Quantcast
Channel: Matukio
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live

KOFFI OLOMIDE AKIWA NA ALIYEMPIGA, AELEZA KILICHOTOKEA KWA WANAHABARI

$
0
0
KOFFI AKIWA NA MNENGUAJI WAKE ALIYEMPIGA TEKE BAADA YA KUWASILI JOMO KENYATA INTERNATIONA AIRPORT


MWENYEKITI CCM MARA ATUHUMIWA KWA USALITI

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MWANZA

BAADHI ya wenyeviti wa Kata,Matawi pamoja na mabalozi wa nyumba kumi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya za Mkoa wa Mara wamemtuhumu Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo Christopher Sanya kuwa alikihujumu kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana na kusababisha kipoteze majimbo manne kati ya tisa na kumtaka ajiuluzu kabla ya kutimuliwa.

Pia walidai kuwa anaongoza kwa majungu akiongozwa na mmoja wa wabunge wa majimbo ya mkoa wa Mara huku wakimtuhumu kujihusisha na kundi linalopinga Rais John Magufuli asikabidhiwe Uenyekiti wa CCM Taifa na amekuwa akiwashawishi wajumbe wasimpigie kura.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jijini Mwanza jana kwa sharti la hifadhi ya majina wenyeviti hao kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana alikisaliti chama pamoja na kuwachonganisha wanachama na kusababisha majimbo manne kunyakuliwa na wagombea wa UKAWA.

Walieleza kuwa Sanya kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana alitafuna posho za mabalozi wa CCM akishirikiana na Katibu msaidizi wa CCM wakashindwa kufanya kampeni kisha katibu huyo akahamishiwa wilayani Rorya.

Kutokana na tuhuma hizo wanachama wa Wilaya za Rorya,Serengeti, Tarime na Bunda wamemwomba mwenyekiti mpya wa CCM Taifa atakapobidhiwa rungu atumbue jipu hilo linalokwamisha maendeleo ya chama na wananchi.

“ Tunafahamu mwenyekiti wetu wa CCM mkoa wa Mara ni jipu na msaliti mkubwa kwenye kampeni alishiriki kuwaangusha wagombea wetu Bunda (Wassira) na Serengeti (Kebwe) kwa kuwasaidia wapinzani.Matokeo baada ya kutangazwa alifanya sherehe” alisema mmoja wa wenyeviti hao wa matawi na kata kwa sharti la hifadhi ya jina.

Wenyeviti hao walionya kuwa endapo mwenyekiti mpya akipuuuza kumfukuza kwenye chama kwa usaliti pamoja na washirika wake basi CCM Mara itaparaganyika kama si kufutika na majimbo yaliyopotea hayatarudi na hata waliyoshinda watayapoteza.

Naye Sanya akizungumza kwa simu na gazeti hili kuhusiana na tuhuma hizo alikana na kumtuhumu Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Rorya Samwel Kiboye “ Namba 3” kuwa ndiye anatengeza habari hizo kwani hakuna mwenyekiti anayeweza kumtuhumu.

“ Usipoteze muda kwa mambo kama hayo,kama ni malalamiko tuna vikao vya kuyasikiliza na kutoa uamuzi,uchaguzi ulishaisha na wananchi walifanya uamuzi.Tuhuma za usaliti sina sera hiyo ya kuhujumu chama na ukweli utabaki pale pale.Mi ni Mwenyekiti, acha mambo hayo usipoteze muda,

“ Wananchi na wanachama si wajinga.Tatizo la kupoteza majimbo linafahamika maana baada ya uchaguzi tulikaa na kubaini nani alifanya nini,hivyo hakuna logic.Lakini kuna wakati tuliwaudhi wananchi na jimbo moja hilo la Bunda haliwezi kuwa na madhara kiasi hicho,” alisema Sanya.

Mwenyekiti huyo alidai kuwa yote hayo yanatengezwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya moja kwa sababu anataka kugombea na hivyo anatafuta nafasi ya kumchafua na kuelea kuwa binafsi anaishi vizuri na wenyeviti wake wa wilaya na watashangaa kusikia mambo hayo.

“Uchaguzi wa kiti ujao ndio umeanza hivyo,wana CCM sio wajinga, niko imara na chama changu na fitna ni sehemu ya siasa.Namba 3 ndiye anatengeneza story ili apate kunichafua sababu anataka kugombea uenyekiti na mimi lazima nitulize hali hiyo maana uchaguzi bado, muda ukifika wanachama wataamua nani anafaa kuwaongoza,”alisema Saa
nya kwa simu.

KOFFI OLOMIDE AKAMATWA NA POLISI KWA KUMPIGA TEKE MNENGUAJI WAKE(VIDEO)

MAMBO YAMENOGA MKUTANO MKUU MAALUMU WA CCM MJINI DODOMA

$
0
0
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza, Stanslaus Mabula (kulia), akiwa pamoja na Diwani wa Kata ya Igoma Jijini Mwanza, wakiwa katika Viunga vya Ukumbi mpya wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Dodoma wa Dodoma Convetional Centre ambapo Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM unafanyika.

