Quantcast
Channel: Matukio
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3497

MASKINI AUNTY EZEKIEL, ALA KICHAPO AKIJIRUSHA

$
0
0
Msanii wa filamu za Bongo, maarufu kama Aunt Ezekiel amepigwa na kuumizwa katika mkono wake wa kushoto alipokuwa Club Bilicanas katika utambulisho wa wasanii wa Bongo Fleva waliokuwa wakitambulishwa na Wema Sepetu.

Wema Sepetu ambaye pia ni msanii maarufu kati ya watu maarufu katika uwanja wa sanaa nchini Tanzania alitambulisha wasanii wapya wa muziki wa kizazi kipya katika ukumbi mkongwe na maarufu wa Bilicanas jijini Dar es Salaam siku ya jumapili.

Inadaiwa kuwa Aunt Ezekiel alipigwa chupa katika mkono wake na mtu asiyejulikana na kitendo hicho kuhusishwa na ugomvi wa mapenzi uliotokea siku za nyuma. Bi Ezekiel ameumiza vibaya katika mkono wake kwa kuchimbwa na kitu chenye ncha kali na kusababisha kidonda kikubwa kilichochimbika.

Kwasasa bi Ezekiel amelazwa akiuguza jeraha hilo.


PICHA ZOTE KWA HISANI YA MTANDAO

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3497

Trending Articles