchakalika na kazi ya kujiandaa kutafuta miti na kujenga nyumba unaweza kujikuta unalala nje
Baadhi yao walikuwa wamesha anza kuweka nguzo za nyumba zao
Akionekana akikomaa kuchimba kitu kabla hajawekea mpini
Ukiwa katika kijiji cha Maisha Plus lazima upate na ubunifu sana .. hawa jamaa washiriki wa Shindano la Maisha plus msimu wa 5 2016 wakiwa wanakata miti kwa ajili ya kujenga nyumba ambapo wataishi kwa wiki 8
Pori kwa pori
Kazi kwa kwenda mbele

MAISHA PLUS EAST AFRICA 2016 itakuwa ikionyeshwa na AZAM Two Chaneli 102 
#HapaKaziTuu
#VijanaNdioNgazi

WIZARA YA AFYA YASISITIZA JUU YA MATUMIZI SAHIHI NA ENDELEVU YA KONDOM MPYA YA ZANA

$
0
0
Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro (katikati), akizungumza kwenye semina elekezi kuhusu uzinduzi wa Kondom mpya ya Zana itakayokuwa ikitolewa bure na serikali kwa wananchi, iliyofanyika Jijini Mwanza leo.


Na BMG

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imewahimiza wananchi kuzingatia matumizi sahihi na endelevu ya kondomu ili kujiepusha na mimba zisizotarajiwa pamoja na magongwa ya kuambukiza ikiwemo virusi vya Ukimwi.

Kaimu Mkuu wa kitengo cha habari, elimu na mawasiliano kutoka Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, Eddah Katikiro, ametoa rai hiyo hii leo Jijini Mwanza, kwenye semina elekezi kuhusu uzinduzi wa Kondom mpya ya Zana itakayokuwa ikitolewa bure na serikali kwa wananchi.

Katikiro amesisitiza matumizi sahihi na endelevu ya kondom ya Zana kwa wananchi walio kwenye mahusiano ya kimapenzi, yatasaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama virusi vya Ukimwi pamoja na mimba zisizotarajiwa na kwamba aina hiyo ya kondom ni imara na yenye ubora.

Mratibu wa mpango wa Taifa wa kudhibiti Ukimwi, mkoani Mwanza, Geofrey Mabu, amesema mkoa wa Mwanza umejipanga vyema ili kuhakikisha kondom za Zana zinawafikiwa walengwa hususani kupatikana bure katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye vituo vyote vya afya, maeneo ya starehe pamoja na kwenye ofisi za serikali na binafsi.

Uzinduzi wa Zana Kondom kitaifa ulifanyika mkoani Mbeya wiki iliyopita ambapo kwa mkoa wa Mwanza uzinduzi utafanyika kesho Jijini Mwanza ambapo aina hiyo ya kondomu itakuwa mbadala wa kondom za MSD zilizokuwa zikitolewa pia bure na Serikali lengo likiwa ni kuhakikisha mapambano dhidi ya Ukimwi yanafanikiwa.
Washirki wa semina hiyo
Wanasemina
Wanasemina
Mmoja wa washiriki wa semina akihojiwa na wanahabari
Mmoja wa washiriki wa semina akihojiwa na wanahabari
Picha ya pamoja
Bonyeza HAPA Kujua Zaidi
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live