Katika tukio lisilokuwa la kawaida na la kushangaza pengine laweza kuwa funga mwaka 2015, likiwa linarushwa moja kwa moja katika runinga ulimwenguni, mwanavichekesho maarufu duniani, Steve Harvey kw bahati mbaya alimvisha kimakosa taji la urembo wa ulimwengu (Miss Universe) Miss Columbia, Ariadna Gutierrez-Arévalo, mshindi wa mwaka 2015.
Kwa mujibu wa mtandao wa Yahoo, mkanganyiko huo ulitokea mwishoni katika tukio hilo la kimataifa ambapo Harvey alitakiwa kumtangaza mshindi wa pili (first runner-up, Ariadna Gutierrez-Arévalo) badala ya mshindi halali Miss Phillippines, Pia Alonzo Wurtzbach. Badala yake Hurvey akachemsha na kutaja jina tofauti.
Mara baada ya kutaja jina hilo watu wakainuka na kushangilia huku Gutierrez-Arévalo akipewa taji na rundo la maua. Lakini dakika chache baadaye watu walikumbwa na mshangao pale ambapo Miss Columbia akipunga mkono hakuchukua muda na furaha yake.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Wakati huo Wurtzbach aliangalia bila kuamini. Kisha akamsogelea Gutierrez-Arévalo na kusimama kama mshindi wa mwaka jana, Paulina Vega, akavua taji kichwani mwa Miss Columbia na kulivaa.
Hata hivyo Harvey, aliomba radhi katika mtandao wa Twitter, kwa watazamaji wa televisheni kwa kuandika “ningependa kuomba radhi kwa watazamaji katika hilo kwa kuwaangusha. Kwa mara nyingiine tena ni kosa la kibinadamu”