Ni Mkutano Maalumu kwa ajili ya Wajumbe hao kumchagua Mwenyekiti Mpya wa CCM Taifa, ambapo jana Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM walipitisha kwa kura zote jina la Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuwa Mwenyekiti wa chama hicho. Dkt.Magufuli anapokea kijiti cha uongozi wa chama kutoka kwa Rais Mstaaf wa awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.

Mji wa Dodoma umegubikwa na shamra shamra mitaa yote na tayari wajumbe wa Mkutano Mkuu wameanza kuingia Ukumbini kwa ajili ya Mkutano huo huku hali ya usalama ikiwa imeimarishwa vyema kila kona.
Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Stanslaus Mabula akisalimiana na mjumbe mwenzake wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM unaofanyika Mjini Dodoma hii leo
Mbunge wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza, Angelina Mabula (kushoto) akiwa na Katibu wake, Heri James, Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM unaofanyika Mjini Dodoma hii leo
Heri James (kushoto) akiwa na mmoja wa wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM, wakisalimiana ukumbini.
Mbunge wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza, Angelina Mabula (kushoto), akiwa ukumbini na mmoja wa wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM.
Kaimu Katibu wa CCM mkoani Mwanza Elias Mpanda (kulia) akisalimiana na aliekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, Manju Msambya (kushoto).
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kutoka mkoani Mwanza
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM akiwemo Le Mutuz (kulia) wakiperuzi taarifa mbalimbali kuhusiana na Mkutano huo.
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambae pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nhauye, akitoa burudani na Bendi ya TOT Pus
Ni burudani kutoka kwa bendi ya TOT Pus Ukumbini
Mbunge wa Jimbo la Mtama ambae pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nhauye, akitoa mwongozo wa kuanza kwa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM unaofanyika Mjini Dodoma.
Taswira Ukumbini

Wanafunzi watarajiwa chuo cha UDSM wafundwa juu ya maisha ya chuo

$
0
0
Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Amina Abdul ambaye pia ni Mratibu wa Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na wanahabari. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Amina Abdul ambaye pia ni Mratibu wa Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na wanahabari.Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki.Mmoja wa waratibu wa semina hiyo akitoa mwongozo kwa washiriki. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB. Mmoja wa waratibu wa semina hiyo akitoa mwongozo kwa washiriki. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB.Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani.IMG_0336 Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.  Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa wanafunzi baada ya kujibu swali kiufasaha. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa wanafunzi baada ya kujibu swali kiufasaha.Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani.Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kulia mbele) akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki.Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo wakiwa kwenye banda la mdhamini mkuu wa semina hiyo kujifunza shughuli mbalimbali wanazofanya. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo wakiwa kwenye banda la mdhamini mkuu wa semina hiyo kujifunza shughuli mbalimbali wanazofanya.Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo. Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo.Msanii nyota Nick Wa Pili akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Msanii nyota Nick Wa Pili akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo. Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo.

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

$
0
0
WAKATI wasanii wa kundi la ngoma za utamaduni la Utandawazi wanajipanga kutumbuiza, watu wengi waliokusanyika kwenye viwanja wa shule ya msingi Bukongo mjini Nansio walikuwa wanajiuliza mtoto Gozbert Bwele (8) aliyekuwa amekumbatia ngoma alikwenda kufanya nini pale.

Lakini mara tu ngoma zilipoanza kupigwa, uwanja mzima ukalipuka kwa furaha na haikushangaza wakati makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandez de la Vega, aliposhindwa kuvumilia na kutoka kwenda kucheza na mtoto huyo aliyeonyesha ufundi mkubwa katika upigaji wa ngoma.

Mama Maria Teresa, ambaye ni rais wa taasisi ya Mfuko wa kusaidia Wanawake Afrika, alijitoma uwanjani kucheza na kumtunza mtoto huyo anayesoma darasa la kwanza kwenye shule ya msingi Nansole katika halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza.





Makamu huyo wa rais mstaafu wa Hispania alizuru kisiwani Ukerewe akiwa ameongozana na ujumbe wake kwa lengo la kujionea kilimo cha viazi lishe na usindikaji wa mazao mbalimbali yatokanayo na viazi hivyo.

Kilimo hicho kinafanywa na akinamama 25 chini ya Mradi wa Green Voices unaofadhiliwa na taasisi ya Mfuko wa kusaidia Wanawake Afrika, ambao kwa hapa nchini umewawezesha wanawake wa Tanzania kubuni miradi endelevu inayoendana na utunzaji wa mazingira pamoja na kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

TAARIFA ZA KUPOTEA KWA MTOTO GERALD DAVID BWANAMGANGA

$
0
0
Mtoto  GERALD DAVID BWANAMGANGA anayetafutwa na wazazi wake.

