Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akutana na ugeni kutoka nchini Uturuki ukiongozwa na Balozi wao Dkt. Ali Daoutoglu mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam.
Ugeni huo umejadili namna yakuboresha Sekta ya Afya nchini hususani katika kuboresha huduma za dharura, uzalishaji wa dawa na ubadilishanaji uzoefu wa Wataalamu wa Afya kati ya nchi hizo mbili.
Balozi Ali Daoutoglu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tazania na ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano katika kuimarisha Sekta ya Afya nchini.