Mtoto GERALD DAVID BWANAMGANGA ambaye anatafutwa na wazazi wake, ana umri wa miaka MIWILI NA NUSU. Amepotea jumapili tarehe 25/7/2016 mida ya saa 09 (tisa) mchana huku juhudi kubwa ya kumtafuta inayofanywa na wazazi, ndugu zake zikiwa bado hazijafanikiwa. Mara ya mwisho mtoto GERALD DAVID BWANAMGANGA alikuwa akicheza na wenzake KANISANI akiwa amevaa T-SHIRT NYEKUNDU na SURUALI YA KAKI maeneo ya BABANA, GONGO LA MBOTO jijini DAR ES SALAAM.

Tunaomba Watu, Mtu yeyote atakayeweza kumuona, basi anaweza kumfikisha Kituo Cha Polisi kilicho karibu nae. Au unaweza kuwasiliana na wazazi wa mtoto kwa namba 0713 040 615 ama 0712 185 226. Pia unaweza kupiga simu namba 0675 306 990.

 Mtoto  GERALD DAVID BWANAMGANGA anayetafutwa na wazazi wake.

Lakini Endapo mtu atamuona basi anaweza kutoa taarifa Polisi au hata Pia Kutoa taarifa kupitia makundi mbalimbali ya Whatsapp ambayo tunaamini pia taarifa itawafikia haraka wazazi au hata ndugu kama ambavyo taarifa ya kupotea kwake ilivyoweza kutufikia sisi na kuamua kutoa msaada wa kutangaza kupitia hapa.

Tunajua ni jinsi gani Maumivu wanayoyapata wazazi wake lakini Tunamuombea kwa Mungu amlinde huko aliko na Malaika wake wamrudishe mtoto wetu GERALD DAVID BWANAMGANGA Salama Salimini kwenye himaya ya wazazi wake.

Tunatoa pole kwa Wazazi kwa kupotelewa na Mtoto wao Kipenzi lakini tunapenda kuwaambia kuwa Wamwamini Mungu kwa maana Kila hatua wazikabidhizo kwake na kuamini basi Mungu atawatendea.

TUNAOMBA MSAADA KUSAMBAZA TAARIFA HIZI.

TANAPA YAIONGEZEA NGUVU TIMU YA TAIFA YA RIADHA INAYOJIANDAA NA MASHINDANO YA OLIMIPIKI

$
0
0
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akitoa neno la ukaribisho kwa wanahabari na wageni wengine katika hafla fupi ya kukabidhi hundi kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa, inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki yatakayoafanyika mwezi Agosti nchini Brazil.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi,akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Shilingi Milioni tano kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni tano kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wakijiandaa na mashindano ya Olimpiki.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi "Track Suit "maalumu zenye maandishi na nembo yanayotangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wanaojiandaa na mashindano ya Olimpiki
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akizungumza mara baada ya kukabidhiwa hundi pamoja na mavazi maalumu kwa ajili ya wanariadha hao .
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) waliohudhuria hafla hiyo.kutoka kushoto Mkurugenzi wa Utalii na Masoko,Ibtahim Musa,Meneja Utalii Johnson Manase na Mhifadhi Vitalis Uruka.
Wanariadha watakaoiwakilisha nchi katika mashindano ya Olimpiki katika jiji la Reo De Jeneiro nchini Brazil wakiwa katika mavazi maalumu yanaotangaza vivutio vilivyoko nchini.
Mkufunzi wa Wanariadha wanaojiandaa na mashindano ya Olyimpiki ,Francis John akizungumzia matarajio yake juu ya vijana hao.
Mmoja wa Wanariadha hao,Alphonce Felix Simbu akizungumza mara baada ya kupoke msaada kutoka  TANAPA.
Baadhi ya Wanahabari na wageni wengine waliofika katika ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kushuhudia makabidhiano hayo.
Mwanariadha Said Makuka atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Sara Ramadhan ,mwanadada pekee atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Alphonce Felix atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Fabian Joseph atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Wanariadha wanne watakao iwakilisha Tanzania katika Michuano ya Olyimpiki nchini Brazil wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Antony Mtaka ,wengine kutoka kulia ni Mkufunzi wa wanariadha hao,Francis John na anyefuatia ni Mkurugenzi wa Utalii na Masokowa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.



Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetangaza kutumia fursa ya mashindano ya Olyimpiki yanayotarajia kuanza mwezi ujao katika jiji la Rio de Janeiro nchini Brazili kutangaza vivutio vya utalii kupitia wanariadha wa Tanzania.

Hadi sasa ni wanariadha wanne ,wakiume watatu na wa kike mmoja ndio waliofuzu kushiriki mashindano hayo na tayari wako kambini katika hosteli za Chuo cha Misitu cha FITI zilizoko West Kilimanjaro wilayani Siha.

Akiongea mjini Arusha wakati akikabidhi msaada wa fedha na vifaa kwa ajili ya wanariadha hao Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA,Allan Kijazi amesema wameamua kutumia fursa hiyo pia kusaidia wanariadha hao wanaoiwakilisha nchi katika mashindano hayo ili waweze kurejea na medali.

Akishukuru kwa msaada huo Rais wa Shirikisho la Riadha nchini ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu AnthonY Mtaka amesema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuwakatia bima ya Afya mwaka mmoja wanariadha hao pamoja na familia zao ili wanapokua nchini Brazili wasiwe na mawazo mengi kuhusiana na familia zao walizoziacha hapa nchini.

Naye mmoja wa wanariadha waliofuzu kushiriki mashindano hayo Alphonce Felix pamoja na mkufunzi wa timu hiyo ya Riadha Francis John wameushukuru uongozi wa Riadha kwa kuiwezesha timu hiyo kukaa kambini kwa miezi saba na kuahidi safari hii timu hiyo haiendi kushiriki bali kupambania medali.

Wanariadha waliopo katika timu hiyo ya taifa wanaotarajiwa kwenda Brazili ni mwanamke pekee Sara Ramadhani, Fabiani Joseph, Saidi Makuka na Alfonce Felix .




MAALIM SEIF KUNGURUMA TENA MAREKANI

$
0
0
Na Mwandishi wetu, Philladelphia
Makamo wa Kwanza Mstaafu wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, anatazamiwa kunguruma tena chini Marekani wiki hii.
Maalim Seif Sharif Hamad  akiwasili katika uwanja wa ndege Philladelphia

Gwiji huyo wa siasa ambaye aliwasili jijini Philladelphia hapo jana, anatarajiwa kuwakhutubia Watanzania katika Mkutano wa hadhara utakaofanyika Jumamosi hii katika jiji la Boston. Katibu huyo Mkuu wa CUF pamoja na ujumbe anaofuatana nao aliwasili nchini humu akitokea Uingereza baada ya kukamilisha ziara yake ya Ulaya iliyochukua muda wa zaidi ya wiki moja.

Akiwa Ulaya Maalim Seif alitembelea Uiengerza na kufanya mikutano na Maofisa wa ngazi za juu wa Serikali ya Uingereza, Vyama vya kisisasa na Taasisi mbalimbali. Baadaye alielekea nchini Ubelgiji ambako alifanya ziara kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Ulaya na kufikisha madai ya Wazanzibari ya kurejeshewa haki yao ya Kidemokrasia.

Aidha alitembelea nchini Uholanzi ambako pamoja na mambo mengine, alikutana na maofisa wa Mahakama ya Ukhalifu ya Kimataifa na kufikisha kilio cha Wazanzibari dhidi ya Uvunjaji wa Haki za Binadamu unaendelea Visiwani Zanzibar.

Ziara hiyo ya Ulaya ilikuja katika kile maofisa wa CUF walichokielezea kuwa ni awamu ya pili ya ziara za nje za mwanasiasa huyo mkongwe katika juhudi za kutafuta uungwaji mkono wa Kimataifa kwa mgogoro wa Kisiasa Zanzibar.

Maalim Seif ambaye anafuatana na Mkuuwa Watumishi katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CUF Bwana Issa Kheir Hussein, yupo nchini Marekani kuitikia mwaliko wa kuhudhuria kwenye Mkutano Mkuu wa Chama Cha Democratic ulioanza jana jijini Philladelphia, mkutano ambao unatazamiwa kumpitisha Bi Hillary Clinton kuwa mgombea wa Urais wa Marekani kwa kuoitia tiketi ya Chama hicho.

Katika mkutano wake wa hadhara na Watanzania, Maalim Seif, aliyekuwa mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha CUF katika uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, anatazamiwa kuzungumzia zoezi zima la uchaguzi huo uliofutwa, na kusisitza madai ya Chama chake ya kurejeshewa haki yao waliyoporwa katika uchaguzi huo, na mwenendo mzima wa Demokrasia nchini Tanzania.

Itafaa kukumbusha kuwa hii ni mara ya pili kwa Maalim Seif kuzuru Marekani katika kipindi cha chini ya miezi miwili. Mwezi uliopita, Maalim Seif alikuwepo nchini humu na kufanya mazungumzo na viongozi wa Kisiasa na mashirika binafsi, na kutembelea Umoja wa Mataifa ambako alifikisha madai ya Chama chake ya ukandamizaji wa demokrasia nchini Tanzania. Aidha alizungumza na Watanzania waishio nchini Marekani katika jiji la Washington.

GGM YAFANIKISHA ZOEZI LA KUKUSANYA PESA KWA AJILI YA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Moshi Kipi Warioba akiongozana na kundi la wapanda mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining (GGM) waliopanda kwa lengo la kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazo shughulika na mapambano dhidi ya Ukimwi.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mining (GGM) ,Simon Shayo akizungumza wakati wa hafla fupi ya mapokezi ya kundi la wapanda mlima wakiwemo wafanyakazi wa mgodi huo waliopanda kwa leongo la kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazo shughulika na mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kiongozi wa kundi la wafanyakazi wa kampuuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining ,Kelvin Yasiwa akizungumza kwa niaba ya wenzake mara baada ya kuwasili wakitokea katika kilele cha Uhuru ,Mlima Kilimanjaro.
Balozi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Msanii Mrisho Mpoto akizungumza mara baada ya kurejea salama kutoka katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba akikabidhi cheti kwa mtoto Lucy Mashauri(15)baada ya kufanikiwa kufika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba akikabidhi cheti kwa mtoto Jacob Musa (16) baada ya kufanikiwa kufika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Balozi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Msanii Mrisho Mpoto akifurahia baada ya kukabidhiwa cheti kwa kufanikiwa kufika katika moja ya vilele vya Mlima Kilimanjaro,kilele cha Stela .
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya ya Moshi, Kipi Warioba akikabidhi vyeti kwa washiriki wengine wa changamoto hiyo ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba aliyekua mgeni rasmi katika hafla hiyo Kipi Warioba akizungumza mara baada ya kuwapokea wapandaji wa Mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining.
Washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengoo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia taasisi mablimbali zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wakifungua "champagne" kuonesha furaha mara baada ya kurejea salama kutoka katika kilele cha Mlima Kilimannjaro.
Washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia taasisi mbalimbali zinazojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa hafla ya mapokezi yao,Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba.
Watoto Yatima ambao ndio pekee walioshiriki katika changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro na kufika Kileleni wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba pamoja na viongozi wengine akiwemo Makamu wa Raisi wa kampuni ya Mgodi wa Geita Gold Mining,(GGM).

Makamu wa Rais wa Kampuni ya Mgodi wa Geita Gold Mining (GGM) Simon Shayo akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya mapokezi ya washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi.



Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.


DC MUHEZA AFANYA ZIARA HOSPITALI YA MUHEZA, AWATAKA WATUMISHI KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA

$
0
0

MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akipofanya ziara ya kuitembelea hospitali ya Teule kuangalia changamoto zinazoikabili kulia ni Mganga Mfawizi wa Hospitali hiyo,Malahiyo Rajabu katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza

Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo aliyekaa kulia kuzungumza na watumishi wa Hospitali Teule ya Muheza

Mganga Mfawizi wa Hospitali Teule ya Muheza Malahiyo Rajabu akizungumza jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye hayupo pichani wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali hiyo

Mganga Mfawizi wa Hospitali Teule ya Muheza Malahiyo Rajabu kulia akitoa ufafunuzi kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza wakati mkuu huyo wa wilaya alipofanya ziara kwenye hospitali hiyo

kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Mhandisi,Hajat Mwanasha Tumbo akisisitiza jambo kwa DMO wa wilaya ya Muheza wa pili kutoka kushoto Dkt Elias Mayala wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali Teule ya Muheza


Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo aliyevaa hijabu akiwa na baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Teule ya Muheza wakati alipofanya ziara kulia ni Mganga Mfawizi wa Hospitali hiyo Malahiyo Rajabu na anayefuata ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza



Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo wa pili kutoka kulia aliyevaa hijabu akipata maelezo kutoka kwa mhudumu wa zama katika hospitali Teule ya Muheza kushoto mara baada ya kufanya ziara ya kuitembelea anayefuatia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza



Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Teule Muheza Mkoani Tanga,Malahiyo Rajabu kushoto akitoa ufafanuzi kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kabla ya kuingia kwenye chumba cha maabara wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali hiyo

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo katikati akitembea hospitali ya Teule wilayani humo kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Malahiyo Rajabu kushoto ni DMO wa wilaya ya Muheza,Daktari Elius Mayala



Kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali Teule ya Muheza,Malahiyo Rajabu akimueleza jambo Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kuhusua namna wanavyofanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ambaye alifanya ziara ya kushtukiza ya kuitembelea hospitali hiyo Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

BRAND NEW MUSIC: KALA JEREMIAH ft. MIRIAM CHIRWA - WANANDOTO (OFFICIAL VIDEO)

VODACOM FOUNDATION YATUMIA BILIONI 15 KATIKA MIRADI YA JAMII NCHINI

$
0
0
Vodacom Tanzania imekuwa na kauli mbiu ya “Kufana maisha ya watanzania kuwa bora,sio kupitia huduma za mawasiliano pekee bali pia kusaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii kupitia taasisi yake ya kusaidia masuala ya kijamii ya Vodacom Tanzania Foundation.

Katika kipindi cha miaka 10 taasisi ya Vodacom Tanzania imekuwa ikifanya kazi na taasisi za serikali na wadau wengine kukabiliana na changamoto zinazowakabili wananchi wengi hususani katika sekta za elimu , afya na uwezeshaji wa kuinua makundi mbalimbali kiuchumi.

Kwa mujibu wa ripoti ya Vodacom Tanzania Foundation imebainishwa kuwa kuanzia mwaka 2006 hadi imetumia shilingi bilioni 15 kwa kufadhili miradi ipatayo 130 ya kijamii lengo kubwa likiwa ni kuleta mabadiliko kwa kuboresha maisha ya wananchi kwenye jamii.

Uboreshaji wa maisha ya wananchi umefanika kwa kutumia teknolojia ya mtandao wake kuboresha huduma mbalimbali na kuokoa maisha ya wananchi kupitia miradi mbalimbali.

Vodacom Tanzania Foundation imekuwa ikitumia teknolojia katika miradi ya kuboresha huduma za uzazi na kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga kupitia huduma ya kutuma na kupokea pesa ya ijulikanao kama M-Pesa.

Moja ya mradi huu wa kuokoa maisha ya akina mama wajawazito kupitia huduma ya M-Pesa unaendeshwa katika wilaya za Sengerema na mkoani Shinyanga ambao unafanika kwa kushirikiana na madereva wa teksi.Madereva waliosajiliwa katika mradi huweza kuwawahisha akina mama wajawazito katika vituo vya afya waonapo dalili za kujifungua ambapo madereva hao hupatiwa malipo yao kupitia simu zao za mkononi na umeonesha mafanikio makubwa ukiwa umeweza kuokoa maisha ya akina mama wajawazito na watoto wachanga wapatao 225 kwa mwezi.

Mradi mwingine ambao Vodacom Tanzania Foundation imeufankisha na umeleta mabadiliko makubwa ni mradi wa kutokomeza ugonjwa wa Fistula ambao imeuendesha kwa kushirikiana na taasisi ya Comprehensive Community Based Rehabilitation in Tanzania (CCBRT).

Kupitia huduma ya M-Pesa akina mama waliobainika kuwa na ugonjwa wa Fistula walikuwa wakilipiwa gharama za usafiri za kuwawezesha kufika katika hospitali ya CCRBT kupatiwa matibabu bila malipo na wakipona wanaripiwa gharama za kurejea makwao.Mradi huu umeweza kuwanufaisha akina mama wapatao 2, 482.

Kwa upande wa elimu ,Vodacom Tanzania Foundation imewezesha wanafunzi kutoka shule za msingi na sekondari kuingia katika ulimwengu wa kompyuta kwa kusaidia kuzipatia vifaa vya maabara za kompyuta ili waweze kusoma somo hilo kwa nasharia na vitendo.Kwa kushirikiana na kampuni ya Samsung imekuwa ikiendesha mradi wa Smart School ambao umekuwa na mafanikio makubwa na kuwanufaisha wanafunzi zaidi ya 8,000 kwa kupatiwa laptop ,vifaa vya kujifunzia kwa njia ya mtandao wa kidigitali na kuunganisha mtandao wa interneti mashuleni.

Afisa Mtendaji wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia amesema kuwa matumizi ya teknolojia ameboresha mabadiliko ya wananchi kuwa bora “Tumeshirikiana na serikali na wadau wengine kuboresha huduma za elimu,afya na kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi”.Baadhi ya miradi ambayo imeleta mabadiliko makubwa kwa jamii ni mradi wa kuwawezesha wasichana wa Hakuna Wasichoweza na mradi wa kuelimisha masuala ya afya na uzazi ujulikanao kama Wazazi Nipendeni.

Katika mradi wa Hakuna Wasichoweza ambao unatekelezwa kwa ushirikiano na shirika lisilo la kiserikali la T-MARC katika mikoa ya Lindi na Mtwara umefanikiwa kupunguza utoro kwa wasichana mashuleni uliokuwa unatokana na changamoto za vipindi vya hedhi kwa kutokuwa na vifaa vya kuwakinga na shule zao kutokuwa na miundombinu ya kuwawezesha kujiweka vizuri katika kubaliana na hali hiyo.

Kupitia mradi huu wasichana wanapatiwa elimu ya afya ya uzazi na kuwapatia taulo za kujihifadhi wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi na hadi sasa zaidi ya wasichana 5,000 wamenufaika na mradi huu.

Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation pia imekuwa ikishirikiana na serikali kupitia Wizara ya Afya katika miradi ya kufikisha jumbe za kuelimisha masuala ya afya bure kwa wananchi kupitia mtandao wa Vodacom na zaidi ya wananchi milioni 1 wanaendelea kunufaika na huduma hii.

Kwa kutumia bilioni 15 ndani ya kipindi cha miaka 10,taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation imeboresha maisha ya watanzania wengi na inaendelea kutimiza dhamira yake ya kuunga mkono jitihada za serikali za kupambana na changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii na kubadilisha maisha ya watanzania kutoka hali duni kuwa bora.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII AKUTANA NA VIONGOZI WA HIFADHI YA KISIWA CHA RUBONDO

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasilili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani ,akiviishwa vazi maalum (Boya) ambalo hutumika kujiokoa wakati uafiri wa maji unatumika.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Mhandisi Ramo Makani akiingia kwenye Boti kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Misana Mwishawa akimueleza jambo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani wakati akitembelea vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.



Mamba ni moja ya vivutio katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo ambayo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani alivutiwa kuwatizama.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akitizama vivutio mbalimbali wakati akizunguka na boti maalumu katika visiwa vilivyoko Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Missana Mwishawa akimuonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani eneo ambalo ni makazi na mazalia ya ndege katika moja ya visiwa vilivyoko katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mkuu wa wilaya ya Geita, Herman Kapufi alikuwa ni mmoja wa viongozi walioongozana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani kazika ziara hiyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akizunbgumza jambo mara baada ya kupata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Misana Mwishawa

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akitia saini katika kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika hoteli ya Asilia Lodge iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa akizungumza wakati wa kikao kifupi cha Naibu Waziri wa Utalii na Maliasili ,Mhandisi Ramo Makani na viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini,Joseph Kasheku (Msukuma) akizungumza wakati wa kikao hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Herman Kapufi akizungumza katika kikao hicho.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani akizungumza na viongozi wa serikali ikiwemo kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo alipokutana nao katika Hoteli ya Asilia Lodge.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani akizungumza na mmoja wa wageni katika Hoteli ya Asilia Lodge iliyopo katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Ugeni wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani ukipunga mikono kuaga wenyeji wao katika Hoteli ya Asilia Lodge ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

NAIBU WAZIRI WA AFYA AKUTANA NA UJUMBE WA VIONGOZI WA MFUKO WA ABBOTT

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akizungumza na viongozi wa mfuko wa Abbott (Abbott Fund) kutoka nchini Marekani na wale wa Tanzania waliomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es salaam kuzungumza naye kuhusu masuala mbalimbali ya uboreshaji wa huduma za Afya na Elimu kupitia program mbalimbali zinazofanywa na Mfuko huo nchini. Kutoka Kulia ni Makamu Mtendaji wa Rais wa Mfuko wa Abbott, Stephen Fussell na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa Abbott (Abbott Fund Bi.Elaine Leavenworth (katikati).
Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa Abbott (Abbott Fund) Bi.Elaine Leavenworth (kulia) akimweleza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) juu ya namna Mfuko wa Abbott ulivyojipanga kuendelea kutekeleza Program mbalimbali nchini Tanzania zikiwemo za Matumizi ya Teknolojia ya kisasa katika utoaji wa Tiba, maabara za kisasa, dawa na vifaa vya mafunzo kwa wanafunzi wa masomo ya Sayansi.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akifurahia jambo na Makamu wa Rais Mwandamizi wa Mfuko wa Abbott (Abbott Fund) Bi.Elaine Leavenworth (kushoto) mara baada ya ujumbe wa viongozi wa mfuko huo kutoka nchini Marekani kumtembelea Ofisini kwake jijini Dar es salaam.
Ujumbe wa viongozi wa mfuko wa Abbott (Abbott Fund) kutoka Marekani ukimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla mara baada ya kumtembelea Ofisini kwake leo jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbott (Abbot Fund) nchini Tanzania Andy Wilson akielezea utayari wa Mfuko huo katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazoikabili sekta ya Afya na Elimu nchini kupitia ufadhili wa Programu mbalimbali zinazofanywa na Mfuko huo kwa niaba ya Watu wa Marekani. Picha/ Aron Msigwa –MAELEZO.

ELIUD NYAUHENGA ATEULIWA KUWA KAIMU MENEJA MFUKO WA BARABARA

WIMBO MPYA WA INJILI KUTOKA KWA MWIMBAJI ELISHA WAUPENDO

$
0
0
Bonyeza HAPA Kusikiliza na Kupakua Wimbo Mpya wa Mwimbaji wa Muziki wa Injili nchini Tanzania, Elisha Waupendo. Wimbo Unaitwa Umenipa Kibali.  Pia waweza kuusikiliza ama kuupakua moja kwa moja hapa chini. Tafadhali sikiliza kwa umakini wimbo huo na utakuwa wa tofauti moyoni mwako.
Na BMG

RATIBA YA USAILI MAISHA PLUS EAST AFRICA 2016

$
0
0
Baada ya Usaili kufanyika kwa kishindo katika mikoa ya Mtwara na Dar es salaam usaili wa Maisha Plus unaendelea katika mikoa mingine ndani ya Tanzania. 
30/07/2016 - MBEYA - Ukumbi wa City Pub 
31/07/2016 - IRINGA - Savanna Garden 
02/08/2016 - DODOMA - Matei Lounge 
04/08/2016 - MWANZA - Rock Garden 
06/08/2016 - ARUSHA - Via Via
 13/08/2016 - ZANZIBAR - Ngome Kongwe 


Vijana wote wenye umri wa miaka 18 - 26 wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi. Elimu na ujuzi ni kiwango chochote. Zawadi kwa mshindi ni Tzshs. Milioni 30. Fomu zinapatikana BURE kabisa kupitia www.maishaplus.tv na katika maeneo tajwa hapo juu. 

 Maisha Plus East Africa 2016 | #VijanaNdioNgazi #HapaKaziTu
   

 Bofya hapa chini kuona video 33 fupi za usaili wa Maisha Plus Dar es salaam.

MAALIM SEIF KUONGEA NA WATANZANIA BOSTON

$
0
0
Zanzibar Diaspora Association inapenda kuwaalika kwenye mkutano wa hadhara utakao fanyika Siku ya Jumamosi July 30th -
MAHALI: 42 Charles St Boston
MA 02122.
MDA: Kuanzia 5:pm mpaka 7:pm
Mgeni rasmi ni Katibu mkuu wa CUF. 
Maalim Seif Shariff Hamad
Nyote mnakaribishwa

MAHAKAMA KUU YATUPILIA MBALI SHAURI LA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI JIMBO LA PANGANI

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)Jumaa Aweso katika akipongezwa na wananchi wa Jimbo la Pangani mara baada ya kutangazwa na Mahakama Kuu Kanda ya Tanga kuwa mshindi halali katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba mwaka jana mara baada ya kuonekana hakuna vigezo vya kutengua matokeo hayo katika kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CUF Amina Mwidau






Mbunge Aweso Jumaa akiwa amebebwa juu juu na wananchi wa Jimbo la Pangani mara baada ya kesi iliyofunguliwa dhidi ya mpinzania wake wa CUF Amina Mwidau ya kupinga matokeo ya uchaguzi kutupiliwa mbali na mahakama kuu kanda ya Tanga


Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)Jumaa Aweso wa pili kutoka kulia akiwa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini,Stephen Ngonyani "Proffesa Maji Marefu " wakiwa ndani ya Mahakama Kuu Kanda ya Tanga wakisuburia kuanzwa kwa kesi hiyo hata hivyo hukumu hiyo ilimpa ushindi halali Mbunge Aweso katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba mwaka jana mara baada ya kuonekana hakuna vigezo vya kutengua matokeo hayo katika kesi ya kupinga matokeo iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CUF Amina Mwidau



MAHAKAMA Kuu Kanda ya Tanga jana imetupilia mbali shauri la kupinga matokeo ya Ubunge Jimbo la Pangani lililofunguliwa na aliyekuwa mgombea kupitia tiketi ya CUF Amina Mwindau dhidi ya Mbunge wa Jimbo hilo Jumaa Hamidu Aweso CCM na kuonekana hakuna vigezo vya kutengua matokeo hayo. 

Akizungumza wakati akitoa huduma ya Shauri hilo,Jaji Patricia Fikirini alisema mlalamikaji Amina Mwindau CUF ameonekana kushindwa katika shauri hilo dhidi ya mlalamikiwa Jumaa Aweso katika upingaji wa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika oct 25 mwaka jana. 

Alisema miongoni mwa malalamiko yalioambatanishwa kutoka kwa mlalamikaji katika zoezi zima la kupinga matokeo hayo ni pamoja na kuwa mlalamikiwa ambae ni Jumaa Aweso katika kampeni zake alikiuka taratibu za uchaguzi,ubaguzi wa mgombea wa jinsia ya kike na kutumia lugha ya siziokuwa za kiungwana jambo ambalo mlalamikaji alidai lilimgharimu kupata matokeo mazuri katika uchaguzi huo. 

Alisema sambamba na vielelezo vilivyoletwa mahakamani hapo pamoja na ushahidi uliotolewa kwa upande wa mlalamikaji havikuwa na ushawishi wa kuweza kutengua matokeo ya uchaguzi huo.
Jaji Fikirini alisema amezingatia hoja zote kutoka pande mbili na kujiridhisha Jumaa Aweso ambae ni mbunge hivi sasa kuwa ni mbunge aliyepita kihalali na hakukuwa na vigezo vya upingwaji wa matokeo aliyopata katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. 

Alisema haki zote za kisheria zipo wazi kwa pande zote mbili mlalamikiwa na mlalamikaji ikiwa pamoja na kukata rufaa kwa maamuzi yaliyochukuliwa na Mahakam hiyo ikiwa kama kuna upande hauta ridhika na hukumu iliyotolewa. 

Kwa upande wake Wakili wa kujitegemea na mahakama kuu Warehema Kibaha alisema Jaji Patisia Fikirini amefanya maamuzi sahihi ya kutenda haki kwa mteja wake katika shauri hilo lililo dumu kwa takriban miezi 7.
Wakili Kibaha alisema katika shauri hilo walijiandaa kwa ushahidi na mashahidi wazuri ili kuweza kukabiliana na kesi hiyo jambo ambaloliliwawezesha kupata ushindi wa kihalali na kuweza kumpa nafasi mteja wake kuendelea na majukumu yake ya Kibunge.
Nae Wakili Mashaka Ngole aliyemsimamia Mlalamikaji Amina Mwindau alisema hana pingamizi lolote na atamsikiliza mteja wake ikiwa ataamua kukata rufaa wataangalia vigezo muhimu vitakavyo wasaidia katika awamu ya pili pindi watakapo kata rufaa hiyo Mbunge wa Jimbo la Pangani Jumaa Aweso ambaye alikuwa anakabiliwa katika shauri hilo alisema kipindi chote alichokuwa anakabiliana na kesi hiyo kulimpotezea umakinifu wa kufanya majukumu yake ya kibunge na kuweza kuangalia shida za wananchi wa Pangani kwa umakini zaidi. 

Aweso alisema kesi imekwisha na sasa kilichombele yake ni kupambana na kero za wananchi wa Wilaya hiyo ili kuweza kuwaletea maendelo kama alivyowaahidi kipindi cha kampeni.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
Viewing all 3497 articles
Browse latest View live